Sunday 28 January 2018

HADITHI!!!!!!!!!!................. SEHEMU YA KUMI

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 10


Ni kweli walishtuka, hawakuamini kile walichokisikia kwamba mbali na kuwatafuta wanawake waliotakiwa kuwapeleka kwa ajili ya kuigiza filamu, kulikuwa na kazi nyingine ya ziada ambayo iliitwa Biashara ya Kifo.

“Ndiyo inakuwaje hiyo?”

“Ni kazi rahisi tu japokuwa unahitajika umakini wa hali ya juu,” alisema bwana Cook.

Hapo ndipo mzee huyo alipoanza kueleza namna ambavyo biashara hiyo ilitakiwa kufanyika. Kulikuwa na kundi la wanawake mitaani waliokuwa wakihitaji ajira, watu waliokuwa wakitafuta ajira kila siku, mbali na hiyo, kulikuwa na kundi kubwa la wanawake ambao kila siku walitamani kufika nchini Marekani.

Hao ndiyo waliotakiwa kufanyiwa biashara hii. Kazi ilikuwa ni kuwafuata na kuanza kuwalaghai kwa maneno matamu kwa kuwaahidi kwamba wangewapa ajira yenye kiasi kikubwa cha fedha na hivyo wawasafirishe kwenda nchini Marekani, wanapofika huko, walazimshwe kuigiza filamu za ngono, kwa atakayetaka kuendelea basi aendelee lakini kwa wale ambao wangekataa kuendelea na kulilia kurudi nyumbani, basi hao wauawe na kisha kuchunwa ngozi ambayo ingepelekwa nchini China kwa ajili ya kutengenezea vitu vya asili.

“Mmmh!” aliguna Ethan.

“Unahisi ni kazi ngumu?”
“Kwangu! Kuchuna ngozi ya binadamu, sijawahi kufanya kazi hiyo,” alijibu Ethan.

“Kazi yako si kuchuna ngozi, kazi yako kubwa ni kutafuta wasichana tu, hakuna jingine, hiyo ni kazi ya watu wengine,” alisema bwana Cook.

“Kama ndiyo hivyo, hakuna shida.”

Hiyo ndiyo kazi aliyoahidiwa kulipwa kiasi kikubwa cha fedha. Kilichofanyika ni kupewa kiasi cha dola elfu hamsini ambazo zilikuwa ni zaidi ya milioni hamsini, akatengenezewa pasipoti kubwa kwa ajili ya kusafiria nchi hadi nchi na kisha kuanza safari za kuwatafuta wasichana kwa ajili ya kuigiza filamu za ngono.

Safari yao ya kwanza kabisa kwenda ilikuwa nchini Hispania, huko wakakutana na wasichana kadhaa na kuhitaji kufanya nao mahojiano kwa ajili ya kazi za uongo walizowaambia kwamba zilikuwa nyingi nchini Marekani.

“Upo tayari?”

“Kiasi gani?”

“Dola elfu moja kwa siku,” alijibu Ethan.

“Mmmh! Ni kazi gani?”
“Zipo nyingi tu lakini unatakiwa kuchagua. Kuna kazi za hotelini, kupika na nyingine nyingi,” alisema Ethan.

“Nipo tayari!”

“Sawa.”
“Si umesema Marekani?”
“Ndiyo!”

“Hakuna tatizo!”

Kutokana na wimbi kubwa la wasichana wa Ulaya kukosa ajira na kutamani sana kwenda nchini Marekani kwa kuamini kwamba kulikuwa na maisha mepesi, wakakubaliana na Ethan na mwisho wa siku kuelekea huko.

Ishu zote za usafirishaji zilikuwa chini yake, alitumia kiasi kikubwa cha fedha alichopewa na bwana Cook hivyo hakukuwa na tatizo lolote lile. Walipofika nchini Marekani katika Jiji la New York ambapo ndipo kulipokuwa makao makuu ya kampuni hiyo ya filamu za utupu, wakapelekwa hotelini na kuambiwa wasubiri.

“How many are they?” (Wapo wangapi?)

“Ten young girls!” (Wasichana wadogo kumi)

“What do you mean? Below 18?” (Unamaanisha nini? Chini ya miaka kumi na nane?) aliuliza bwana Cook.

“No! Above 18 but below 23,” (Hapana! Zaidi ya miaka 18 lakini chini ya miaka 23)

“Ok!” (Sawa)

Mara baada ya kufika katika hoteli hiyo, wakaambiwa waoge kwa ajili ya chakula cha usiku na siku inayofuata wangeanza safari ya kuelekea katika eneo la kazi, kule walipotakiwa kufanya kazi.

