Saturday 29 October 2016

HADITHI ZETU!!!

MTU ALIYEKUWA TAJIRI NA HAKUBAHATIKA KUPATA MTOTO WA KUMFAA

Imesimuliwa na Ngwali Mashaka
Hapo zamani za kale alikuwepo bwana mmoja aliyekuwa akiitwa Hassan Saira.  Bwana huyo alikuwa ni tajiri sana kwa wakati wake. Vile vile alikuwapo mtu mmoja katika kijiji hicho ambae ni masikini sana bwana huyo alikuwa akiitwa Bwana Vuai Pandu. Bwana Hassan ni mtu mmoja wapo aliyepewa uwezo mzuri na Mwenyezi Mungu.
 Bwana huyo alioa na akapata mtoto mmoja wa kiume aliyeitwa Maulid. Mtoto wake huyo alikuwa ni mgonjwa, lakini moyo wake ulipenda amuozeshe na huenda ikawa bahati nzuri akapoa na kupata mtoto ambaye aliweza kumfaa babu yake. Bwana Hassan alikwenda kwa jirani yake Bwana Vuai Pandu ambaye alikuwa na watoto wengi wake na waume. Bwana Hassan alikwenda kuposa katika nchi moja wapo ya kifalme na kumwambia mzee Vuai kuwa mtoto wangu nimemposea lakini ni mgonjwa haifai kuonekana. Lakini nimekuja kwako unipe mtoto wako mmoja aitwae Yunus. Bwana Vuai alisema na kumwambia Bwana Hassan mimi mtoto wangu ni masikini jee atawezaji kufika kutoka nchi hizo za kifalme na akaonekane kuwa ni mtu? Bwana Hassan alijibu kuwa ataonekana kuwa ni mtu, usijali.
 Bwana Vuai alimuelezea mkewe Bibi Khadija kadhia hiyo. Bi. Khadija alimwambia mumewe jee haitakuwa taabu baada ya kwishakuoana, kwa sababu kila mmoja atakuwa anampenda mwenziwe?  Mzee Vuai alisema si tatizo nitamnasihi sana baada ya kurudi hapa tu kuwa amwache. Hapo alimwambia asili ya kukwambia hayo sisi hapa ni masikini tusipokubali anaweza hata kutufukuza, tutafanya nini?  Kwa hiyo ni bora tukubali.  Baada ya maneno hayo Bi Khadija aliridhika na Bwana Vuai alipeleka jawabu kwa Bwana Hassan Saira kuwa ameridhika kumpa mtoto wake. Na hapo ilifanywa safari, akasafi ri kwa meli, huku mtoto wa Bwana Vuai akapambwa na kuonekana ni mtoto wa mfalme. Pia askari walichukuliwa wakenda kwenye harusi. Mizinga ilisikika siku ile ya kupokewa bwana harusi na kukaribishwa wapite ndani ya kasri ya Mfalme. Gari nyingi za watu zilikuja katika sherehe hiyo na mtoto wa mfalme akachukuliwa na kufanyiwa kama ilivyo ada ya harusi na wafalme wote waliohudhuria walifurahi sana kwa kupata mchumba mzuri wa kifalme.
Baada ya hapo ilifanyika safari ya kurudi nyumbani ambapo alikabidhiwa watumishi mbali mbali, wa kike na wanaume. Mizinga ya harusi ya kurudi ilisikika na watu wote walikuja kumpokea harusi. Shangwe na vigelegele vilizagaa mtaani kwa Bwana Hassan Saira. Na walipofi ka maharusi nyumbani kwao watu walikaa na kushereheka usiku wa kucha.  Ilipofi ka siku ya pili Bwana Vuai alikwenda kuomba kuonana na mwanawe Yunus. Yunus hakupinga amri ya mzee wake na hapo Yunus akamuaga mkewe kuwa anakwenda kuangalia bustani zake na alitoka nje kwa muda mchache na hatimayae mtoto wa mfalme akaletewa mume mwengine na kuambiwa huyu ndie mumeo. Bi harusi alisema huyu siye mume wangu niletewe mume wangu na hapo alilia kwa muda mrefu na kilio kilizagaa katika nyumba mpaka watu wote wakatetemeka.
