SIMULIZI

RUDI 03
HUSSEIN O. MOLITO
Kwa james ilikua ni kitu kingine kabisa baada ya kuruhsiwa kuushika mkono mlaini kabisa wa Jasmini huku tabasamu alilo liachia likimfanya James ahamie dunia nyingie. Hakumuachia haraka hadi pale Jasmini alipotumia nguvu kidogo kuutoa mkono wake na kumfanya James kurudisha network zake zilizopotea kwa sekunde kadhaa baada ya kushikana tu mikono na kuangaliana usoni.
“karibu sana Jasmini.. jisikie upo nyumbani.” Aliongea James na kumfanya Jasmini atabasamu na kwenda kukaa kwenye moja ya masofa yaliyopo hapo sebuleni.
“ngoja nimalizie kupika shoga yangu.. nakuja sasa hivi.” Aliongea Miriam
“ngoja na mimi nije jikoni nikusaidie shoga yangu.” Aliongea Jasmini na kunyanyuka.
“we kaa tu, mimi namalizia. Nilianza kupika muda mrefu sana. Yaani hapa kila kitu kimeshaiva. Naenda kumalizia tu hatua za mwisho.” Miriam aliongea hayo na kwenda jikoni kuendela na mapishi yake.
“karibu sana Jasmini.” Alikaribisha James na kumsogozea Jasmini rimonti zote alizokua nazo pale karibu.
‘mimi naenda ndani kujipumzisha kidogo. Kuwa huru Jasmini. Angalia kipindi ukipendacho na kama ni mpenzi wa filamu basi kua huru kwenda kuchagua filamu uipendayo na kuangalia.” Aliongea hayo James na kunyauka. Aliondoka na kumuacha mgeni huyo peke yake sebuleni.
Baada ya kuiva kwa vyakula vyote vilivyopikwa na Miriam. Alitenga kila kitu mezani na kweda kumuamsha mume wake.
Hapo wakakaa pamoja kwenye meza ya chakula na kupata chakula cha mchana.
Jasmini alishinda nyumbani kwa rafiki yake mpaka jioni. Hapo ndipo alipoaga na kuondoka.
“kumbe shemeji mtu poa sana… nilikua namuogopa nilivyomuona kwa mara ya kwanza.” Aliongea Jasmini wakati walipokua njiani yeye na rafiki yake Miriam.
“ndio hivyo… usipotee tena siku nyingine, ukishuka gari hapa unafika nyumbani ukinyoosha tu hii barabara moja kwa moja.” Aliongea Miriam na kumuonyeshea njia Jasmini.
“yaani wewe unataka niwe nakuja kwako tu, mbona huniambii ni lini utakuja kwetu?” aliuliza Yasmini.
“nitakuja jumamosi ijayo… nakuahidi.” Aliongea Miriam na wakati huo huo daladala ikawa imeshafika.
“bye mpenzi… tutaonana jumamosi kama kweli utakuja.” Aliongea Yasmini na kupanda gari hiyo na ndipo Miriam alipoonyesha mkono ishara ya kumuaga rafiki yake na kurudi nyumbani.
Maisha ya ubabe na maamuzi ya upande mmoja ndio aliyotakiwa kuyazoea Miriam pindi atakapo amani na mume wake. James hakua na muda maalumu wa kurudi nyumbani. Na anaporudi pia hahitaji maswali juu ya wapi alikuwepo.
Ilimlazimu Miriam avumilie tu na aone ni hali ya kawaida japokua kuna muda alikua akiumia moyo hasa akisikia tetesi za mume wake kutembea na wadada wanaoanya kazi bar.
Starehe ya James ni pombe. Na mara nyingi akilewa hulala nje ya nyumba au kurudi usiku ukiwa umeshasogea sana.
Siku moja James alikua kwenye moja ya Bar kubwa kinondoni mida ya saa kumi na moja jioni. Ilikua ni bar ambayo hajawahi kwenda kunywa hata siku moja. Sema alivutiwa tu mandhari ya bar hiyo na jinsi ilivyochangamka.
