Friday 26 January 2018

HADITHI SEHEMU YA NANE

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 08


Biashara ilimwendea vizuri, japokuwa hakuwa bosi lakini kwa kiasi fulani kila kitu kilikwenda kama alivyokuwa akitaka. Yeye ndiye alikuwa msafirishaji mkuu wa madawa hayo kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Aliaminika mno kwa kuwa kila mzigo aliokuwa akitumwa ulifika salama mikononi mwa mtu aliyekuwa akihitajika kuupata mzigo huo. Siku zikaendelea kukatika, akaanza kuwa na maendeleo makubwa lakini tatizo lilikuja pale alipoanza kufanya starehe.
Kiasi kikubwa cha fedha alichokuwa akikipata kutoka katika biashara zile, alikiweka katika mstari wa starehe zake. Kila siku Ethan alikuwa mtu wa kubadilisha wanawake na kubadilisha viwanja kiasi kwamba kiasi cha fedha alichokuwa akikipata wakati mwingine hakikutosha kabisa.
Alisahau alipotoka, alisahau kama kule Manhattan alipokuwa kulikuwa na rundo la watoto masikini, watu wasiojiweza ambao kila siku maisha yao yalikuwa pembeni ya mapipa ya takataka. Alisahau kila kitu, aalichokuwa akikifanya kwa wakati huo kilikuwa ni starehe tu.
Wanawake walimopapatikia kwa kuwa hakuwa mchoyo, alichokuwa akikipata aligawana nao na hivyo kutengeneza jina kubwa masikioni mwao. Siku zikakatika na kukatika mpaka pale aliposikia taarifa kwamba bosi wake aliyekuwa akimuweka mjini, bwana Sanchez alikuwa hoi kitandani.
Kilichomlaza kilikuwa ni saratani ya damu, alikuwa akiugua kila siku kwa kutokwa na damu puani na mdomoni. Ugonjwa huo ulimuanza kwa kasi hali ambayo ilimfanya kupelekwa hospitali ambapo madaktari wakawaambia ndugu zake kwamba asingeweza kupona.
“Hawezi kupona ugonjwa huu, ni lazima afe,” alisema daktari, aliamua kuwaambia ukweli kwamba mgonjwa waliyekuwa wamempeleka ilikuwa lazima afe.
“Hawezi kupona?”
“Hawezi. Ni lazima afe.”
Kansa yake ilisababishwa na ubwiaji mkubwa wa madawa ya kulevya, hakuwa na nafuu hata kidogo walichokifanya ndugu zake ni kumchukua na kumrudisha nyumbani kumuuguza katika kipindi cha mwisho.
Walipomfikisha huko, wakamfungia chumbani kwake. Hawakutaka kumuacha hata kidogo na hawakutaka kumficha juu ya kile alichokisema daktari kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kufa hivyo kama alitaka kufanya vitu vyake kwa mara ya mwisho, alitakiwa kufanya kwa wakati huo.
“Nitagawa utajiri kwa watoto wangu! Niitieni mwanasheria wangu,” alisema bwana Sanchez.
Mwanasheria wake akaitwa na kisha kuandika kile alichotakiwa kuandika, mirathi ikagaiwa kwa watoto wote. Kitu ambacho hakukiamini Ethan ni kwamba hakukuwa na mali yoyote aliyoachiwa japokuwa yeye alikuwa mtu wa karibu sana na mzee huyo.
Bwana Sanchez alipofariki hapo ndipo maisha yalipomgeukia, akaanza kurudi kule alipotoka, bisahara zikakata, mitego yote aliyokuwa ametega ikaharibika vibaya, marafiki zae ambao kila siku alifanya nao starehe wakamkimbia kwani waliona kwamba hakuwa na kitu tena.
Aliogopa kurudi New York katika mtaa aliozaliwa kwa kuhisi kwamba bado alikuwa akitafutwa sana, hivyo alichokifanya ni kukimbilia Texas, sehemu iliyokuwa na mpaka mkubwa wa kuingilia nchini Mexico.
Huku akiwa huko ndipo alipokumbuka kwamba mara ya mwisho alikutana na mzee mmoja ndani ya ndege ambaye alimwambia sana kuhusu biashara ile ya madawa kwamba haikuwa nzuri hivyo alitakiwa kuachana nayo.
“Namba yake niliiweka wapi?” alijiuliza.
Hicho ndicho kilichomuumiza kichwa wakati huo, hakukumbuka mahali alipoihifadhi namba ile, alikumbuka vilivyo kwamba alipewa na kurudi nayo nyumbani, baada ya hapo, hakukumbuka aliiweka wapi kwani kilipita kipindi kirefu mno na hata kumbukumbu zake zikawa zimepotea kabisa.
“Nilirudi nyumbani nikiwa nacho, nikakaa kitandani, baada ya pale nilikiweka wapi? Mhh! Hapana! Mbona sikumbuki vizuri?” alijiuliza lakini akakosa jibu.
Aliendelea kupigika mitaani, maisha yakampiga sana. Alipoona kwamba kila kitu kinakwenda kombo hapo ndipo alipoingia katika biashara ya kuuza magari, yaani walikuwa wakiiba magari nchini Marekani, wanayapitisha kwa njia za panya kuelekea Mexico na kuyauza huko.
Hakuwa na jinsi, japokuwa ilikuwa ni kazi ya hatari iliyohatarisha maisha yake lakini hakuwa na jinsi, alitakiwa kupambana ili atoke katika umasikini mkubwa uliompigia hodi mlangoni. 
“Ushawahi kuiba Lambonghin?”
“Hapana!”
“Sasa leo tunakwenda kuiiba, kama tukifanikiwa, sisi matajiri,” alisema jamaa yake, walikuwa wezi wakubwa hapo Texas.
“Hakuna noma, ila hatuwezi kukamatwa?”
“Tutakamatwa vipi? Kama tumewahi kuiba magari zaidi ya mia tano, tutakamatwaje kwa gari moja?” aliuliza rafiki yake huyo.
“Basi sawa. Lipo wapi?”
Huo ndiyo mpango waliopanga siku hiyo, walitaka kuiba gari ya thamani na kisha kuisafirisha kwa njia za panya mpaka nchini Mexico. Kuhusu kuiba, hilo wala halikuwa tatizo kabisa, waliweza kufanya hivyo ila kazi kubwa waliyokuwa nayo mahali hapo ni kulitoa gari hilo sehemu lilipokuwa na kulipeleka huko walipotaka kulipeleka.
Saa mbili usiku wakakutana karibu kabisa na ukumbi mmoja wa starehe, mbele yao kulikuwa na magari mengi lakini miongoni mwa magari hayo, kulikuwa na gari moja la thamani sana lililokuwa na gharama zaidi ya dola mioni tano, zaidi ya bilioni moja, ilikuwa lambonghin nyekundu iliyoonekana kuwa mpya kabisa.
Walikuwa wazoefu wa kuiba magari, hata kuiba gari hilo wala haikuwasumbua kabisa. Kwa sababu Ethan alikuwa mtaalamu mkubwa wa kuendesha magari, akakaa sehemu ya dereva, kwa kutumia utundu kwa kuunganisha nyaya, wakaunganisha na gari kuwaka, kilichobakia ni sauti za watu huko nyuma.
Hapo ndipo walipoanza safari ya kuelekea mpakani kwa njia za panya ili waweze kuliingiza gari hilo nchini Mexico. Walipanga kwamba huo ndiyo ungekuwa wizi wao wa mwisho hivyo baada ya hapo wangeacha kabisa kwani ilikuwa moja ya kazi ya hatari kabisa kuwahi kuifanya.
“Hivi unakanyaga mafuta kweli?” 
“Ndiyo!”
“Upo ngapi hapo?”
“180 kwa saa!”
“Gari mwisho ngapi?”
“400 kwa saa!”
“Sasa hizo nyingine unamuachia nani?”
“Ebwana tutakufa.”
“Kama kufa acha tufe, kuna raha gani ya kuishi, kama kufa tutakufa hata ukiendesha 1 kwa saa, kanyaga moto kaka,” alisema rafiki yake.
Mwendo aliokuwa akiendesha ulikuwa ni wa kasi mno, gari lilikuwa likijiweza kwa kasi hivyo Ethan hakuwa na jinsi, akaanza kukanyaga mafuta mpaka kuhisi kwamba gari hilo lingeweza kupaa. 
Kutokana na kuwa usiku mwingi, barabarani hakukuwa na magari kabisa, walitembea kwa mwendo waliotaka tena kwa kasi zaidi na baada ya masaa mawili walitaraji kufika karibu na mpaka huo ambapo wangechukua njia za panya na kuingia Mexico.
Wakati wamebakiza kilometa tatu kabla ya kuingia katika kituo cha mafuta cha Gapco, kwa mbali wakaanza kuyaona magari ya polisi yakiwa yamesimama barabarani huku taa zikiwaka.
Kwanza wakaogopa, kwa kasi waliyokuwa wakienda nayo walijua kwamba endapo wangeyagonga magari yale basi ingekuwa kifo chao hivyo alichokifanya Ethan ni  kupunguza kasi na kisha kuchukua barabara nyingine ya vumbi, magari yale ya polisi yakawashwa na kanza kuwafuata.
“Kanyaga mafuta!”
“Haiwezekani! Hakuna lami huku,” alisema Ethan.
Walikwenda na gari hilo kwa umbali mrefu mpaka mafuta yalipowaishia. Hawakuwa na jinsi, wasingeweza kubaki na wakati polisi waliendelea kuwasogelea kule walipokuwa, walichokifanya ni kuteremka na kisha kuanza kukimbia huku wakiwa wamelitelekeza gari lile.
Walikimbia kwa umbali mrefu, mbele kabisa wakakutana na korongo kubwa, lilionyesha kwamba mchana huwa kunakuwa na watu wanaochimba kokoto kutokana na ardhi ya Texas kuwa na kokoto nyingi, walichokifanya ni kuingia katika korongo lile na kuendelea na safari yao.
Hawakutaka kusimama sehemu yoyote ile, walichokuwa wakikitaka ni kufika walipotaka kufika pasipo kugundua kwamba polisi wale wa nyuma walipoona wezi wale kule walipokimbilia, wakawasiliana na polisi wa mpakani na kuwapa taarifa, nao wakaanza kusogea kule walipoambiwa wezi wale walipokimbilia, kwa maana hiyo, kadiri Ethan na rafiki yale walivyokuwa wakipiga hatua, ilikuwa ni sawa na kuwasogelea polisi hao waliotoka mpakani.