Aliitwa Bwana Hassan na kuelezwa kuwa Bi harusi hataki lolote na anataka kurudi kwao au aletewe mume wake kwani aliyeletewa siye mumewe halisi. Bwana Hassan alipofi ka mabibi wa nyumbani walimwambia utuletee mume wetu kwa haraka. Si hivyo tunakwenda zetu.  Ikabidi Bwana Hassan kusema kuwa huyu ndiye mume wako lakini bibi harusi akasema aitwe baba yake mzazi.  Bwana Hassan alipeleka barua ya ugonjwa ili kumrudisha kwao kwa sababu tu hataki kukaa na mume aliyekuwa siye aliyeozeshwa.
Mfalme alipopata barua na kufi ka kule nyumbani aliletewa mwanawe. Baada ya kuzungumza na watu wa nyumbani alihisi kuwa hana sifa ya ugonjwa. Hivyo bwana mfalme aliandika barua ya kumshitaki Bwana Hassan kwa kitendo alichokifanya ambacho si cha ukweli. Bwana Hassan alishitakiwa na kutakiwa kulipa fi dia kwa kitendo alichokifanya cha kuozeshwa mtu mgonjwa .
Bwana Hassan alikubali na kulipa fedha pamoja na masharti yote aliyopewa. Baada ya hapo mtoto wa mfalme alimwambia mzee wake kuwa alifanya hadaa tu kumletea mtu mzima na baadae kupewa mbovu, kwa hivyo mimi ninamtaka yule niliyeozeshwa mwanzo. Nina hakika bado kijana yule hajafa katika nchi ile, hivyo nikaozeshwe yule yule na niletewe mwenyewe.
Kwa kweli mfalme alisononeka sana kwa kitendo hicho kwa sababu mtoto wake alikuwa hali wala halali. Mfalme alitoa askari na kwenda kwa Bwana Hassan Saira na kumtaka apewe yule kijana aliyekuja kumuozesha mwanawe na wampeleke kule aliko mwana wa mfalme. Hapo Bwana Hassan alikwenda kwa Bwana Vuai na kumwambia kuwa mfalme amekuja na anamtaka yule kijana wako tumpelekee.
Lakini Bwana Vuai alimwambia Bwana Hassan kuwa mwambie mfalme aje mwenyewe na asitume askari. Baada ya hayo askari walipeleka ujumbe na mfalme akaja kutokana na shida ya mwanawe. Mfalme baada ya kufi ka kwa Bwana Hassan, akapelekwa kwa Bwana Vuai Pandu.  Bwana Vuai alitakiwa kumwita mtoto wake ili waende pamoja.  Walipofi ka alisema; „nasikia umetuma ujumbe kuwa nije mwenyewe nisitumize mtu yeyote, kwa hivyo tayari nimekwishafi ka.” Hapo Bwana Vuai alisema huyu ndie mtoto wangu alichukuliwa kwa hadaa ili kuozeshwa mtoto wako. „Jee wewe ukiangalia anastahiki kuchukuliwa kuja huko?”
„Unakuja kuchukua mtoto wangu, kutokana na umasikini tulio nao hebu twende ukaangalie nyumba yetu ilivyo tunavyoishi,” alisema. Mfalme alikubali hayo yote na baada ya kufi ka aliona nyumba yao na alimwambia warudi tena kwa Bwana Hassan. Na baada ya kufi ka aliamrisha aletewe yule motto aliyekuwa mgonjwa, kwa kweli mfalme alisikitika sana baada ya kuona hali yake. Baadae mfalme alizungumza na Bwana Vuai juu ya shida iliyompata kutokana na mtoto wake, hivyo ninakiri umasikini wako na kwamba nitakujengea nyumba yako na nitakusaidia kama ipasavyo lakini mtoto wako amuoe mtoto wangu, kwa sababu ninaridhika vya kutosha. Na hapo Bwana Vuai alikubaliana na mfalme na wakaandikiana mkataba kuhusu hayo waliyoyazungumza.