Alitulia na kuangalia sehemu nzuri na kukaa huku akiliweka gazeti lake alilolinunua kwenye meza.
“nikuhudumie nini?” aliuliza muhudumu mmoja aliyefika hapo kumuhudumia.
“niletee maji ya Kilimanjaro makubwa.” Aliongea James na muhudumu huyo aliondoa na kurudi na maji hayo. Baada ya kumuwekea kwenye meza, muhudumu uyo aliendelea kuwahudumia wateja wengine.
Akiwa anakunywa maji yae taratibu, ndipo kwa mbali alipoweza kumuona Jasmini akiwa na marafiki zake wawili wakike wakipiga story na kunywa Savana. Alinyanyuka na kuwasogelea.
“habari warembo!”
Alisalima na kuwafanya wote wamgeukie. Jasmini alimkumbuka na kumsalimia. Kwakua James alikua sio mkubwa sana. Wote walimpa salamu ya vijana na kumfanya James atabasamu.
“naweza kukaa hapa. Au nitawatibulia story zenu?” aliuliza James na kuwafanya wasichana hao watabasamu.
“karibu tu shemeji.. wala hakuna cha maana hapa tunachoongea zaidi ya kufurahi tu na kula mishikaki.” Aliongea Jasmini na kumfanya James avute kiti na kukaa.
“mlikua mnahudumiwa na nani?” aliuliza James.
“na Yule dada pale.” Jasmini aliomuonyesha Yule muhudumu aliyemuhudumia hata yeye.
James alimuita ana kuomba apigiwe hesabu zote walizokunywa hao wasichana pamoja na maji waliyoagiza.
“jumla ni elfu kumi na nane na mia tano.” Alijibu msichana huyo baada ya kuangalia karatasi yake.
“haya.. hii tunalipa bili za nyuma. Kwa sasa tunaanza upya na chenji utakunywa soda na wewe.” Aliongea James na kulipia kiasi cha shilingi elfu ishirini.
“ahsante sana.” Aliongea msichana huyo na kutabsamu.
‘kuweni huru… kama mnakunywa chochote ruhusa ya kuagiza nimetoa.” Aliongea James na kuwafanya wasichana hao waliokua wanakunywa savanna zao huku wakilambalamba kama walikua wakizibembeleza zisiishe mapema.
“niitieni mtu wa nyama. Naona pamepooza hapa.” Aliongea James na mtu wa jikoni akaitwa kwenye meza hio.
“nichomee miguu miwili ya mbuzi na mishikaki hamsini… fanya haraka uje na bili yako kabisa nikulipe.” Alingea hayo James na mtu wa jikoni akaitikia na kwenda kuandaa hiyo oda.
“shemeji kula nyama, kula bia. Usiogope ukiwa na mimi shemeji yako wa ukweli.”
Aliongea James baada ya kilevi kuanza kumkolea. Hata Jasmini nae alianza kulewa na hao rafiki zake waliokua wakizifakamia pombe ndio walipunguza spidi ya kunywa huku wakijitahidi kwenda chooni ili kupunguza hali ya kimea kilichokua kikiwapanda kila dakika.
Walikaa mpaka saa nne usiku. James aliteketeza kiasi cha shilingi laki sita pale pale na kuwafanya wadada waliokua wanakunywa pombe kuzidiwa kabisa na mmoja wapo akazima pale pale.
“shemeji utaweza kuondoka kweli au niwatafutie chumba mlale?” aliuliza James kwa sauti ya kilevi na isiyokua na aibu hata kidogo.
“ Mi siwezi kwenda nyumbani, wewe nifanyie tu mpango wa chumba ili niweze kupumzika.” Aliongea hayo Jasmini na kumfanya James aende conter na kulipia chumba kwa ajili ya wasichana hao.
Yeye alijitahidi kujikokota mpaka kituo cha kukodi taksi na kurudi nyumbani kwake.
Miriam hakua na shida, bali furaha yake ni kushuhudia mume wake kua ameruudi salama bila kujali amerudi saa ngapi.
