Saturday 29 October 2016

HADITHI!! HADITHII!!!

WIZI MBAYA

Imesimuliwa na Zubeda Abdalla Omar.
Hapo zamani za kale alikuwepo bwana mmoja, aliekuwa na wake watatu mmoja alikuwa mwizi. Yule
bwana alikuwa anafuga mbuzi, siku moja kati ya wale wake zake mmoja aliiba mbuzi na kumchinja na kumpika bila ya yeye kujua. Aliporudi safari yake aliuliza nani alimchinja mbuzi? Wote walikataa. Yule bwana akasema basi mimi nitafanya dawa. Wakajibu sawa, yule bwana akafanya mambo yake kisha akawapeleka mtoni. Walipofika aliwambia  mmoja mmoja aanze  kuingia mtoni na huku akiimba.
Aliingia wa kwanza huku akiimba nyimbo:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Alipomaliza kuimba akaibuka, kwani yeye hakuwa mwizi. Akafuata wa pili huku akiimba:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Yeye pia akaibuka na kukaa pembeni.  Akafuata yule wa tatu akaingia huku akiimba:
     Kachiriri, kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri. 
     Mani nenga Kachiri
     Depala dipolo kachiri
     Dipolo dabambo kachiriri
     Kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri kachiriri.
Lakini yeye alizama.
Kuona vile yule bwana akajua kwamba yule mke wa tatu ndie mwizi. Hapo akafanya dawa zake na yule bibi  akaibuka, alimuomba radhi mumewe na kuahidi kuwa  hatorudia tena kosa lake. Na yule bwana alikubali na wakaendelea kuishi kwa raha mustarehe.


No comments:

Post a Comment