Kila mmoja alikuwa na furaha mno, kutoka nchini Hispania mpaka kufika nchini Marekani, tena kufanya kazi ndogo kwa mshahara mkubwa ilionekana kuwa kama bahati kwao. Sheria moja kubwa waliyokuwa wamepewa ni kutokutumia simu tu.

Waliufurahia usiku huo kwa kuona kwamba ndiyo ilikuwa mwanzo wa safari yao ya kuwa mamilionea mara watakaporudi nchini mwao, hakukuwa na mtu aliyehisi kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na zoezi zima la kuigiza filamu za utupu na kama kungekuwa na yeyote atakayekataa basi ilikuwa ni lazima auawe na kuchunwa ngozi.

“Andikisheni majina yenu na nafasi unazotaka kufanya kazi,” alisema Ethan, alikuwa akiwaambia wasichana hao kumi ambao wakafanya kama walivyotakiwa kufanya.

Siku iliyofuata Ethan akarudi hotelini hapo kisha kuwachukua, akawapeleka katika jumba moja kubwa lililokuwa pembezoni mwa Jiji la New York, aliwaandaa kwa ajili ya kazi aliyotaka kuwapa. Kwa kuwaangalia wasichana wale, walionekana kuwa na furaha kubwa kwa kuamini kwamba huo ungekuwa mwanzo tu kwani hata mapokezi waliyokuwa wamepewa siku hiyo yalikuwa makubwa na ya kifahari.
Wakateremka kutoka garini na kuingia ndani ya jumba moja kubwa, humo wakaambiwa watulie kwani kulikuwa na mtu aliyetaka kuzungumza nao. Wakatulia vitini na Ethan kuelekea chumbani. Baada ya dakika moja akarudi na mwanaume mmoja, alikuwa mtu mwenye umri mkubwa ambapo kwa kumwangalia tu, ungehisi kwamba alikuwa na miaka zaidi ya hamsini.

“Karibuni sana,” aliwakaribisha mzee huyo.

“Asante sana,” waliitikia kwa pamoja.

“Mpo hapa kwa ajili ya kufanya kazi, si ndiyo?”
“Ndiyo!”

“Kazi ipo, ila mmekwishaambiwa ni kazi gani mtakayofanya?”

“Hotelini!”

“Sawa! Ila kwa bahati baya huko kazi imekwisha, iliyobakia ni moja tu,” alisema mzee huyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Gregory.

Wasichana wale walipoambiwa kwamba kazi ya hotelini ambao walikuwa wameifuata ilikwisha, kila mmoja akanyong’onyea lakini walipoambiwa kwamba kulikuwa na kazi nyingine ambayo ilikuwepo mahali hapo, wakarudi kwenye tumaini jipya.

“Kazi gani?”
“Mnajua kuigiza?”

“Mimi najua...” alisema msichana mmoja.

“Hata mimi najua,” alisema mwingine, mwisho kabisa, wote walisema wanajua.

“Nani anamjua Blue Diamond?”

“Mimi simfahamu.”

“Mimi namfahamu! Ni mcheza filamu za utupu,” alijibu msichana mmoja.

“Sawasawa! Blue alikuwa msichana kama nyie, wakati alipotoka nchini Canada, alifikia ndani ya nyumba hiihii, alikuwa masikini sana, lakini tukayabadilisha maisha yake na kuwa tajiri namna hiyo. Tulipomwambia kuhusu kuigiza filamu hizo, aliogopa sana lakini sasa hivi anatushukuru na kutulaumu kwa kuwa tulimchelewa kumwambia juu ya mafanikio makubwa ambayo angeyapata.

“Sasa hivi Blue ni msichana mwenye mafanikio, anaoglelea kwenye bwawa la fedha, anaendesha gari analotaka. Wangapi mpo tayari kuwa kama Blue?” alisema mzee Gregory na kumalizia na swali.

“Kuwa muigizaji wa filamu za utupu?” aliuliza msichana mmoja.

“Ndiyo! Hatukulazimishi kuigiza, hakuna mtu anayelazimishwa kuyafuata mafanikio na utajiri. Huwa tunalipa dola elfu tatu kwa kila kipande kimoja kwenye filamu zetu, kwa maana hiyo ikitokea ukafanya mapenzi na wanaume wawili kwa mpigo, utapata dola elfu sita,” alisema mzee huyo.