INAENDELEA...

HADITHIIII...........SEHEMU YA SABA

BIASHARA  YA KIFO

SEHEMU YA 7.

 “Ethan, stop,” (Ethan, acha) ilisikika sauti ya mama yake kutoka nyuma.
Ethan hakutaka kuiachia bunduki ile, alikuwa amedhamiria kumuua baba yake wa kambo, hakumpenda kabisa, alimchukia mno, kitendo cha kumuona kila siku katika maisha yake kilimkasirisha.
Alijiandaa kumfyatulia risasi na kumuua kabisa, lakini hata kabla hajafanya hivyo, mama yake akamsogelea na kisha kumzuia kubonyeza kitufe cha bunduki ile. Hiyo ikaonekana kuwa bahati ya mtende kwa mzee George, kwa jinsi alivyomwangalia Ethan, alikuwa amedhamiria kumuua kabisa.
Ethan akaondoka mahali hapo, kundi lile la watu lililokuwa limewazunguka nao wakaondoka kuendelea na kazi zao kama kawaida. 
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, alichukiwa na kila mtu kwa kuwa alikuwa mtemi, japokuwa alikuwa na miaka kumi na sita lakini tayari Ethan alijifunza maisha ya mitaani hasa ya kutumia bunduki katika maisha yake.
Alikuwa mtu wa fujo, alijulikana sehemu kubwa hapo Manhattan huku akianzisha kundi lake kubwa la kihuni lililojulikana kama The Mobb. Lilikuwa na vijana ishirini, walioshindikana katika maisha yao, walikuwa watumiaji wazuri wa bunduki, walikuwa wavuta bangi na hata wakati mwingine kutumia madawa ya kulevya.
Walikuwa vijana wadogo lakini wale ambao hawakuwa na huruma hata kidogo. Polisi wa hapo Manhattan waliliogopa kundi hili, hawakuyathamini maisha yao, kwao, kupigwa risasi na kufa lilikuwa jambo jema tu kwani waliamini kwamba kulikuwa na mungu wao wa kisela ambaye angewpokea nakuwaingiza katika mbingu yao iliyokuwa na makontena makubwa ya madawa ya kulevya na bangi.
Wakati kundi hilo likiendelea kukua, likiwapiga watu na hata wakati mwingine kuwaua, hapo ndipo walipotumwa polisi waliokuwa na hasira, polisi waliotoka nje ya Manhattan kwa ajili ya kufanya jambo moja tu, kuwakamata vijana hao na hata kama wataleta ubishi au kufanya chochote kilicho kibaya cha kuhatarisha maisha yao, basi wawaue.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kumaliza magenge hayo, vijana wengi walikamatwa na kufungwa gerezani lakini kwa Ethan, akatoroka jijini New York na kuhamia Washington DC ambapo maisha yake yakaendelea.
Hakutaka kuwa mhuni kama alivyokuwa, hakutaka kufanya usela wa mitaani alichokifanya kwa wakati huo ni kujikita katika uuzaji wa madawa ya kulevya kwa kuyasafirisha sehemu moja kwenda nyingine. 
Hapo ndipo alipokutana na wale watu aliokuwa akiwasikia kwamba walikuwa wauzaji wazuri wa madawa ya kulevya na walikuwa watu wenye kuogopwa sana. Alipofikishwa kwa mzee mmoja aliyekuwa na asili ya Mexico, mzee Sanchez El Paso, akamchukua na kumfanya mfanyakazi wake ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kusafirisha madawa nchini Marekani.
“Ukifanya kazi na mimi, utakuwa tajiri mno,” alisema mzee Sanchez.
“Nitatajirika vipi?”
“Utafahamiana na watu wengi, nisingependa ufanye kazi kwangu milele, pia ningependa baadaye ufanye kazi wewe kama wewe,” alisema mzee Sanchez.
“Ili nifikie ndoto ya kufanya biashara zangu mwenyewe, natakiwa kufanya nini?”
“Kujitoa kazini, hakuna cha zaidi, ila epuka sana wizi, ukiiba na kugundulika, nitakuua,” alisema mzee huyo maneno yaliyomtia hofu mkubwa.
“Siwezi kufanya hivyo! Umenitoa mbali, hakika nitaendelea kukuheshimu na sitokufanyia ujinga,” alisema Ethan.
Alimheshimu mzee huyo kwa kuwa ndiye aliyekuwa akimfanyia mambo mengi na kukutana na watu ambao hakutegemea kukutana nao katika maisha yake. Kila siku alikuwa mtu wa kutoka, hakutulia sehemu moja, leo alikuwa akienda California, kesho Texas na kesho kutwa sehemu nyingine.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, kila siku alikuwa akibadilisha muelekeao wake ambapo kote huko kazi kubwa aliyokuwa akiifanya ni kusafirisha madawa ya kulevya tu. Jina lake likaanza kukua, mnyororo mkubwa aliokuwa nao mzee Sanchez ukamsaidia mno na hata katika viwanja vya ndege mbalimbali hakuwa akipata usumbufu wowote ule.
“What do you want?” (Unataka nini?) aliuliza mzee mmoja.
“What do I want? What do you mean?” (Nahitaji nini? Unamanisha nini?)
“For how long have you been doing this work?” (Kwa kipindi gani umekuwa ukifanya kazi hii?)
“Three years?” (Miaka mitatu)
“Ok!” (Sawa)
Alikuwa akizungumza na mzee mmoja aliyekuwa amekaa naye ndani ya ndege. Hakujua ni nani alimwambia kuhusu biashara ya madawa ya kulevya aliyokuwa akiifanya, mzee huyo alianza kumuuliza maswali mengi kiasi kwamba akaanza kuogopa kwani hata humo ndani ya ndege alipokuwemo, alikuwa na mzigo mkubwa aliokuwa akiupeleka Los Angeles.
“Lakini wewe ni nani?” aliuliza Ethan huku akionekana kushikwa na hofu.
“Ninaitwa Boyle Cook,” alijibu mzee yule.
“Umejua vipi kama ninafanya kazi hii?”
“Hauwezi kunificha, ninawajua kwa kuwaangalia, umekuwa na amani katika kufanya kazi hii?” aliuliza bwana Cook.
“Kiasi, si sana, wakati mwingine unakuwa na hofu kubwa.”
“Utakuwa tayari kama nikikupa kazi nyingine, nzuri tu?”
“Kazi gani?”
“Ninataka uwe na amani, siwezi nikakupa kazi ngumu. Niambie, upo tayari?” aliuliza bwana Cook.
“Mmmh!”
“Usijali! Chukua hii, ukiwa tayari niambie,” alisema bwana Cook na kisha kumpa business card yake iliyokuwa na mawasiliano yote.
Mpaka kufikia hatua hiyo Ethan alichanganyikiwa, alikuwa akimwangalia mzee huyo mara mbilimbili, hakumfahamu alikuwa nani, hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana naye, tena walizungumza kwa muda mchache kabla ya mzee huyo kubaki kimya mpaka ndege ilipotua Jijini Los Angeles na kisha kuteremka.
Hawakuzungumza chochote kile, kila mmoja akaendelea na kazi zake zilizomleta ndani ya jiji hilo la starehe. Ethan akaondoka na kupeleka mzigo alipoelekezwa kwani hata kuutoa pale uwanja wa ndege hakukuwa na kazi kubwa kwani kila kitu kiliwekwa tayari.
Kichwa chake kikawa na maswali mengi, alikuwa akijiuliza kuhusu mzee yule ambaye alionekana kumfahamu mno, hakuishia hapo, aliendelea kufikiria hata ile kazi aliyotaka kumpa, hakujua ilikuwa kazi gani ila alimwambia kwamba endapo angekuwa tayari basi amtafute.
Uuzaji wa madawa ya kulevya ilikuwa biashara mbaya na yenye hatari mno lakini hakutaka kuiacha kwani ilimpa kisasi fulani cha fedha na kuanza kuyabadilisha maisha yake. Alichokifanya ni kumpuuzia bwana Cook na yeye kuendelea na maisha yake kama kawaida ingawa mara nyingi mno alikuwa akijiuliza kuhusu mzee yule na kukosa jibu.