Palipokucha asubuhi, alienda bar kukata kilevi alichokua nacho na kuitazama simu yake. Aligundua kua kuna missed call ya Jasmini. Alikumbuka kua alimpa namba yake na Jasmini alimbipu. Ndipo alipojaribu kumpigia ili kumjulia hali.
“niambie shemu lake.” Aliongea James baada ya Jasmine kupokea simu yake.
“yaani shemeji wewe, umenifanya mpaka muda huu naona mia mia tu hapa.” Aliongea Jasmini na kulegeza sauti hadi mwisho kutokana na uchovu aliokua nao.
“usijali, we kunywa supu na soda, hicho kimea kilichopo kichwani kwako kitaondoka chote.” Aliongea James na kumfanya Jasmine atabasamu.
“shemeji unaweza kuja asubuhi hii?... au umebanwa?” allulza Jasmini swali la mitego na kumfanya James atabsamu.
“sisi tunavyoishi hakuna wa kumbana mwenzie. Nahisi ndio maana hatugombani. Hivyo wewe niambie unahitaji nifike hapo saa ngapi. Maana asubuhi inaisha saa tano huko.” Aliongea James.
“ukija muda huu nitafurahi sana shemeji yangu.” Aliongea Jasmini huku akiwa amezidi kuilegeza sauti yake na kuwa ya kudeka zaidi.

ITAENDELEA……….


RUDI 02
HUSSEIN O. MOLITO
 “kwa hiyo ulitaka nije kulala nao hapa ndani… si ndio?” aliongea James na kumtazama mke wake kwa dharau kasha akaondoka.
“naondoka. Nitarudi nikijisikia. Na ukiongea naondoka tena. Mpaka uache huo mdomo wako. Pumbavu kabisa wewe.” Aliongea James na kuondoka zake.
Hali iliyomfanya mwanamke huyo mkjamzito aka echini ya kochi na kuamua kuangua kilia huku machzi yakilowanisha mashavu yake.
Siku hiyo ilipita tena bila James kurudi nyumbani. Alliirudi siku inayofuata huku akiwa amelewa chakari. Aligonga mlango kwa fujo huku akimtukana Miriam
Miriam alienda kufungua mlango na kumshuhudia mume wake akiingia ndani huku akipepesuka na kwenda kujilaza kitandani.
Kwakua hakuhitaji tena matatizo, alienda kumvua viatu na kuviweka mahala pake. Aliandaa chai na kuitenga mezani kisha yeye mwenyewe kutoa nguo na kuanza kuzifua.
Baada ya James kuamka. Alienda kunywa chai na kutoka nje. Hakumuongelesha kitu chochote Miriam zaidi ya kumuangalia tu na kutoka huku kimea kilichokua kichwani mwake kikiendelea kumtesa.
Baada ya james kutoka nyumbani kwake, alienda moja kwa moja mpaka Bar na kulazimika kupata supu na soda ili aweze kukata kilevi alichojitwika usiku kucha.
“nakuona bosi.. fanya basi na mimi nishtue tumbo.” Ilisikika sauti ya msichana mmoja ambaye ni muhudumu kwenye bar hiyo.
“unataka kunywa nini mrembo?” aliuliza James huku anatabasamu
“mimi ninunulie tu supu kama hiyo unayokunywa wewe.” Aliongea muhudumu huyo na kumfannya James aingize mkono wake mfukoni na kutoa noti ya shilingi elfu kumi.
Lipia bili yangu ya supu na bili yako. Kisha chenji utabaki nayo.” Aliongea hayo Jmaes na kumfanya muhudumu huyo afurahi sana na kumshukuru.
Baada ya kupata supu na soda baridi. Ndipo alipoanza kujisikia vizuri na kurudi nyumbani kwake.
Alimkuta mke wake akimalizia kufua na kumpita tena bila kuongea naye kitu chochote. Alienda sebuleni na kuwasha Televisheni. Alichukua rimonti ya king’amuzi na kuweka stesheni aipendayo.
Baada ya Miriam kumaliza kufua. Alirudi ndani na kumfuata mume wake kwa upole kabisa.
“nikupikie chakula gani mume wangu?” aliuliza Miriam kwa sauti ya upole na kumfanya James amuangalie.