Kiasi cha fedha ambacho walitajiwa kilikuwa kikubwa mno zaidi ya milioni sita kwa mtu mmoja na milioni kumi na mbili kama utafanya mapenzi na wanaume wawili kwa pamoja, kila aliyekisikia, alitamani kukipata hapohapo lakini tatizo likawa namna ya kuigiza filamu hizo.  Wasichana hao wakaanza kutoa minong’ono ya chinichini lakini mzee yule aliendelea kuwaambia kwamba ilikuwa ni lazima wafikie mafanikio kama wangekubaliana nae.

Ili kuendelea kuwalaghai, wakawaletea mikataba na kuwawekea mbele yao, walitakiwa kusaini kisha kuandika akaunti zao ili mara watakapoanza kuigiza basi wawekewe kiasi hicho cha fedha.

“Mimi sipo tayari,” alisema msichana mmoja.

“Hata mimi sipo tayari,” alisema msichana mwingine.

“Sawa! Hakuna tatizo!”

“Mimi nipo tayari!”

“Safi sana!”

Kati ya wasichana kumi, wanne walikuwa tayari, wakakubaliana na mzee Gregory kisha kuambiwa wabaki mahali hapo huku wale sita waliokataa wakiambiwa warudi hotelini tayari kwa kujiandaa na safari siku ijayo kurudi nchini Hispania.


Wakasimama na kutolewa nje, wakaingizwa ndani ya gari huku Ethan akiwa pamoja nao. Gari halikwenda hotelini, lilibadilisha njia na kwenda katika jumba jingine kabisa, wao wenyewe walishangaa, hawakujua waliletwa pale kwa ajili gani, wakashushwa na kuingizwa ndani ya jumba lile, lengo kamili lilikuwa ni kuuawa na kisha kuchunwa ngozi, hiyo ndiyo ilikuwa Biashara ya Kifo, walitakiwa kuuawa na ngozi zao kutumwa nchini China ambapo kulikuwa na biashara nzuri tu.

HADITHI!III!!!!!!!!!!............SEHEMU YA TISA

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 09
 Hawakuwa na haja ya gari lile, walikuwa tayari kuliacha lakini wayaokoe maisha yao, hawakutaka kusimama sehemu yoyote ile, waliendelea kusonga mbele kwa kuamini kwamba wangefika sehemu iliyo salama kabisa.

Wakati wamefika umbali urefu, mara wakaanza kuwaona polisi wakiwa mbele yao, tena wakija kwa kasi huku wakiwa na bunduki na mbwa walioonekana kuwa na mafunzo makubwa ya kunusa. Wakati wamebakiza kama hatua mia moja kutoka walipokuwa, wakawaona mbwa wale wakiongeza kasi ya unusaji wao na kuona kwamba iwe isiwe wangeweza kukamatwa.

“Tufanye nini? Turudi tulipotoka au?” aliuliza rafiki yake, Thomson.

“Twende kulia,” alisema Ethan na kuanza kukimbilia upande wa kulia.

Hiyo haikusaidia, mbwa wale waliendelea kuwaongoza polisi kule walipokuwa, tayari waliona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wao. Hawakusimama zaidi ya kuongeza kasi zaidi, hiyo wala haikusaidia kwani kadiri walivyoongeza kasi na ndivyo ambavyo polisi wale waliokuwa na mbwa walipozidi kuwafuata, tena nao wakiongeza kasi.

“Wooo...wooo...wooo...” walisikika mbwa wakibweka.

Japokuwa walikimbia sana tena kwa kasi lakini mwisho wa siku wakajikuta wakikamatwa na kutiwa nguvuni. Hawakuwa na jinsi, wakabebwa na kupelekwa Jijini Texas ambapo huko wakafikishwa kituo cha polisi tayari kwa kupelekwa mahakamni.

“Sikutarajia kama kuna siku ningekamatwa,” alisema Ethan.

“Hata mimi! Ila kosa lilikuwa pia?”
“Hatukujipanga, tulikurupuka tu.”

Kesho yake, wakachukuliwa na kupandishwa mahakamani ambapo huko wakajikuta wakikosa dhamana na hivyo kupelekwa rumande. Baada ya wiki mbili Ethan na mwenzake wakarudishwa tena mahakamani ambapo siku hiyo ilionekana kuwa bahati kwao kwani hakukuwa na shahidi yeyote ambaye alijitokeza na kusema kwamba kweli gari hilo liliibwa, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alisimama kinyume nao na kuweka ushahidi wao ili wahukumiwe, hivyo mwisho wa siku wakajikuta wameshinda kesi ile.

“Siamini,” alisema Ethan huku akionekana kutokuamini macho yake.