INAENDELEA...

Wednesday 24 January 2018

HADITHI!!!......SEHEMU YA SITA

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 06


Maisha yaliendelea kama kawaida. Hakukuwa na kitu kilichokisumbua kichwa cha padri Benedicto kama kumuona mzazi mwenzake akiishi mbali naye. Hakuwa na uwezo wa kwenda kukaa naye lakini kila siku alikuwa mtu wa kutamani kumuona mwanamke huyo akiwa karibu naye kwani ndiye mtu pekee aliyeonekana kuwa faraja katika maisha yake.
Kutokana na mapenzi mazito aliyokuwa nayo juu yake, muda wote alihisi kwamba alikuwa akiibiwa tu. Aliwafahamu vijana wa Sinza, walikuwa vijana makini kuhusu masuala yote ya mapenzi, walikuwa na uwezo mkubwa wa kumteka msichana yeyote hata kama angekuwa mgumu kiasi gani.
Hakutaka kusalitiwa, alitaka Irakoze awe wake peke yake, hivyo alichokifanya ni kuanza kupanga mipango kabambe ya kumbana mwanamke huyo kwa kumpeleka katika Chuo cha Utawa,  St. Mary’s Catholic kilichokuwa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam na kuingia pale kama mpishi.
Mipango yote ya Irakoze kuingia ndani ya chuo kile ilifanywa na padri Benedicto huku akimchukua Annabel na kumpeleka nchini Marekani kwa ajili ya kusoma huko katika Shule ya Consolatha Seminary School iliyokuwa katika Jiji la New York nchini Marekani.
Kidogo moyo wake ukawa na amani, kutokana na umbo lake kuwa dogo na sura ya kitoto aliyokuwa nayo, mara baada ya kufika katika chuo hicho cha Utawa, masista wote walihisi kwamba Irakoze alikuwa msichana mdogo, hivyo wakamchukulia hivyohivyo.
Kila siku alikuwa hapo huku akiwasiliana na padri Benedicto simuni, bado wawili hao waliendelea kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa siri sana kiasi kwamba hakukuwa na mtu yeyote aliyefahamu kilichokuwa kikiendelea.
Huo ulikuwa mwaka wake wa kwanza chuoni hapo, alionekana kuwa mtu mwenye heshima, alimheshimu kila mtu kuanzia wale wa chini mpaka wa juu. Wasichana wengi waliokuwa chuoni hapo walimpenda Irakoze ambaye walipenda kumuita kwa jina la Sista Magdalena.
Siku zikaendelea kukatika, kila alipokuwa akitumwa mjini kwa ajili ya kununua baadhi ya vitu kwa ajili ya shule hiyo, alikuwa akienda na kuonana na padri Benedicto na kisha kulala wote hata kwa masaa mawili kisha kurudi chuoni.
Huko ndipo alipopata taarifa kuhusu binti yake aliyekuwa nchini Marekani. Masomo yaliendelea vizuri na mara kwa mara safari za Benedicto kuelekea nchini Marekani hazikuisha, kila alipokwenda, alihakikisha anaonana na binti yake na kisha kurudi nchini Tanzania.
“Amekua sana, mwaka wa sita huu,” alisema Benedicto, alikuwa akimwambia Irakoze.
“Nina kiu ya kumuona.”
“Usijali! Ila nataka tuifanye kitu kimoja”
“Kipi?”
“Na wewe usomee utawa!”
“Mmmh!”
“Hakuna tatizo! Utafanikiwa tu, nataka uwe na safari za kutosha kwenda Ulaya na sehemu nyingine,” alisema Benedicto.
“Sawa! Hakuna tatizo!”
Hilo ndilo walilokuwa wamekubaliana, ilikuwa ni lazima Irakoze aanze kusomea utawa ndani ya chuo hicho alichokuwa akifanya kazi kama mpishi. Hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu tayari alikwishafanya kazi hiyo kwa miaka mitatu, akachukuliwa na kuanza masomo moja kwa moja.
Kila siku alikuwa akiamka asubuhi na mapema kama wanachuo wengine na kisha kuelekea kanisani ambapo walisali kisha kujiandaa na masomo kama kawaida. Japokuwa hakuwa amesoma sana kipindi cha nyuma lakini uwezo wake wa kawaida ulitosha kabisa kuonyesha kwamba kama angeendelea zaidi basi angeweza kufanikiwa sana katika maisha yake.
Aliishi kama mtumishi wa Mungu, kila wakati alikuwa mtu wa kusali huku rozali ikiwa shingoni mwake. Kila mtu alimheshimu na alipoonekana kwamba yeye ndiye alikuwa mcha Mungu mkubwa kuliko wengine, wakampa uongozi wa bweni pasipo kujua kwamba mwanamke huyo alikuwa na mtoto ambaye alikuwa akisoma nchini Marekani.
Padri Benedicto hakuacha, kwa kuwa katika kila hatua aliyokuwa akipitia Irakoze ilikuwa chini yake, hivyo alihakikisha kwamba hata kwenda nje ya chuo hicho linakuwa jambo jepesi ili mradi mwisho wa siku aweze kuonana naye na kufanya mambo yao.
Alichokifanya ni kukaa chumbani na kuandika barua, alikuwa akiuandikia uongozi wa chuo hicho kwamba kutokana na heshima aliyokuwa nayo Irakoze, aliruhusiwa kila Jumapili kwenda kusali nje ya chuo hicho.
Nafasi hiyo haikutolewa mara kwa mara, ilitolewa mara chache sana tena kwa wanachuo walioonekana kuwa na nidhamu ya hali ya juu. Kwa Irakoze hakukuwa na mtu aliyeonekana kuwa na wasiwasi, jinsi nidhamu yake ilivyokuwa chuoni hapo, ilimfanya kila mmoja kukubaliana na padri Benedicto kutokana na jinsi alivyokuwa chuoni hapo.
Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi nyingine na waliitumia vilivyo kuwa pamoja. Kila kitu kilichokuwa kikifanyika kiliendelea kuwa siri kubwa. Baada ya miaka miwili kukatika, hatimaye aliyekuwa Kardinari wa Kanisa la Kiroma nchini Tanzania, Paulo Alonso akafariki dunia na hatimaye barua kuandikwa kutoka Vatican kwamba Padri Benedicto alitakiwa kutawazwa na kuchukua nafasi hiyo kwani kwa sifa zote za kuwa kardinari alikuwa nazo.
“Lakini kwa nini apewe padri? Kwa nini asipewe askofu?” maaskofu waliulizana tu.
“Hata sisi hatufahamu, ila kwa sababu ni barua iliyoletwa kutoka Vatican, hatuna budi, acha tukubaliane nayo,” alisema askofu mmoja.