‘kumbe adabu unayo… pika ugali na samaki.” Aliongea James na kuingiza mkono mfukoni na kumpatia mke wake noti ya shilingi elfu kumi.
Miriam alitoka na kwenda kununua samaki . huko njiani ndipo alipokutana na msichana ambaye walikua wanasoma wote shule moja kipindi alipokua sekondari.
“Miriam, hata siamini. Umekua mdada mwenyewe mpaka umeamua na kuzaa kabisa.” Aliongea msichana huyo huku akiwa na furaha ya kuonana na Miriam.
“si unajua maisha tu Jasmini. Mii mwenywe natamani sana ningekua shuleni kama wewe.” Aliongea Miriam.
“vipi, unaishi na shemeji au ndio wale wale baada ya kutia mimba wanatoka mbio?” Aliongea Jasmini na kumfanya Miriam atabasamu.
“mama nifungie haraka… nachelewa.” Aliongea Miriam na kumuharakisha muuza samaki baada ya kumpa maagizo na kumlipa kiasi cha fedha kulingana na mahitaji aliyochukua kwa muuza samaki huyo anayemiliki na genge pia.
“twende kwangu mpenzi, angalau ukatie hata Baraka.” Alongea Miriam.
“nitakuja siku nyingine nyonyo… leo nimechelea vipindi. Halafu sio vizuri shemeji akiniona na hizi sare za shule.” Aliongea Jasmini na kuonekana kukataa kabisa kwenda kwa Miriam akiwa na sare za shule.
“na mimi ningekua kidato cha sita kama wewe mwenzangu. Huu ukahaba huu umenifelisha mambo yangu yote na mipango yangu yote imeyeyuka.” Aliongea Miriam na kuonyesha dhahiri kua anajuta kukubali kuolewa na mvulana huyo ambaye hataki tena kusikia mambo ya shule.
“usiseme hivyo.. maadamu umepata mtu wa kukusitiri basi shoga yangu tulia.” Aliongea Yasmini na kumfanya Miriam atabasamu.
“ngoja nikapike mie. Chukua basi namba yangu. Utanitafuta ukipta nafasai. Maana sipati picha ulivyokutana na machizi wapya huko shuleni.” Aliongea Miriam na kumfanya Jasmini acheke.
“yaani… huku kuna machizi hata mimi mwenyewe naomba poo. Halafu katika kundi letu ni mimi peke yangu ndio sina mimba. Wengi wana watoto na wengine wana mimba kama wewe. Ila wengi wamekimbiwa na wengine waliozaa wamewaongezea mizigo wazazi wao. Sasa ninachokushauri wewe tulia ili familia yako iishi kwenye mstari ulionyooka.” Aliongea Jasmini na kuomba peni dukani na kuandika namba ya Miriam.
“nitakupigia usiku wa leo nikirudi tu nyumbani. Nadhani jumamosi nitakuja nyumbani kwako. Unipikie mahanjumati na mahanjamu mama kijacho.” Aliongea Jasmini na kuondoka huku wawili hao kila mmoja akiwa amejawa na tabsamu.
Miriam alirudi nyumbani na kumuandalia mume wake chakula anachokipenda na kutenga mezani. Walikula kwa pamoja huku MMiriam akiuchunga mdomo wake asije kuulizia habari a mume wake kuanz a kulala nje ya nyumba hiyo.
Usiku walilala pamoja. Lakini James hakupitiwa na usingizi mapema kutokana na kuwa bize na simu yake. Muda wote alikua akiichezea na kuchat na watu mbali mbali.
Huo ndio ulikua ugomvi wa kwanza wa Miriam na mumewe. Lakini mwisho wa siku alizoea na ndio ikawa kawaida kwa mume wake kuchati na watu mbali mbali mpaka muda ambao hata Miriam hajui kutokana na kupitiwa na usingizi.
Palipokucha, mume wake aliacha hela mezani na kutoka kwenda kwenye ofisi yake anayomiliki yeye mwenyewe ndio maana anaenda muda anaotaka kwakua wafanya kazi walikua wanatosha kuhudumia watu hata kama yeye asipokuwepo.