Ilipofi ka siku ya sita mfalme alifi ka na zana zote, na kuanza shughuli za ujenzi. Na baada ya siku kidogo nyumba ilimalizika na kwenda kufunga ndoa. Hapo tena baada ya ndoa mtoto wa mfalme alipoa matatizo yake na hatimae mtoto wa Bwana Vuai alipewa mali nyingi sana na mfalme na unyonge pamoja na umasikini waliokuwa nao awali ukaondoka na akawa wakati wowote anaruhusiwa kwenda kuwaona wakwe zake.

HADITHI!! HADITHII!!!

WIZI MBAYA

Imesimuliwa na Zubeda Abdalla Omar.
Hapo zamani za kale alikuwepo bwana mmoja, aliekuwa na wake watatu mmoja alikuwa mwizi. Yule
bwana alikuwa anafuga mbuzi, siku moja kati ya wale wake zake mmoja aliiba mbuzi na kumchinja na kumpika bila ya yeye kujua. Aliporudi safari yake aliuliza nani alimchinja mbuzi? Wote walikataa. Yule bwana akasema basi mimi nitafanya dawa. Wakajibu sawa, yule bwana akafanya mambo yake kisha akawapeleka mtoni. Walipofika aliwambia  mmoja mmoja aanze  kuingia mtoni na huku akiimba.
Aliingia wa kwanza huku akiimba nyimbo:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Alipomaliza kuimba akaibuka, kwani yeye hakuwa mwizi. Akafuata wa pili huku akiimba:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Yeye pia akaibuka na kukaa pembeni.  Akafuata yule wa tatu akaingia huku akiimba:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Lakini yeye alizama.
Kuona vile yule bwana akajua kwamba yule mke wa tatu ndie mwizi. Hapo akafanya dawa zake na yule bibi  akaibuka, alimuomba radhi mumewe na kuahidi kuwa  hatorudia tena kosa lake. Na yule bwana alikubali na wakaendelea kuishi kwa raha mustarehe.


DAMU NZITO KULIKO MAJI

Damu ni nzito kuliko maji

                




Methali: Damu ni nzito kuliko maji damu blood      maji - water Meaning: Blood is thicker than water.
Application: It is important to keep family ties last forever.
 

Friday 28 October 2016

THE TOP TEN SCHOOLS AND STUDENTS IN STANDARD SEVEN RESULTS 2016

Ufaulu kwa watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2016 umepanda kwa asilimia 2.52 kutoka asilimia 67.84 mwaka jana hadi asilimia 70.36, huku wavulana waking’ara katika matokeo hayo ambao wengi wametoka shule za Kanda ya Ziwa.
Matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk Charles Msonde ambaye alisema kati ya wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri katika mtihani huo, msichana ni mmoja tu, Justina Gerald wa Shule ya Msingi ya Tusiime ya jijini Dar es Salaam.
Kati ya wanafunzi hao 10, watahiniwa saba wanatoka Shule ya Msingi Kwema iliyopo mkoani Shinyanga, wawili Tusiime na mmoja kutoka Kaizirege ya Bukoba mkoani Kagera. 
Dk Msonde alisema jumla ya watahiniwa 555,291 kati ya 789,479 waliofanya mtihani huo wamefaulu kwa kupata jumla ya alama 100 na zaidi kati ya alama 250.
“Idadi hii ya watahiniwa waliofaulu ni sawa na asilimia 70.36, kati ya hao wasichana ni 283,751 na wavulana 271,540. Mwaka 2015 ufaulu ulikuwa ni asilimia 67.84 kuwapo ongezeko la ufaulu kwa asilimia 2.52,” alisema Dk Msonde.
Watahiniwa 16,929 wamepata daraja A, watahiniwa 141,616 wamepata Daraja B, watahiniwa 396,746 wamepata daraja C, watahiniwa 212,072 wakipata daraja D na 21,872 wakipata daraja E . 
Dk Msonde alisema ufaulu katika masomo ya Sayansi na Maarifa ya Jamii umepanda kwa asilimia kati ya 4.06 na 14.76 ikilinganishwa na mwaka 2015 huku masomo ya Kiswahili, Hisabati na Kiingereza ufaulu umeshuka kwa asilimia kati ya 0.39 na 12.51 ukilinganisha na mwaka jana.
“Watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili ambalo ufaulu wake ni asilimia 76.81 na somo walilofaulu kwa kiwango cha chini ni Kiingereza lenye ufaulu wa asilimia 36.05,” alifafanua Dk Msonde.
Dk Msonde aliwataja watahiniwa waliofanya vizuri na shule zao kwenye mabano kuwa ni:
  • Japhet Stephano, Jamal Athuman na Enock Bundala (Kwema),
  • Justina na Shabani Mavunde (Tusiime),
  • Jacob Wagine, Isaac Isaac, Daniel Kitundu na Benjamin Benevenuto (Kwema)
  •  Azad Ayatullah (Kaizirege).
Wasichana 10 bora:
  1. Justina Gerald (Tusiime)
  2.  Danielle Onditi (Tusiime)
  3. Linda Mtapima (Kaizirege),
  4. Cecilia Kenene (Mugini),
  5. Magdalena Deogratias (Rocken Hill),
  6. Asnath Lemanya (Tusiime),
  7. Fatuma Singili (Rocken Hill),
  8. Ashura Makoba (Kaizirege),
  9. Rachel Ntitu (Fountain of Joy),
  10. Irene Mwijage (Atlas)
Wanafunzi wavulana 10 bora kitaifa,
  1. Japhet Stephano (Kwema),
  2. Jamal Athuman (Kwema),
  3.  Enock Bundala (Kwema),
  4. Shabani Mavunde (Tusiime),
  5. Jacob Wagine (Kwema),
  6. Isaac Isaac (Kwema),
  7. Daniel Kitundu (Kwema),
  8. Benjamin Benevenuto (Kwema),
  9. Azad Ayatullah (Kaizirege)
  10. Benezeth Hango (Kwema).
Shule 10 bora ni:-
  1. Kwema (Shinyanga),
  2. Rocken Hill (Shinyanga),
  3. Mugini (Mwanza),
  4. Fountain of Joy (Dar es Salaam),
  5.  Tusiime (Dar es Salaam),
  6. Mudio Islamic (Kilimanjaro),
  7. Atlas (Dar),
  8. St Achileus (Kagera),
  9. Giftskillfull (Dar),
  10. Carmel (Morogoro).
Shule 10 ambazo hazikufanya vizuri ni:-
  1. Mgata (Morogoro)
  2. Kitengu (Morogoro)
  3. Lumba Chini (Morogoro),
  4. Zege  (Tanga),
  5.  Kikole (Tanga),
  6. Magunga ya Morogoro,
  7. Nchinila (Manyara),
  8. Mwabalebi (Simiyu)
  9. Ilorienito (Arusha)
  10. Chohero (Morogoro)
Mikoa 10 iliyoongoza kitaifa ni Geita, Katavi, Iringa, Dar es Salaam, Kagera, Mwanza, Kilimanjaro, Arusha, Njombe na Tabora wakati Halmashauri 10 bora ni Mpanda Manispaa, Geita Mji, Arusha Mji, Mafinga Mji, Chato, Mwanza Jiji, Moshi Mji, Mji Makambako, Ilemela na Hai.