Baada ya wiki mbili, padri Benedicto alitakiwa kuelekea nchini Vatican kwa ajili ya kutawazwa na hatimaye kuwa kardinari mkubwa nchini Tanzania. Hiyo ilikuwa nafasi yake pekee, moyo wake ulikuwa na furaha kubwa, hakukuwa na kitu kilichowahi kumpa furaha maishani mwake kama kipindi hicho.
Suala la kuwa na mtoto liliendelea kuwa siri yake, hakutaka mtu yeyote afahamu na alikuwa akijitahidi kufanya kila liwezekanalo kusiwe na mtu yeyote anayelifahamu hilo. Kwenye kila mwaka, alikuwa akimtumia mtoto wake Annabel kiasi cha fedha kwa kutumia akaunti nyingine kabisa iliyosomeka kwa jina la Andrew McDonald, raia kutoka nchini Kenya.
Japokuwa Annabel katika kipindi hicho alikuwa na miaka kumi, lakini aliendelea kufichwa kwamba baba yake alikuwa padri ambaye katika kipindi hicho alitarajiwa kutawazwa na kuwa kardinari nchini Tanzania.
“Unataka kuwa nani ukikua?” aliuliza Benedicto.
“Nataka kuwa mwanasheria.”
“Kwa nini usiwe sista?”
“Sitaki! Nitataka niolewe. Nimesikia kwamba sista haolewi! Kweli baba?”
“Ndiyo!”
“Basi mimi nataka kuwa mwanasheria, ninataka kuolewa baadaye!”
Alikuwa akizungumza na binti yake katika kipindi alichokwenda kumtembelea nchini Marekani. Japokuwa alikuwa nchi nyingine lakini kofia aliyokuwa ameivaa haikutoka kichwani mwake. Shule hiyo aliyompeleka binti yake kusoma ilimtunza vizuri, alipata malezi yote na hakukuwa na shida sana kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akifika hapo na kumuona.
Annabel alikuwa binti mzuri, mwenye sifa zote za kuitwa mrembo. Alichanganyikana, alikuwa na sura ya baba yake lakini pia alikuwa na sura ya mama yake. Watu wengi waliokuwa wakimuona, walikiri kwamba binti huyo angekuja kutikisa sana siku za usoni kutokana na urembo wake huo.
“Baba!”
“Naam!”
“Unafanya kazi gani?”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Kwani sijawahi kukwambia binti yangu?”
“Hapana! Hukuniambia!”
“Mimi ni mfanyabiashara binti yangu, huwa nasafirisafiri sana,” alijibu Benedicto.
“Kweli baba?”
“Ndiyo! Nikitoka hapa, nakwenda Dubai, nikuletee zawazi gani nikija?”
“Chochote upendacho baba, nitafurahi!” alisema Annabel.
Benedicto hakuwa na jinsi, ni kweli alimpenda binti yake lakini kulikuwa na vitu ambavyo hakutakiwa kuwa mkweli kabisa, alimdanganya kwamba alikuwa mfanyabishara kwa kuwa hakutaka ajue kwamba alikuwa padri ambaye hakutakiwa kuoa au kuwa na mtoto yeyote yule.
Kwake, bado lile liliendelea kuwa siri kubwa, kila siku lilimuumiza moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi, alikubaliana na kila kitu kilichokuwa kiiendelea, na hata kama alifanya dhambi, aliamini kwamba hakukuwa na mwanadamu aliyekuwa mkamilifu mbele za Mungu.
Baada ya siku tatu, akarudi nchini Tanzania ambapo moja kwa moja akawasiliana na Irakoze na kumwambia kuhusu mtoto wao na ndoto aliyotaka kuwa nayo katika maisha yake.
“Kakataa kuwa sista?”
“Amekataa!”
“Daaah! Ngoja niende, nitazungumza naye,” alisema Irakoze.
“Hakuna tatizo!”
Japokuwa aliamini kwamba binti yake angeweza kumsikiliza na hatimaye kukubaliana nao kuwa sista lakini hilo halikuwezekana, bado msimamo wa Annabel ulikuwa ni kuwa mwanasheria mkubwa duniani.
Hakukuwa na mtu aliyemzuia, waliachana naye, aendelee na maisha yake na mwisho wa siku kukamilisha kile alichokuwa akikitaka.
Wakati Annabel akifikisha miaka kumi na sita, alionekana kuwa binti mrembo mno, kipindi kirefu cha maisha yake alikitumia nchini Marekani, hakuwahi kurudi nchini Tanzania, aliondoka huko miaka mingi iliyopita, tangu alipokuwa na miaka minne.
Hakufahamu sehemu yoyote nchini Tanzania, hakufahamu mitaa na hata watu wa huko walikuwa na utamaduni gani. Baada ya kufikisha miaka hiyo, hakutaka kukaa nchini Marekani, alitaka kuwa na muda wa kurudi nchini Tanzania ili aweze kukaa na wazazi wake ambao hakuwahi kukaa nao hata siku moja.
Alitaka malezi yao, alichokifanya ni kuwasiliana nao, hawakuwa najinsi, wakajipanga kwamba mara binti yao atakapofika nchini Tanzania, wampelekea katika nyumba yao nyingine iliyokuwa Kisarawe, pembezoni mwa Jiji la Dar es Salaam ambapo waliamini kwamba hakukuwa na watu wengi.
Siku ya safari ilipofika, Annabel akaingia ndani ya ndege tayari kwa kurudi nchini Tanzania. Hapo Marekani akapanda ndege ya Shirika la Ndege la American Airlines ambayo ilikuwa ikifanya safari mpaka nchini Uingereza, Italia na baadaye kuelekea Uholanzi ambapo huko wangebadilisha ndege na kuelekea Dubai, kisha India na Kenya jijini Nairobi na kuingia nchini Tanzania kabla ya kuelekea Afrika Kusini.
Baada ya abiria kutakiwa kuingia ndani ya ndege hiyo, Annabel akasimama na kuanza kuelekea ndani ya ndege hiyo. Kwa muonekano, alionekana kuwa binti mkubwa, mrembo, mwenye mvuto ambaye alivutia sana, kila mwanaume aliyemwangalia, alitamani kuwa na msichana mrembo kama alivyokuwa.
Wakati ameingia ndani ya ndege hiyo na kukaa katika viti vya watu wawili, akaja mwanaume mmoja, alionekana kuwa kijana mtanashati, aliyependeza, alivalia suti ya gharama, muda wote uso wake ulionekana kuwa na tabasamu pana, alimuona Annabel, tabasamu likaongezeka usoni mwake.
“How are you cute,” (Habari yako, mrembo) alimsalimia Annabel.
“I’m fine, you are welcome,” (Salama, karibu) alimkaribisha mwanaume yule aliyejitambulisha kwa jina la Ethan Dylan.