Wakawa huru, Ethan akamuahidi rafiki yake huyo kwamba asingeweza kurudia tabia ya kuiba magari tena kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea ni Mungu tu ndiye aliyemsaidia mpaka kuwa huru muda huo. Baada ya kila kitu kuihs amahakamani, wakatoka nje.

“Samahani,” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja, alikuwa amemshika bega kwa nyuma, Ethan akageuka.

“Bila samahani.”
“Unahitajika!”

“Wapi? Na nani?”

“Kuna mtu anakusubiri ndani ya gari ile pale.”
“Nani?”
“Twende, utamfahamu tukifika,” alisema mwanaume huyo.

“Twende Thomason....” alimwambia rafiki yake.

“Hapana! Unahitajika peke yako, labda huyu anaweza kusubiri hapa,” alisema mwanaume yule.

Hakuwa na amani kabisa, alikuwa akijiuliza juu ya huyo mtu aliyekuwa akimsubiri ndani ya gari lile. Kwa kuliangalia tu, lilikuwa gari la thamani lililomfanya kuona kwamba mtu aliyekuwa akimiliki gari hilo alikuwa na fedha nyingi.

Hakutaka kusita, alichokifanya ni kuelekea lilipokuwa gari lile, alipolifikia, mlango ukafunguliwa na mwanaume yule kisha kuingia ndani. Kulikuwa na giza, hakukuwa na mwanga, alipokaa kitini, taa zikawashwa na macho yake kutua kwa mwanaume mmoja, hakuwa mgeni machoni mwake, alimfahamu sana, mara ya kwanza kabisa alikutana naye ndani ya ndege na kumpa business card yake, na ndiye yule aliyekuwa akitamani kuwasiliana naye kipindi cha nyuma, alikuwa bwana Boyla Cook.

“Cook!” aliita Ethan kwa mshtuko mkubwa.

“Unaendeleaje Ethan?” aliuliza bwana Cook huku akichia tabasamu pana.”
“Naendelea vizuri, nilikutafuta sana, nilisahau nilipoiweka business card yako, nimefurahi kuonana nawe tena,” alisema Ethan huku akionekana kutokuamini.

“Nimefurahi pia.”

Hapo ndipo bwana Cook alipomwambia kwamba kila kitu kilichoendelea kule mahakamani kilikuwa nyuma yake, alikuwa amepanga kila kitu na ndiyo maana hata mara ya pili alipofikishwa mahakamani pale kesi ilikuwa nyepesi sana kwa kuwa alitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumtoa katika matatizo aliyokuwa nayo.

Ethan akafurahi sana, akamshukuru mzee huyo lakini hapohapo akaanza kujiuliza juu ya msaada ule, mzee yule alikuwa akihitaji nini.

“Nashukuru sana! Ila kwa nini umenisaidia? Na umejuaje kama nilikamatwa?” aliuliza Ethan.

“Nilikuwa nakufuatilia kila kona, nilikwamba kwamba biashara uliyokuwa ukiifanya haikuwa salama kwani muda wowote ule ungekuwa kwenye hatari. Nilitamani sana kufanya kazi na wewe na ndiyo maana kila ulipokuwa, nilihakikisha nakufuatilia kwa ukaribu.

“Wakati mzee Sanchez amefariki, nilitaka kuja kukuchukua lakini nilikuwa na safari ya kwenda Brazil, hivyo nikaamua kuachana nawe kwa muda. Nimerudi siku kadhaa zilizopita na ndipo nilipotuma vijana wakufuatilie na kujua upo wapi, wakasema umekuja huku Texas na umekamatwa kwa kosa la kuiba gari na kutaka kulivusha mpakani, hivyo nikatuma fedha zisaidie kukutoa ili tufanye kazi,” alisema mzee huyo kwa kirefu.

Ethan akashusha pumzi ndefu, hakuamini kile alichokuwa amekisikia, kumbe wakati yeye akijaribu kukumbuka juu ya kile kikaratasi alichokuwa amepewa chenye namba ya bwana Cook, kumbe naye alikuwa akimfuatilia kwa ukaribu. Mpaka kufikia hatua hiyo tayari akajiona kuwa miongoni mwa watu waliokuwa na bahati kubwa.

“Unataka tufanye kazi gani?” aliuliza Ethan.

“Twende nyumbani, tutaongea mengi,” alisema bwana Cook.

“Siwezi kwenda peke yangu, si unajua nina mwenzangu,” alisema Ethan huku akimwangalia rafiki yake, Thomson dirishani.

“Mwambie aje,” aliagiza mzee huyo.