Jiioni ya siku hiyo Miriam alipigiwa simu na rafiki yake na ikawa sababu ya yeye kuiihifadhi namba ya Jasmini kwenye kitabu chake cha majina ya simu yaliyokua kwenye simu yake.
Siku ya jumaamosi, alipigiwa simu na Jasmini na kumpa taarifa juu ya ugeni wake. Miriam alijitahidi na kupia pilau la kuku. Na upande wa pili akaivisha wali wa maua. Alianda rosti la maini na kufanya aamini kua mgeni wake atakifurahia sana chakula hicho.
Alipata amani baada ya simu yake kuita na kutokea jina la rafiki yake kwenye kioo cha simu yake.
“nipo hapa tulipokutana siku ile.” Aliongea Jasmini na kumfanya Miriam amuambie asubri hapo kwa dakka mbili tu.
Alimfuata mgeni wake na kurudi nae nyumbani. Alimtambulisha rafiki yae huyo kwa James. Maana siku hiyo James alipendelea kutulia nyumbani. Na hata kama akitaka kunywa basi huijaza friji vinywaji mbali mbali hivyo kumfanya asitamani kutoka kabisa.
“huyu ni rafiki yangu toka kidato cha kwanza… anaitwa Jasmin. Jasmin. Huyu ndio baba kijacho wangu.” Alitambulisha Miriam na kumfanya Jasmin ampe mkono James.
Kwa james ilikua ni kitu kingine kabisa baada ya kuruhsiwa kuushika mkono mlaini kabisa wa Jasmini huku tabasamu alilliachia likimfanya James ahamie dunia nyingie. Hakumuachia haraka hadi pale Jasmini alipotumia nguvu kidogo kuutoa mkono wake na kumfanya James kurudisha network zake zilizopotea kwa sekunde kadhaa baada ya kushikana tu mikono na kuangaliaa usoni.

ITAENDELEA…..







RUDI 01
HUSSEIN O. MOLITO
Alarm iliyotegeshwa mida ya saa kumi na moja kamili ilianza kulia kwa fujo baada ya muda husika kufika. Kwa uchovu kabisa kutokana na kuchelewa kulala siku iliyopita, ZABRON aliamua kulitupa shuka pembeni na kuizima saa yake hiyo iliyokua ikitoa mlio mkali.
Alipapasa kwenye meza na kuchukua kibiriti. Alichukua njiti moja na kukiwasha kibiriti hicho kilicholeta mwanga hafifu na kumfanya aweze kuiona kandili yake iliyokua kwenye meza hiyo iliyokua mita moja tu kutoka kwenye usawa wake wa kitanda.
Baada ya kuiwasha kandili hiyo. Aliufuata mswaki wake na kuuweka mdomoni bila kujali kama bado hajaweka dawa ya meno kwenye mswaki wake. Hilo alilifanya kwakua tu alikua anafahamu kua hiyo dawa ya meno alikua ameitumia kwa mara ya mwisho miezi miwili iliyopita na hakua na bajeti ya kuinunua tena kwa wakati huo.
Alimimina maji nusu kenye ndoo yake a kuufungua mlango wake a kutoka nje. Baada ya kuvaa ndala zake, alihesabuhatua kama ishirini na ndipo alipokfikia choo na bafu ambavyo vyote vipo sehemu moja.
Baada ya kumaliza kuoga, alirudi ndani na kujiandaa tayari kw ajili ya kwenda kusaka riziki.
Kwakua Mabibo bonde la mchicha sio mbali sana na kiwanda cha Vitenge na Khanga cha NIDA sio mbali sana na anapoishi, basi ilikua ni kazi yake kutembea kwa mguu hadi kazini kwake. Ilikua inamchukua mwendowa nusu saa au dakika arobaini sik nyingine.
Alifika kiwandani hapo na kukutana na wenzake wengi ambao alikua wanasubiri muda w akuingia ufike.
Walitwa kwa majina na kuingia huku wakiwaacha vibarua wengine wakiwa nje baada ya kukosa nafasi kutokana na idadi ya wafanyakazi waliokua wakihitajika siku hiyo.