INAENDELEA...                        

HADITHI!!!!! HADITHI SEHEMU YA TANO

BIASHARA YA KIFO
sehemu ya 05

Kwa kumwangalia usoni tu, padri Benedicto alionekana kuhitaji msaada, alitia huruma mno, macho yake alikuwa ameyapeleka usoni mwa Irakoze huku akionekana kuwa na hofu kubwa. Kile alichokuwa amekifanya kilikuwa ni kinyume na sheria za kanisa hilo hivyo kama kanisa lingejua kile kilichokuwa kimetokea, lingekuwa tatizo kubwa.
Hakukuwa na mtu ambaye angeweza kumsaidia katika kipindi hicho zaidi ya msichana huyo. Alizungumza naye kwa kipindi kirefu, tena kwa unyenyekevu mkubwa na mwisho wa siku akamwambia ukweli kwamba alitakiwa kuondoka mahali hapo.
“Niende wapi?”
“Popote pale, ili mradi utoke ndani ya nyumba hii,” alisema padri Benedicto.
“Kwa hiyo unanifukuza?”
“Hapana! Sikufukuzi.”
“Ila?”
“Nitakupangia chumba, utakwenda kuishi huko mpaka utakapojifungua, nakuahidi kukusaidia kwa kila kitu,” alisema padri Benedicto.
“Una uhakika?”
“Ndiyo!”
Hicho ndicho walichokubaliana, padri hakutaka Irakoze abaki nyumbani hapo kwa kuhofia kwamba watu wangeweza kujua kwamba alikuwa mjauzito na hivyo mwisho wa siku kumletea matatizo, alichokifanya ni kumwambia aondoke nyumbani hapo huku akimgawia kiasi cha shilingi milioni moja.
Kabla ya kuondoka kwanza akaanza kutafuta chumba ambacho alikipata maeneo ya Sinza Makaburini, huko ndipo alipoanza maisha yake. Alikuwa akihudumiwa kila kitu na padri huyo, kuanzia chakula, mavazi, vitu vya ndani na mambo mengine mengi.
Alipewa kiasi cha shilingi milioni moja kila mwezi kitu kilichompeleka kuanza kufanya biashara zake binafsi, japokuwa zilikuwa ndogondogo lakini akafanikiwa kwa kiasi kikubwa kuyaendesha maisha yake.
Katika kipindi hicho cha kwanza tumbo lake halikuwa likionekana lakini baada ya miezi kadhaa kupita, kila mtu aliyekuwa akimwangalia alijua kwamba msichana huyo alikuwa mjauzito.
Padri Benedicto akawa akifika sana nyumbani hapo nyakati za usiku tena huku akiwa amevalia kofia kubwa ili asiweze kujulikana. Kila kitu kilichokuwa kikiendelea, kilikuwa siri kubwa mno kiasi kwamba hakukuwa na mtu aliyefahamu ukweli.
Baada ya miezi tisa kukatika, hatimaye Irakoze akajifungua mtoto wa kike aliyempa jina la Annabel kama ambavyo padri Benedicto alivyotaka aitwe na hivyo maisha yake na mtoto wake kuanza.
Padri huyo hakukata mguu nyumbani hapo, kila alipomuona Annabel, moyoni mwake alijisikia furaha mno, hakuamini kama mwisho wa siku na yeye alifanikiwa na kuitwa baba. Moyoni mwake alijiona kuwa mwanaume wa shoka, alijikubali japokuwa sheria ya kidini ilimkataza kuwa na mwanamke yeyote, kuona au kuzaa mtoto.
Siku zaikaendelea kukatika, hakuacha kufika nyumbani hapo, aliendelea kumlea Irakoze na mtoto wake na baada ya miaka mitatu kupita huku akiwa amekwishaanza kumjengea nyumba Irakoze maeneo ya Mbezi Beach, hapo ndipo alipoamua kumwanzisha Annabel Shule ya Chekechea ya Antonino iliyokuwa Mbezi Beach ambapo wanafunzi wengi walisoma shuleni hapo walikuwa ni wale waliotoka katika familia za kitajiri.
Mwaka uliofuata ambapo Annabel aliingia mwaka wa nne hapo ndipo alipoanza kumsumbua mama yake kuhusu baba yake. Kila siku alikuwa mtoto wa kulia tu, hakukuwa na kitu alichokuwa akikitamani wakati huo kama kumuona baba yake tu.
“Mama nataka kumuona baba.....” alisema Annabel kwa sauti ya chini huku akilia.
“Baba yako atakuja.”
“Lini?”
“Kesho! Twende shule kwanza.”
“Sitaki kwenda mpaka nimuone baba.”
“Atakuja tu mwanangu! Twende shule kwanza.”
Japokuwa aligoma kwenda shule lakini Irakoze hakuwa na jinsi, alimlazimisha Annabel mpaka akakubali kwenda shuleni. Njiani, alikuwa akilia tu, hakunyamaza, kila walipofika bado alikuwa akilia kumuona baba yake.
Hicho kilimuumiza sana Irakoze, kila aliposikia kwamba binti yae mzuri akimuulizia baba yake, moyo wake ulimuuma mno. Hakuwa na jinsi, alimpigia simu padri Benedicto na kumwambia ukweli kwamba binti yake alitaka kumuona, hivyo alitakiwa kufanya kila awezalo aje kumuona.
“Nitakuja.”
“Lini?”
“Sijajua! Ila nitakuja hivi karibuni.”
“Unajua mtoto wako anasumbua sana, siku hizi hata kula hataki!”
“Kisa?”
“Anataka kukuona wewe!”
“Aiseee! Nitakuja basi.”
“Lini?”
“Kesho usiku!”
“Sawa!”
Siku iliyofuata usiku, padri Benedisto alikuwa mahali hapo, kitu cha kwanza kabisa alitaka kumuona binti yake. Japokuwa mara kwa mara alikuwa akifika na kumuona lakini siku hiyo Irakoze akaamua kumwambia Annabel kwamba yule alikuwa baba yake.
Annabel akafuata na kumkumbatia, alionekana kuwa na furaha sana na hakutaka kutoka mikononi mwa baba yake. Kila alipomwangalia binti yake, alifanana naye sana, alijifariji sana, japokuwa sheria hazikutana padri kuwa na mtoto lakini kwake ilionekana kuwa furaha kubwa. 
Kuanzia siku hiyo, mara kwa mara alikuwa akifika nyumbani hapo huku akimkataza Irakoze asimwambie Annabel kama alikuwa padri kuepuka matatizo hapo baadae. Hilo wala halikuwa tatizo, Irakoze akakubaliana naye kwamba jambo hilo liendelee kuwa siri siku zote.