Hapohapo Thomson akaitwa na kisha kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwa mzee huyo. Kichwa cha Ethan bado kiliendelea kujiuliza maswali juu ya kazi aliyotakiwa kufanya kwa mzee huyo. Hakuijua ilikuwa ni kazi gani lakini kwa sababu alionyeshewa msaada mkubwa, hakuwa na jinsi, alijiona lingekuwa suala la busara kama angekubaliana naye.

Safari ile ikaishia mbele ya jumba moja la kifahari, kwa kuliangalia wala usingejiuliza maswali kwamba jumba hilo lilikuwa likimilikiwa na mtu mwenye fedha, mtu aliyekuwa na zaidi ya dola bilioni kumi katika akaunti yake. Geti likafunguliwa na kisha gari kuingizwa.

Lilikuwa jumba kubwa lililosheheni vitu vyote ambavyo vilitakiwa kuwa ndani ya jumba la bilionea fulani, kulikuwa na bwana kubwa la kuogelea ambalo sakafu yake ilikuwa ni ya kioo, kulikuwa na mbuga ndogo ya wanyama na kwa mbali kulionekana kuwa na wanyama fulani na ndege wengi, kulikuwa na magari ya kifahari na vitu vingine, ukiachana na hivyo, kulikuwa na masanamu manne ya kike yaliyoonekana kuwa uchi kabisa.

Milango ya gari ikafunguliwa na kisha kuteremka, wakaanza kupiga hatua kuelekea ndani. Muda wote huo Ethan na Thomson walikuwa wakiangalia huku na kule, kila kitu kilichoonekana kwao kilionyesha ni kwa namna gani bwana Cook alikuwa mtu tajiri aliyeogelea fedha.

Walipojingia ndani, kitu cha kwanza kabisa walichokutana nacho ni picha za wanawake wengi zilizokuwa zimebandikwa ukutani, walikuwa watupu kama walivyozaliwa, walikaa katika mapozi tofautitofauti na walikuwa wanawake wa kila asili.

Ethan aliziangalia picha zile, hakuelewa ni kwa nini zilikuwa mahali hapo, ziliusisimua mwili wake kwani kilipita kipindi kirefu hakuwahi kukutana kimwili na mwanamke yeyote yule. Alizunguka huku na kule, macho yake yalikuwa yakiangalia kila kona.

“Mbona kuna picha nyingi sana za wanawake?’ aliuliza Ethan.

“Ninapenda kuwa nazo.”
“Ndiyo ziwe nyingi namna hii?”
“Yeah! Huwa ninafurahia ninapomwangalia mwanamke akiwa mtupu.”
“Mmmh!”

“Ndiyo hivyo! Karibuni sana,” alisema bwana Cook huku akiachia tabasamu pana.

Wakakaa kwenye makochi ya manyoya na kutulia. Wote wawili walikuwa wakiangalia huku na kule, bwana Cook akatoka sebuleni hapo na kuelekea chumbani kwake, baada ya dakika tatu akarudi huku akiwa amebadilisha nguo zake, akaagiza vinywaji, vikaletwa na kuanza kunywa.

“Ninataka unifanyie kazi Ethan,” alisema bwana Cook.

“Kazi gani?”

“Kwanza unajua mimi ni nani?”
“Unaitwa Boyle Cook, sijui kingine zaidi ya hicho,” alijibu Ethan.

“Sawa. Hujawahi kulisikia jina langu sehemu yoyote?”

“Hapana!”

“Mimi ni mkurugenzi wa kampuni ya kutengeneza filamu za utupu ya Bravilian.sex, ni kampuni inayojitegemea na ambayo imetengeneza filamu nyingi mno,” alisema bwana Cook.

“Sawa! Nimefurahi kukufahamu! Kwa hiyo unataka na mimi niigize?”

“Ungependa kuigiza?”
“Hapana! Siwezi kabisa.”
“Sawa! Lengo la kukuita hapa si kutaka uigize bali kuna kazi nyingine nataka uifanye,” alisema bwana Cook.

“Kazi gani?”
“Kunitafutia wasichana wengi duniani kwa ajili ya kuigiza, kila msichana nitakulipa dola elfu kumi,” alisema bwana Cook.

“Mmmh!”

“Ni kazi ngumu?”

“Si sana, kama nitapewa fedha za kutosha kuzunguka duniani, si kazi ngumu, hakuna tatizo,” alisema

“Ila kuna kazi nyingine nataka ufanye, ila kwa siri sana.”
“Kazi ipi?”

“Biashara ya Kifo,” alisema bwana Cook, Ethan na Thomson wakashtuka.

INAENDELEA...