Baada ya kupiga kazi kwa masaa nane. Ndipo alipopokea ujira wake ambao ni shilingi elfu nne na mia tano. Akatoka na kwenda kwa mama muuza chakula na kununua chakula cha shilingi elfu moja na mia mbili na kushushia na maji ya kufunga mawili.
Kwa kila siku alikua akihakikisa anarudi na shilingi elfu tatu nyumbani. Hivyo mara zote Zabron hua hanywi chai. Anasubiri chakula cha mchana na ndipo anapozitibu njaa zote alizokua nazo. Hata chakula hua anapendelea makoko au matandu, kwa maana watu wanaokula vyakula hivyo vya chini huwekewa ujazo mkubwa kuliko chakula kilichokua kwenye hali ya kawaida.
Baada ya kufika nyumbani. Ndipo alipoamua kujipumzisha ili kupuguza uchovu aliokua nao.
Ilipofika saa kumi na moja na nusu, Zabron aliamka na kwenda uwanjani kutazama mpira. Alirudi nyumbani kwake saa kumi na mbili na nusu na ndipo alipoenda kuoga kwa mara nyingie ili apate akili mpya.
Mbali na kufanya kazi kiwandani. Zabron ana ndoto nyingi. Moja wapo kuja kuwa muandishi mkubwa sana wa vitabu vya riwaya, tamthilia na mashairi.
Alinunua daftari lake kubwa kabisa na kuanza kuandika story moja ya hisia aliyoitunga kichwani mwake.
Mara nyingi hua anaandika karatasi sita mpaka saba ndio anaridhika. Maana hutumia muda wa masaa mawili mpaka matatu kutimiza karatasi hizo na ndipo anapotoka na kwenda kutafuta chakula ambacho hununua kwa shilingi elfu moja na kumfanya awe na uwezo wa kuhifadhi shilingi elfu mbili kwa siku.
Maisha yalikua ni ya kawaida kwake kwakua alishayazoea. Na hakuonekana kusononeka kwakua alikua na uwezo wa kulipa kodi ya chumba bila maatizo yoyote yale. Kubwa zaidi anachoshukuru ni kwamba, kazini kwao alikua anategemewa sana. Hivyo alikua na uhakika wa kuingia kila siku na sio wengine ambao mara nyingi walikua wanapenda kuingia lakini siku nyingine wanakosa nafasi iwapo watahitajika wafanyakazi wa chache kwa siku hiyo.
Hayo ndio maisha ya Zabron. Na mara zote kwake huwa ni furaha kwenda kazini siku za sikukuu. Maana huwa wanalipwa elfu kumi na kumfanya afurahie zaidi kuwepo kazini siku za sikukkuu kuliko kubaki nyumbnani.
Hakuwahi kuwa na mwanamke katika maisha yake. Maana aliwahi kuanza kujitegemea na baadae kuwa mlezi akiwa na umri wa miaka kumi pekee.
Alisoma shule ya awali na msingi ambapo hakufanikiwa kufika hata darasa la saba. Aliacha shule akiwa darasa la tatu pekee baada ya nguzo ya familia kuteketea.
Zabron alianza kusimama kama baba akiwa na umri wa miaka kumi huku akitakiwa kumuuguza mama yake mzazi ambaye alikua kiugua virusi vya Ukimwi.
Ndugu wote waliwatenga hasa baada ya kumshutumu mama yake Zabron kua ndio aliyemuambukiza baba yake ugonjwa huo.
Ukweli juu ya maisha ya mama yake Zabron alikua akiujua Zabron japo alikua na umri wa miaka sita pekee. Hata shule ni mama yake ndio alikubali kupigwa na baba yake ili mradi aweze kupata elimu. Japo hakupata elimu kubwa, lakini daima anamuombea mama yake alazwe mahala pema peponi baada ya kumsaidia angalau akajua hata kusoma na kuandika.