“I will kill you, bullshit,” (Nitakuua kinyesi cha ng’ombe)
“Do you really want to kill me?” (Unataka kuniua?)
“Yes!” (Ndiyo!)
“Ok! Just shoot me.” (Sawa! Nipige risasi)
“I will kill you.” (Nitakuua)
“Shoot me! Shoot me right here,” (Nipige risasi, nipige hapa)
Lilikuwa kundi kubwa la watu zaidi ya thelathini waliozunguka sehemu iliyokuwa na mapipa makubwa ya uchafu katika mtaa wa kimasikini wa Manhattan uliokuwa katika Jiji la New York nchini Marekani.
Kila mtu alikuwa akimwangalia kijana aliyeshika bunduki, alikuwa amemnyooshea mwanaume mmoja, alionekana kuwa mtu mzima, alikuwa akitamka maneno kwamba angempiga na risasi endapo tu angeendelea kuzungumza naye mahali hapo.
Kijana huyo aliyeonekana kuchoka kimaisha aliitwa Ethan Dylan, alikuwa kijana mwenye asili ya Kingereza ambaye aliishi nchini Marekani. Katika maisha yake yote, hakuwahi kumuona baba yake, kipindi ambacho mama yake aliondoka nchini Marekani na kwenda Uingereza ndipo alipokutana na baba yake, akarudi nchini mwao Marekani ambapo huko ndipo alipokutana na mwanaume aliyeitwa George.
Wawili hao wakapenda na kuoana. George alikuwa mwanaume mpole, aliyejiheshimu ambaye kila siku alitamani sana kumuona Ethan akikulia katika maisha mazuri, yenye heshima ambayo yangemfanya kuwa baba bora miaka ya baadae.
Kutokana na eneo walilokuwa wakiishi kuwa na vijana wengi wenye fujo, waliojihusisha na madawa ya kulevya, naye Ethan akajikuta akiingia katika huo mkumbo na mwisho wa siku kuwa mhuni wa mtaani.
Mama yake aliumia sana lakini hakuwa na cha kufanya. Kama kuongea, aliongea sana lakini hakukuwa na kitu kilichobadilika. Baadaye akajiingiza kwenye makundi ya wahuni, huko akaanza kuuza madawa ya kulevya na mwisho wa siku kumiliki bunduki yake.
Siku hiyo ambayo alizungukwa na watu wengi, alikuwa amemnyooshea bunduki baba yake wa kambo, mzee George. Alimwambia ukweli kwamba alitaka kumpiga risasi. Maneno hayo hayakumshangaza mzee huyo, alichokifanya ni kumsogelea Ethan na kuiweka bunduki ile kwenye paji lake la uso na kumwambia ampige risasi hapohapo.
“Shoot me right here,” (Nipige risasi hapa) alisema mzee George, watu wote waliokuwa wamewazunguka walianza kuogopa kwani walimjua fika Ethan, hakuwa kijana mwenye masihara, alipokuwa akishinda bastola, hakurudisha nyuma hata mara moja, alikuwa tayari kuua, pasipo kutegemea, akaikoki bastola yake kitendo kilichomfanya kila mtu kushtuka mahali hapo. Hata mzee George naye kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Ethan alionekana kukasirika mno, hata mwili wake ulimtetemeka.


INAENDELEA...

Tuesday 23 January 2018

HADITHI!!!......SEHEMU YA NNE

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 04

Hakukuwa na kitu alichokifikiria zaidi ya ngono, alitaka kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake, hakutaka kumuacha Irakoze hivihivi, alitaka kuhakikisha kwamba kibaridi kile kilichokuwa kikipiga, ni lazima kikatishwe na joto la mwili wa Irakoze.
Alitembea kwa harakaharaka kama mtu aliyekuwa akiwahi kitu fulani, alipofika ndani, akasikia maji yakimwagika bafuni, akajua ni lazima Irakoze alikuwa ndani ya bafu lile akioga. Hakutaka kujiuliza, akausukuma mlango, ukafunguka, naye akazama ndani.
“Aaaah! Padri!” alisema Irakoze huku akijifanya kujificha.
“Usiogope.”
“Naoga padri, naomba uende nje,” alisema Irakoze.
Hiyo ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze, padri Benedicto hakutaka kutoka, alichokifanya ni kuusukuma mlango na kubaki humohumo. Kwa sababu naye mwenyewe alikuwa akimpenda sana padri huyo kutokana na uzuri wa sura yake, hakutaka kuiacha nafasi hiyo, akaitumia vilivyo na hivyo kujikuta wakigusana miili yao, maji ya bomba la mvua yaliwamwagikia, walipapasana hapa na pale na hatimaye kufanya dhambi.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kila kitu, mchezo walioufanya siku hiyo ukampelekea hata Irakoze kuhama chumba chake na kuhamia kwa padri huyo. Waliishi kama mume na mke, hakukuwa na mtu yeyote nje ya nyumba hiyo aliyefahamu kile kilichokuwa kikiendelea.
Ilikuwa siri kubwa mno, na kila alipotoka nyumbani, padri Benedicto alijifanya kuwa mtakatifu mno, kumbe jana yake tu alikuwa amelala na Irakoze usiku mzima. 
“Tumsifu Yesu Kristo!” alisema padri yule.
“Milele Amina.”
Usiri mkubwa uliendelea, padri Benedicto hakutaka kuonekana kuwa rahisi kwa wanawake wengine ambao walimfuata kwa kisingizio cha kutaka kumwagiwa maji ya baraka kumbe upande wa pili walikuwa wakihitaji kulala naye.
Mwanamke aliyekuwa naye nyumbani, alimtosheleza na hata alipokuwa akifuatiliwa na wanawake wengine, hakutaka kuwakubalia kwa kisingizio kwamba alikuwa mtu wa Mungu na hakutakiwa kuoa kutokana na cheo alichokuwa nacho.
“Ninakupenda mpenzi,” alisema Irakoze.
“Nakupenda pia!”
“Hivi siku ikitokea nikapata mimba?”
“Utapataje? Haiwezekani, tupo makini kila siku, wala usijali, mimba haiwezi kutokea,” alisema padri Benedicto.
Hakukuwa na aliyejali sana, padri Benedicto alikuwa na uhakika kwamba kila kitu ambacho kiliendelea kamwe asingeweza kumpa mimba msichana huyo. Siri kubwa iliendelea, waliishi kama mume na mke.