WAHENGA WETU!!

Ganda la muwa la jana, chungu kaona kivuno 
Ganda la jana la muwa huwa limekauka, lakini chungu anapolipata huona ni mavuno maridhawa. Maana asiyezoea kuwa nacho, akipatapo hata kama ni kitu duni au hafifu namna gani na kidogo, hushangilia. Mathalani, kukengeuka kwa maadili kwa vijana barani Afrika na kuzamia tamaduni za kigeni.

Milima haikutani, lakini binadamu hukutana
Milima haina uwezo wa kukutana, lakini binadamu wakiwa hai huweza kukutana hata baada ya kuwa mbalimbali kwa muda mrefu. Hii ni methali inayotumika katika kutiana moyo wakati wanapoagana kwamba wakijaliwa watakutana. Pia hutumika katika kuwaonya watu kuacha tabia ya kuwatendea vibaya wengine kwani huenda wao pia wakatendewa hivyo siku za usoni. 

SHULE YA KWANZA KITAIFA

TAZAMA MATOKEO YA SHULE YA KWANZA KITAIFA MWAKA 2016 KATIKA MATOKEO YA DARASA LA SABA


Thursday 27 October 2016

Tuesday 25 October 2016

KNOWING GOD'S PRESENCE

KNOWING GOD'S PRESENCE
Who Is Pulling Me?
As I lay on my bed, I felt as if someone was pulling me off  the  mattress  and  onto  my  knees.  It  was  a  strange sensation, but I felt it so strongly I couldn't resist.
There I was, in the darkness of that room, on my knees.
God wasn't  through with me yet,  and I  responded to His leading.
I knew what  I wanted to say,  but I didn't  quite know
how to ask for it. What I wanted was what that minister in
Pittsburgh had. I thought, "I want what Kathryn Kuhlman's
got."  I  wanted it  with every atom and fiber  within me.  I
hungered for what she was talking about— even though I
didn't understand it.
Yes, I knew what I wanted to say but didn't know how
to say it. So I decided to ask the only way I knew—in my
own simple words.
I  wanted to address  the Holy Spirit,  but I  had never
done that before. I thought, "Am I doing this right?" After
all, I'd never spoken to the Holy Spirit. I never thought He
was a person to be addressed. I didn't know how to start the
prayer, but I knew what was inside me. All I wanted was to
know Him the way she knew Him.
And  here  is  what  I  prayed:  "Holy  Spirit.  Kathryn
Kuhlman says you are her  friend." I slowly continued, "I
don't think I know you. Now, before today I thought I did.
But after that meeting I realize I really don't. I don't think I
know you."
And then, like a child, with my hands raised, I asked,
"Can I meet you? Can I really meet you?"
I  wondered,  "Is  what  I'm saying  right?  Should  I  be
speaking to the Holy Spirit like this?" Then I thought, "If
I'm honest in this, God will show me whether I'm right or
wrong." If Kathryn was wrong, I wanted to find out.
After  I  spoke to  the  Holy Spirit,  nothing  seemed  to
happen. I began to question myself, "Is there really such an
experience  as  meeting  the  Holy  Spirit?  Can  it  truly
happen?"
My eyes were closed. Then, like a jolt of electricity, my
body began to vibrate all  over—exactly as it had through
the two hours I waited to get  into the church. It was the
same shaking I had felt for another hour once inside.
It was back, and I thought, "Oh. It's happening again."
But this time there  were no crowds.  No heavy clothes.  I
was just in my own warm room in my pajamas—vibrating
from my head to my toes.
I  was afraid to open my eyes.  This  time it  was as if
everything that happened in that service all rolled into one
moment.  I was shaking, but  at  the same time I again felt
that warm blanket of God's power wrapped all around me.
I felt as if I had been translated to heaven. Of course I
wasn't,  but  I  honestly  don't  believe  heaven  can  be  any
greater than that. In fact, I thought, "If I open my eyes, I'll
either be in Pittsburgh or inside the pearly gates."
Well,  after  a  time,  I  did  open  my  eyes,  and  to  my
surprise I  was right there in my same room.  Same floor.
Same pajamas.  But I was still  tingling with the power  of
God's Spirit.
When I  finally dropped off to sleep that  night,  I  still

