Tuesday 23 January 2018

HADITHI!!!!!.....SEHEMU YA TATU

BIASHARA YA KIFO
sehemu ya 03


Alijulikana kwa jina la Pius Massawe, Mchaga kutoka mkoani Kilimanjaro, alikuwa kijana mwenye sura nzuri kiasi kwamba wanawake wengi wakatokea kumpenda kutokana na uzuri wa sura aliokuwa nao.
Wasichana wengi kutoka katika Shule ya Sekondari ya Majengo mkoani humo walivutiwa na Pius lakini kijana huyo hakutaka kabisa kujihusisha na mambo ya mapenzi kabisa. Wasichana hao hawakutaka kuvumilia, waliamua kumfuata na kumwambia ukweli kwamba walikuwa wakimpenda lakini Pius hakutaka kukubaliana nao, aliwakataa kitu kilichowafanya watu wengi kumshangaa.
Uvumi ukaanza kusikika kwamba Pius alikuwa akishiriki mapenzi ya jinsia moja, uvumi huo ulivuma kwa kasi lakini yeye mwenyewe hakutaka kulizungumzia suala hilo, alijua kwamba kulikuwa na maneno mengi yangesemwa, kwake, hizo zote alizichukulia kama changamoto.
Mbali na uzuri wa sura aliokuwa nao, Pius alikuwa na uwezo mkubwa darasani, katika kila mtihani, alikuwa akiongoza kitu kilichowachanganya watu wengi kabla ya kugundua kwamba mtu huyo alikuwa na akili za kuzaliwa, yaani kile alichokuwa akifundishwa leo, hakuweza kukisahau hata kama ni miaka mingapi ingepita.
Wanawafunzi wengi walikimbilia kwake kufundishwa, Pius hakuwa na maringo, alimfundisha kila mtu japokuwa wanawake wengi walitumia njia hiyo kumtongoza lakini bado msimamo wake ulibaki kuwa uleule kwamba asingeweza kutembea na msichana yeyote yule shuleni hapo.
“Kwani tatizo nini Pius?” aliuliza msichana Thedosia, japokuwa alisifika kwa uzuri shuleni hapo kwa upande wa wanawake, lakini kwa Pius alionekana si chochote.
“Ninataka kuwa padri.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Kwa hiyo hautooa?”
“Hakuna tatizo. Siwezi kufanya mapenzi na msichana yeyote,” alisema Pius huku akimwangalia msichana huyo usoni.
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, hakutaka kufanya mapenzi na msichana yeyote yule. Pius alikuwa kijana wa tofauti na wengine, alihusudu sana ibada, kila siku alipokuwa akihitajika kwenda kanisani, alikwenda, alipofika huko, alikaa katika kiti cha mbele kabisa na kuanza kusali.
Kila alipokuwa, rozali ilikuwa mkononi mwake, na kama haikuwa mkononi, aliichukua na kuivaa shingoni. Alikuwa hivyo, nyumbani napo kulikuwa kama shuleni. Uzuri wa sura yake ulizidi kuwatetemesha wanawake wengi, wengine walijipendeza waziwazi lakini hakuwa na habari nao, alichokuwa akikihitaji ni kuwa padri tu.
Alipomaliza kidato cha nne na kujiunga na cha tano katika Shule ya Sekondari ya Tambaza iliyokuwa jijini Dar es Salaam. Kila alipofika, Pius alikuwa gumzo, japokuwa alipokuwa mkoani Kilimanjaro aliambiwa kwamba atakapofika Dar es Salaam basi msimamo wake ungeweza kulegea lakini huko akawa vilevile kiasi kwamba watu wakampa jina la padri kitu kilichomfurahisha mno.
Alipomaliza kidato cha sita kwa masomo ya kawaida, akafaulu lakini akajiunga na chuo cha upadri kilichokuwa Morogoro na kisha kuanza masomo rasmi. Haikuwa kazi ngumu, alizingatia masomo yake, kila siku asubuhi alikuwa akiamka na wenzake na kwenda kanisani kusali, walipomaliza na ndipo walipoendelea na mambo mengine.
Alisoma huko kwa muda wa miaka mitatu na ndipo walipoandaliwa kwenda kumalizia masomo ya mwisho katika Jiji la Venice nchini Italia. Ilikuwa furaha kwake kwani alibakiza hatua chache kabla ya kufika pale alipotaka kufika.
Kutoka Venice mpaka Vatican haikuwa mbali sana, mara kwa mara alikuwa akielekea huko na kukutana na viongozi wa dini ya Kiroma na kuzungumza nao mawilimatatu kitu kilichomfanya kujisikia vizuri na kuahidi kushinda kile kilichobakia mbele yake.
Huko ndipo alipopewa jina la Benedicto badala la lile la Pius alilokuwa akilitumia kabla. Baada ya kukaa huko Venice kwa miaka miwili ndipo aliporudi nchini Tanzania na kupewa kanisa huku akijulikana kwa jina la Padri Benedicto.
Kanisa likajaza wanawake wengi kuliko wanaume, tetesi zilizokuwa zikisikika kwamba kanisa hilo lilikuwa na padri aliyekuwa na sura nzuri iliwachanganya wanawake wengi na hivyo kutaka kwenda huko kushuhudia kwa macho yao.
Walipomuona, waliamini kwamba duniani kulikuwa na wanaume wenye sura nzuri mno, kila walipomwangalia padri wao, walimtamani mno.
“Jamani hii sheria ya mapadri kuoa si ipitishwe tu, nahisi kama bahati inaweza kuniangukia,” alisikika akisema msichana mmoja.
“Bahati ya nini?”