Wakati mwingine padri Benedicto hakuwa akielekea kanisani, alibaki nyumbani kwa ajili ya kufanya mapenzi na msichana huyo tu. Japokuwa kila siku washirika walimtembelea padri wao lakini hakukuwa na yeyote aliyefahamu kama watu hao walikuwa kwenye uhusiano mkubwa wa kimapenzi.
Siku zikakatika, miezi ikaendelea kukatika. Padri Benedicto akaingia moja kwa moja kwenye ulimwengu wa kishetani, naye akaanza kwenda klabu usiku, akaanza kunywa pombe kali zilizomfanya hata kutokuthamini kazi yake ya upadri.
Mabadiliko yale yalimshangaza mno Irakoze, hakutaka kuzungumza naye sana kwa kuamini kwamba mabadiliko hayo yangetokea kipindi hicho tu, cha kushangaza, hakuacha, kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo alivyozidi kubadilika.
Kila siku usiku, akawa mtu wa kutoka na kwenda klabu, huko, alikuwa akivalia kofia kubwa ili asijulikane na mtu yeyote. Alikunywa pombe na wakati mwingine kulewa mno, maisha ya kidunia yakaanza kumteka kiasi kwamba wakati mwingine alipokuwa akirudi nyumbani na kulewa, kesho yake hakwenda kabisa kanisani kwani kichwa bado kilikuwa na pombe kali.
“Kuna kitu ninataka kuzungumza nawe,” alisema Irakoze.
“Kitu gani?”
“Mbona sikuelewielewi! Hebu tulia kwanza,” alisema msichana huyo.
“Nitulie kivipi tena? Unajua leo lini?”
“Jumapili!”
“Basi subiri kwanza niende kanisani,” alisema padri Benedicto.
Japokuwa Irakoze alikuwa na jambo muhimu la kuzungumza na padri huyo lakini hakuweza kupata nafasi hiyo. Ilikuwa ni Jumapili ya tatu tangu asitishe kwenda kanisani kwa kisingizio cha kuwa bize kufuatilia mizigo iliyotumwa kutoka nchini Vatican kwa maendeleo ya kanisa hilo.
Ingawa alikuwa akidanganya kwa kujifanya mfuatiliaji namba moja lakini hakukuwa na mtu aliyemshtukia kwamba ni pombe za janausiku ndizo zilizomuweka nyumbani na kushindwa kabisa kwenda kanisani.
Siku hiyo alipanga kwenda huko kwa ajili ya kuhubiri, alijua ni kwa jinsi gani washirika wake walikuwa wamemkumbuka kwani katika kipindi chote alichokuwa akikaa nyumbani, alikuwa akipigiwa simu na kuuliziwa maendeleo yake.
Siku hiyo alipoonekana kanisani, kila mshirika alikuwa na furaha, wiki tatu ambazo hakuonekana kabisani hapo zilionyesha kila dalili kwamba kanisa hilo lingepwaya sana na hatimaye lingeweza kupotea kabisa.
Ujio wake ukaibua ari ya washirika wake na hatimaye kuendelea na huduma kama kawaida. Kwa kumwangalia, usingeweza kuamini kwamba jana usiku alishinda klabu ya muziki, alionekana mchangamfu na hata macho yake hayakuonyesha kabisa kama alikuwa mtu aliyekesha.
Japokuwa alikuwa akihubiri na kuwabariki watu waliokuja na watoto wao kanisani hapo lakini mara alipokumbuka kwamba Irakoze alitaka kuzungumza naye asubuhi ya siku hiyo, ghafla amani ikakatika.
Hakukuwa na kitu alichokiogopa kama kuambiwa kwamba mtu fulani alitaka kuzungumza naye. Hakujua ni kitu gani kiliendelea lakini mwisho wa siku akataka kukaa chini na msichana huyo ili kumsikia alikuwa na jambo lipi la kuzungumza.
Ibada ilipokwisha, hakutaka kukaa kanisani na kuwasalimia washirika, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea nyumbani kwake. Alipofika huko, kama ilivyokuwa siku nyingine, alipokelewa kwa mahaba mazito mpaka chumbani, hata kabla hajafanya lolote, akavuliwa joho na kupigwa mabusu mfululizo, ndani ya dakika tatu tu, alibaki kama alivyozaliwa.
Kilichofuata ni kilekile kilichokuwa kikitokea siku zote, walifanya dhambi kwa takribani masaa matatu na ndipo kila mmoja akaridhika na kutulia pembeni ya mwenzake.
“Aya niambie ulitaka kuniambia nini asubuhi,” alisema padri Benedicto.
“Una moyo?”
“Ninao. Hebu niambie wala usinitishe.”
“Usiogope, nafikiri ni baraka kutoka kwa Mungu.”
“Ipi?”
“Nina mimba yako!”
“Unasemaje?” aliuliza padri huku akionekana kushtuka.
“Nina mimba yako!”
Padri Benedicto akasimama na kuanza kumwangalia Irakoze, hakuamini kile kilichokuwa kimeongelewa maahali hapo, alimwangalia msichana yule, ndiyo kwanza alikuwa akitabasamu kwa furaha, hakuonekana kujua ni kwa jinsi gani padri alijisikia moyoni mwake.
Kama masharti ya kanisa hilo, hawakutakiwa kuoa, si kuoa tu, hawakutakiwa kuwa na mtoto pia. Kauli ya Irakoze ilimuweka katika wakati mgumu,  mwili wake ukaanza kutetemekea huku kijasho chembamba kikimtoka.
“Unasemaje?”
“Nina mimba yako!”
Alitamani jibu libadilike na kuambiwa kwamba alikuwa akitaniwa, kile alichoambiwa sekunde chache ziliopita kilikuwa kilekile alichoambiwa kwa mara nyigine tena, akajikuta akitoka chumbani humo na kuelekea sebuleni.
“Kuna nini?” aliuliza Irakoze.
“Hivi unajua misingi ya kania letu?”
“Ndiyo! Ila mtoto ni baraka mpenzi!”
“Haiwezekani! Mtoto si baraka katika maisha yangu! “
Hakukuwa na kitu kilichomchanganya katika maisha yake kama hicho, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea kwamba baada ya kufanya sana mapenzi mwisho wa siku msichana wake alikuwa mjauzito.
Wakati mwingine alifikiria kuikataa mimba hiyo ila kila alipona kwamba ndipo kungekuwa na madhara zaidi kwa msichana huyo kutangaza, akaogopa. Kama ilivyokuwa siri katika kipindi cha nyuma, ilitakiwa kuendelea kuwa siri maisha yake yote, iwe isiwe, ilikuwa ni lazima kuhakikisha kwamba jambo hilo halijulikani na mtu yeyote yule.
“Naomba tufanye kitu ili unifiche na aibu hii,” alisema Padri Benedicto huku kijasho chembamba kikianza kumtoka na mwili ukizidi kumtetemeka. Irakoze akamkazia macho.