didn't realize what had begun in my life.

Monday 24 October 2016

WHAT YOU WANT IN LIFE

THE IMPORTANCE OF KNOWING WHAT YOU WANT FROM LIFE

Most people never think about what they want in their lives. They live without this knowledge or forethought and become victims of their own circumstance. Work is just about a job – to get by financially. Life becomes a series of issues like choosing to live somewhere because therent is cheap, never understanding how to be in relationships or becoming ineffectual parents. The list goes on and on. Within yourself there is a craving for more. Is it substance, contact or a deeper understanding of life? No one has ever introduced such people to the concept of endless possibility. “As a man thinketh, so is he.”

A major key to manifesting the life you want is to ponder what you want out of life. What is it that you want to do with your life? A good exercise is to take a piece of paper and write down the answers to the following questions:

Ø What is my deepest desire?
Ø What would I like to accomplish in my life?
Ø What would I like to accomplish this year?
Ø Where would I like to be in 5 years?
Ø Where would I like to be in 20 years?
Ø What am I good at?
Look into all areas of your life:
Ø Your profession
Ø Your relationships
Ø Your health
Ø Your financial situation
Ø How you have fun (how you spend your holidays)
Think back to your childhood:
Ø What were the toys you liked to play with?
Ø What were you interested in?
Ø What did you like best to play?
Ø What presents did you wish to receive for your birthday and Christmas?
Ø What did you dream of becoming in your future?

Ask your Closest Friends
Tell your friends that you want to re-evaluate your talents and you need an honest opinion from them. Make sure to ask your friends to be 100% honest with you. Allow them to take a fresh look at you and ask them to forget all about what you are doing professionally – keep it on a personal level.
Ø What do your friends think you are good at?
Ø What do they think your talents are?
Ø What do they recommend what you should do with your life?

Ask Yourself a Few Questions
Take a notebook and read through these questions. Make sure you open up your mind and allow these questions to solidify in your imagination. Don't take these questions too seriously, play with them and also write down what comes up spontaneously – these are sometimes the most profound answers.

These questions are designed to expand your consciousness out of the normal mindset. The best solutions are always found outside the normal realm of thinking. Remember, your mind is part of the collective consciousness; therefore you have access to all information. Your mind is connected to the infinite source of all existence.
Ø  What would you do if you had enough money not to work ever again?
Ø  What were your dreams when you were younger?
Ø  What do you think is impossible for you to do?
Ø  What would you do if you won five million dollars?
Ø  What would you do if this was the last day of your life?
Ø  What would you do if you couldn't fail?
Ø  What are your strengths and talents?
Ø  Do you have a wish but don't know how to fulfill it?
Ø  What do you admire most about others?
Ø  What would your ideal lifestyle look like?
Ø  What does success mean for you?
Ø  What makes you really happy?
Ø  Is there anything that needs to be invented?
Ø  What does a perfect day look like for you?
Ø  What would you do if there were no restrictions?
Ø  What really excites you?
Ø  What would you be honored and recognized for?
Ø  Where do you see your life in ten years?
Ø  If you were immortal, what would you do with your life?
Ø  What needs to change to make this a better world?
Ø  What would you do if you were Superman?
Ø  What are you proud of?
Ø  What would you do if you were the President?
Ø  What would you like to accomplish this year?

Ø  What would you do differently if you could start over again?