“Kuolewa na padri Benedicto, ninampenda sana jamani!”
“Wewe Upendo, humuogopi Mungu!”
“Namuogopa, lakini kwa nini ameamua kutupa jaribu kubwa namna hii?”
Padri Benedicto alikuwa akiishi peke yake nyumbani kwake, wafanyakzi wengi wa ndani aliokuwa akiwahitaji walikuwa wa kiume tu ambao wengi alikorofishana nao na mwisho wa siku kuwafukuza kihekima.
Baada ya kufukuza wafanyakazi watano, akaamua kuishi peke yake, hakutaka tena kuwa na mfanyakazi yeyote nyumbani kwake kwani aliona kama angeweza kufanya kazi peke yake pasipo mfanyakazi yeyote yule.
“Ila kuna msichana ana matatizo sana, naomba aje akusaidie padri,” alisema mama John, mwanamke aliyekuwa ameonana na Irakoze.
“Nimsaidie vipi?”
“Aje kufanya kazi hapa!”
“Msichana?”
“Ndiyo!”
“Hapana! Haiwezekani hata kidogo.”
Japokuwa padri Benedicto alikataa lakini mama John hakuacha kumbembeleza akubaliane naye kwani mtu kama yeye alihitaji mfanyakazi wa kike kwa ajili ya kufanya usafi wa nyumba muda wote kitu ambacho kwa kiasi fulani kikaanza kumuingia padri huyo.
Mbali na kumwambia hivyo, pia alimsimulia historia ya kusikitisha ya msichana Irakoze kiasi kwamba padri akaingiwa na huruma na kuona kwamba kumsaidia msichana huyo ilikuwa kama baraka kwa Mungu kwa kuwa ameamua kumtoa mtu fulani kutoka sehemu moja ya chini na kumuweka sehemu ya juu.
Wakakubaliana na hivyo mama John kuelekea nyumbani ambapo akamchukua Irakoze na kuelekea naye nyumbani hapo. 
“Ni mzuri mno, sijawahi kuona mwanaume mzuri kama huyu,” alijisemea Irakoze katika kipindi alichomuona padri Benedicto kwa mara ya kwanza.
Hiyo ndiyo ikawa siku ya kwanza kukutana kwa watu hao, Irakoze akaanza kazi ndani ya nyumba hiyo. Alikuwa msichana mwenye heshima kubwa, kila siku alikuwa mtu wa kuvaa mavazi marefu ambayo aliamini kwamba yasingemtia majaribu padri huyo.
Waliheshimiana mno, kila siku asubuhi walikutana sebuleni, walishikana mikono na kuanza kusali kisha kuendelea na ratiba nyingine. Katika kipindi chote hicho, Irakoze alikuwa kwenye mapenzi ya dhati kwa padri huyo, alitamani kumwambia ukweli kwamba alimpenda lakini aliogopa kufanya hivyo, akabaki akiugulia moyoni mwake tu.
Siku zikaendelea kukatika, heshima ilikuwa kubwa ndani ya nyumba, Irakoze aliendelea kufanya kazi ndani ya nyumba hiyo huku kila siku akijitoa kitendo kilichomfurahisha padri Benedicto kiasi kwamba alijiona kuchelewa mpaka kuchukua uamuzi wa kumuajiri mfanyakazi wa kike.
“Nakuja, niandalie chakula,” alisema padri Benedicto.
Siku hiyo hakuwepo nyumbani, alikuwa kanisani akiendelea na huduma, mawingu mazito yalitanda angani kuonyesha kwamba muda wowote ule mvua ingeweza kunyesha. Mara baada ya kumaliza kila kitu likiwa suala la kupika chakula, Irakoze akachukua khanga yake na kuelekea bafuni kuoga.
Alipokuwa huko, akasikia mvua kubwa ikianza kunyesha huku kiubaridi kikianza kuongezeka. Alichokifanya Irakoze, akatoka bafuni na khanga yake kisha kutoa ndoo nje kwa ajili ya kukinga maji ya mvua yaliyokuwa yakidondoka.
Mwili wake ukalowa, khanga ikanata mwilini mwake, umbo lake lenye mvuto, makalio yaliojaajaa yakawa yanaonekana vizuri kabisa. Hakuwa na wasiwasi wowote ule, alikuwa peke yake nyumbani hapo hivyo aliendelea kufanya kazi yake.
Wakati yupo hapo akiendelea kukinga maji, mara geti likafunguliwa na padri Benedicto kuingia. Irakoze hakumuona padri huyo, aliendelea kukinga maji huku wakati mwingine akijimwagia, kifua chake kikanata kwenye ile khanga, kila kitu mwilini mwake kilionekana wazi.
Padri Benedicto alipoona hivyo, moyo wake ukashtuka, hakupiga hatua, alibaki akimwangalia Irakoze huku akiwa na mwamvuli wake. Alibaki akimeza mate na maeneo ya zipu yake kuanza kusogea mbele. Alichanganyikiwa, kila alipojitahidi kuyaamisha macho yake, yaligoma kabisa kuhama.
Mpaka Irakoze anageuka na kumwangalia padri huyo, alikuwa hoi, kwa kujishtukia, Irakoze akamsalimia na kisha kuelekea ndani, sehemu ya nyuma ilikuwa ikichezacheza, padri akaona haiwezkani, japokuwa hakuwahi kulala na mwanamke yeyote maishani mwake, uzalendo ukamshinda, pepo la ngono likamwingia, mwili wake ukaanza kumsismka huku akihisi vijidudu fulani vikianza kumtembelea mwilini mwake, naye akaanza kuelekea ndani huku akiwa amechanganyikiwa kimahaba, pepo la ngono lilishamvaa, hakukubali, alitaka kuonekana kwamba hata na yeye alikuwa mwanaume.


INAENDELEA...                        

No comments:

Post a Comment