INAENDELEA...

HADITHI!!!!!.....SEHEMU YA TATU

BIASHARA YA KIFO
sehemu ya 03


Alijulikana kwa jina la Pius Massawe, Mchaga kutoka mkoani Kilimanjaro, alikuwa kijana mwenye sura nzuri kiasi kwamba wanawake wengi wakatokea kumpenda kutokana na uzuri wa sura aliokuwa nao.
Wasichana wengi kutoka katika Shule ya Sekondari ya Majengo mkoani humo walivutiwa na Pius lakini kijana huyo hakutaka kabisa kujihusisha na mambo ya mapenzi kabisa. Wasichana hao hawakutaka kuvumilia, waliamua kumfuata na kumwambia ukweli kwamba walikuwa wakimpenda lakini Pius hakutaka kukubaliana nao, aliwakataa kitu kilichowafanya watu wengi kumshangaa.
Uvumi ukaanza kusikika kwamba Pius alikuwa akishiriki mapenzi ya jinsia moja, uvumi huo ulivuma kwa kasi lakini yeye mwenyewe hakutaka kulizungumzia suala hilo, alijua kwamba kulikuwa na maneno mengi yangesemwa, kwake, hizo zote alizichukulia kama changamoto.
Mbali na uzuri wa sura aliokuwa nao, Pius alikuwa na uwezo mkubwa darasani, katika kila mtihani, alikuwa akiongoza kitu kilichowachanganya watu wengi kabla ya kugundua kwamba mtu huyo alikuwa na akili za kuzaliwa, yaani kile alichokuwa akifundishwa leo, hakuweza kukisahau hata kama ni miaka mingapi ingepita.
Wanawafunzi wengi walikimbilia kwake kufundishwa, Pius hakuwa na maringo, alimfundisha kila mtu japokuwa wanawake wengi walitumia njia hiyo kumtongoza lakini bado msimamo wake ulibaki kuwa uleule kwamba asingeweza kutembea na msichana yeyote yule shuleni hapo.
“Kwani tatizo nini Pius?” aliuliza msichana Thedosia, japokuwa alisifika kwa uzuri shuleni hapo kwa upande wa wanawake, lakini kwa Pius alionekana si chochote.
“Ninataka kuwa padri.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Kwa hiyo hautooa?”
“Hakuna tatizo. Siwezi kufanya mapenzi na msichana yeyote,” alisema Pius huku akimwangalia msichana huyo usoni.
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, hakutaka kufanya mapenzi na msichana yeyote yule. Pius alikuwa kijana wa tofauti na wengine, alihusudu sana ibada, kila siku alipokuwa akihitajika kwenda kanisani, alikwenda, alipofika huko, alikaa katika kiti cha mbele kabisa na kuanza kusali.
Kila alipokuwa, rozali ilikuwa mkononi mwake, na kama haikuwa mkononi, aliichukua na kuivaa shingoni. Alikuwa hivyo, nyumbani napo kulikuwa kama shuleni. Uzuri wa sura yake ulizidi kuwatetemesha wanawake wengi, wengine walijipendeza waziwazi lakini hakuwa na habari nao, alichokuwa akikihitaji ni kuwa padri tu.
Alipomaliza kidato cha nne na kujiunga na cha tano katika Shule ya Sekondari ya Tambaza iliyokuwa jijini Dar es Salaam. Kila alipofika, Pius alikuwa gumzo, japokuwa alipokuwa mkoani Kilimanjaro aliambiwa kwamba atakapofika Dar es Salaam basi msimamo wake ungeweza kulegea lakini huko akawa vilevile kiasi kwamba watu wakampa jina la padri kitu kilichomfurahisha mno.
Alipomaliza kidato cha sita kwa masomo ya kawaida, akafaulu lakini akajiunga na chuo cha upadri kilichokuwa Morogoro na kisha kuanza masomo rasmi. Haikuwa kazi ngumu, alizingatia masomo yake, kila siku asubuhi alikuwa akiamka na wenzake na kwenda kanisani kusali, walipomaliza na ndipo walipoendelea na mambo mengine.
Alisoma huko kwa muda wa miaka mitatu na ndipo walipoandaliwa kwenda kumalizia masomo ya mwisho katika Jiji la Venice nchini Italia. Ilikuwa furaha kwake kwani alibakiza hatua chache kabla ya kufika pale alipotaka kufika.
Kutoka Venice mpaka Vatican haikuwa mbali sana, mara kwa mara alikuwa akielekea huko na kukutana na viongozi wa dini ya Kiroma na kuzungumza nao mawilimatatu kitu kilichomfanya kujisikia vizuri na kuahidi kushinda kile kilichobakia mbele yake.
Huko ndipo alipopewa jina la Benedicto badala la lile la Pius alilokuwa akilitumia kabla. Baada ya kukaa huko Venice kwa miaka miwili ndipo aliporudi nchini Tanzania na kupewa kanisa huku akijulikana kwa jina la Padri Benedicto.
Kanisa likajaza wanawake wengi kuliko wanaume, tetesi zilizokuwa zikisikika kwamba kanisa hilo lilikuwa na padri aliyekuwa na sura nzuri iliwachanganya wanawake wengi na hivyo kutaka kwenda huko kushuhudia kwa macho yao.
Walipomuona, waliamini kwamba duniani kulikuwa na wanaume wenye sura nzuri mno, kila walipomwangalia padri wao, walimtamani mno.
“Jamani hii sheria ya mapadri kuoa si ipitishwe tu, nahisi kama bahati inaweza kuniangukia,” alisikika akisema msichana mmoja.
“Bahati ya nini?”
“Kuolewa na padri Benedicto, ninampenda sana jamani!”
“Wewe Upendo, humuogopi Mungu!”
“Namuogopa, lakini kwa nini ameamua kutupa jaribu kubwa namna hii?”
Padri Benedicto alikuwa akiishi peke yake nyumbani kwake, wafanyakzi wengi wa ndani aliokuwa akiwahitaji walikuwa wa kiume tu ambao wengi alikorofishana nao na mwisho wa siku kuwafukuza kihekima.
Baada ya kufukuza wafanyakazi watano, akaamua kuishi peke yake, hakutaka tena kuwa na mfanyakazi yeyote nyumbani kwake kwani aliona kama angeweza kufanya kazi peke yake pasipo mfanyakazi yeyote yule.
“Ila kuna msichana ana matatizo sana, naomba aje akusaidie padri,” alisema mama John, mwanamke aliyekuwa ameonana na Irakoze.
“Nimsaidie vipi?”
“Aje kufanya kazi hapa!”
“Msichana?”
“Ndiyo!”
“Hapana! Haiwezekani hata kidogo.”
Japokuwa padri Benedicto alikataa lakini mama John hakuacha kumbembeleza akubaliane naye kwani mtu kama yeye alihitaji mfanyakazi wa kike kwa ajili ya kufanya usafi wa nyumba muda wote kitu ambacho kwa kiasi fulani kikaanza kumuingia padri huyo.
Mbali na kumwambia hivyo, pia alimsimulia historia ya kusikitisha ya msichana Irakoze kiasi kwamba padri akaingiwa na huruma na kuona kwamba kumsaidia msichana huyo ilikuwa kama baraka kwa Mungu kwa kuwa ameamua kumtoa mtu fulani kutoka sehemu moja ya chini na kumuweka sehemu ya juu.
Wakakubaliana na hivyo mama John kuelekea nyumbani ambapo akamchukua Irakoze na kuelekea naye nyumbani hapo. 
“Ni mzuri mno, sijawahi kuona mwanaume mzuri kama huyu,” alijisemea Irakoze katika kipindi alichomuona padri Benedicto kwa mara ya kwanza.
Hiyo ndiyo ikawa siku ya kwanza kukutana kwa watu hao, Irakoze akaanza kazi ndani ya nyumba hiyo. Alikuwa msichana mwenye heshima kubwa, kila siku alikuwa mtu wa kuvaa mavazi marefu ambayo aliamini kwamba yasingemtia majaribu padri huyo.
Waliheshimiana mno, kila siku asubuhi walikutana sebuleni, walishikana mikono na kuanza kusali kisha kuendelea na ratiba nyingine. Katika kipindi chote hicho, Irakoze alikuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa padri huyo, alitamani kumwambia ukweli kwamba alimpenda lakini aliogopa kufanya hivyo, akabaki akiugulia moyoni mwake tu.
Siku zikaendelea kukatika, heshima ilikuwa kubwa ndani ya nyumba, Irakoze aliendelea kufanya kazi ndani ya nyumba hiyo huku kila siku akijitoa kitendo kilichomfurahisha padri Benedicto kiasi kwamba alijiona kuchelewa mpaka kuchukua uamuzi wa kumuajiri mfanyakazi wa kike.
“Nakuja, niandalie chakula,” alisema padri Benedicto.
Siku hiyo hakuwepo nyumbani, alikuwa kanisani akiendelea na huduma, mawingu mazito yalitanda angani kuonyesha kwamba muda wowote ule mvua ingeweza kunyesha. Mara baada ya kumaliza kila kitu likiwa suala la kupika chakula, Irakoze akachukua khanga yake na kuelekea bafuni kuoga.
Alipokuwa huko, akasikia mvua kubwa ikianza kunyesha huku kiubaridi kikianza kuongezeka. Alichokifanya Irakoze, akatoka bafuni na khanga yake kisha kutoa ndoo nje kwa ajili ya kukinga maji ya mvua yaliyokuwa yakidondoka.
Mwili wake ukalowa, khanga ikanata mwilini mwake, umbo lake lenye mvuto, makalio yaliojaajaa yakawa yanaonekana vizuri kabisa. Hakuwa na wasiwasi wowote ule, alikuwa peke yake nyumbani hapo hivyo aliendelea kufanya kazi yake.
Wakati yupo hapo akiendelea kukinga maji, mara geti likafunguliwa na padri Benedicto kuingia. Irakoze hakumuona padri huyo, aliendelea kukinga maji huku wakati mwingine akijimwagia, kifua chake kikanata kwenye ile khanga, kila kitu mwilini mwake kilionekana wazi.
Padri Benedicto alipoona hivyo, moyo wake ukashtuka, hakupiga hatua, alibaki akimwangalia Irakoze huku akiwa na mwamvuli wake. Alibaki akimeza mate na maeneo ya zipu yake kuanza kusogea mbele. Alichanganyikiwa, kila alipojitahidi kuyaamisha macho yake, yaligoma kabisa kuhama.
Mpaka Irakoze anageuka na kumwangalia padri huyo, alikuwa hoi, kwa kujishtukia, Irakoze akamsalimia na kisha kuelekea ndani, sehemu ya nyuma ilikuwa ikichezacheza, padri akaona haiwezkani, japokuwa hakuwahi kulala na mwanamke yeyote maishani mwake, uzalendo ukamshinda, pepo la ngono likamwingia, mwili wake ukaanza kumsismka huku akihisi vijidudu fulani vikianza kumtembelea mwilini mwake, naye akaanza kuelekea ndani huku akiwa amechanganyikiwa kimahaba, pepo la ngono lilishamvaa, hakukubali, alitaka kuonekana kwamba hata na yeye alikuwa mwanaume.


INAENDELEA...