“mwanangu. Najau umri wako bado mdogo sana na kuna uwezekano ukashindwa kuhimili haya mazito nitakayokuelezea. Ila amini kuwa wazazi wako tuna miaka michache sana ya kuishi. Nakuomba usome kwa bidii ili aweze kuyaokoa maisha yako kwenye ulimwengu huu ambao tutakuacha. Huo ulimwengu hautakua na ndugu wala rafiki atakaye kuthamini. Ulimwengu ambao unatakiwa ujishike mwenyewe na utakapopata bahati ya kubebwa basi jishikilie vizuri na uwe mstaarabu ili usimkere huyu ambaye ataamua kukubeba na kukufikisha mahali. Nakuambia soma kwakua mwisho wako naujua mwanangu. Niombee maisha marefu. Angalau miaka kumi mbele. Pengine utaweza hata kufika la saba na kufuta ujinga. Najua unajua kua baba yako hawezi kukusomesha na hataki kusikia habari za shule ya awali. Lakin mimi nitakupeleka na ujitahidi kumsikiliza mwalimu ili mwakani ukaanze la kwanza.”
Hayo yalikua ni maneno ya mama yake Zabron akimuambia mtoto wake pindi alipofikisha umri wa miaka sita pekee.
Yalikua ni maneno yasiyokua na uzito moyoni wa Zabron kwa wakati huo. Lakini kumbukumbu ya maneno hayo yalikua yamepokelewa vizuri kwenye ubongo utunzao kumbukumbu. Kwani kila anavyozidi kukua ndipo maana halisi ya kile alichokua akiambiwa kilikuja na kujirudia katika ubongo wake. Ndipo kila tamshi la mama yake alipoliona lina ukweli ndani yake.
“ulazwe mahala pema peponi mama.”
Alijikuta akiongea hayo kila akiyapitia mazito ambayo mama yake alishamtabiria akiwa na umri mdogo kabisa.
********
“nimekuambiaje, ukitaka kujua nikiwa na hasira hua nakuwaje, basi endelea kuniuliza maswali ya kijinga.” Aliongea baba mmoja kwa hasira huku akimfokea mke wake ambaye nae alionekana kua na hasira pia.
“hapana James, leo utaniambia tu jana umelala wapi?” aliongea mwanamke huyo mjamzito na kumfanya James amuangalie na kumshika mikono yake kwa nguu.
“isingekua hii mimba ningeshakuvuruga sasa hivi. Mimi mwanaume ndani ya hii nyumba. Mwanaume haulizwi ulikua wapi au unatoka wapi. Mwanaume anapokewa alichokileta kisha ndio kwa utaratibu unahoji na sio kuropoka na kupaza sauti tu. Hivi hujafundwa wewe huko kwenu jinsi ya kumpokea mwanaume pindi akichelewa kurudi?.. unakua kama umezaliwa shimoni bwana.” Aliongea James na kuiachia mikono ya mke wake.
“James leo unanitusi?” aliuliza mwanamke huyo kwa hasira.
“usinipigie kelele wewe mwanamke. Maana ukiendelea kuongea nitaondoka tena.” Aliongea James na kwenda kukaa kwenye kiti.
“mimi leo hata sikubali.. liwalo na liwe.” Aliongea mwanamke huyo na kumfuata mpaka pale James alipokaa.
“naomba niambie ni wapi ulipoenda kulala jana.. yaani James mbali na visa unavyonifanyia, bado unaamua kulala na wanawake zako huko nje kweli?” aliuliza Mwanamke huyo huku machozi yanamtoka.
“kwa hiyo ulitaka nije kulala nao hapa ndani… si ndio?” aliongea James na kumtazama mke wake kwa dharau kisha akanyanyuka.
“naondoka. Nitarudi nikijisikia. Na ukiongea naondoka tena. Mpaka uache huo mdomo wako. Pumbavu kabisa wewe.” Aliongea James na kuondoka zake.
Hali iliyomfanya mwanamke huyo mjamzito akae chini ya kochi na kuamua kuangua kilio huku machozi yakilowanisha mashavu yake.

ITAENDELEA…………..


USIWAELEZE WATU SHIDA ZAKO, KWA SABABU:-

1. 3/4 (ROBO TATU) YA UTAOWAAMBIA HAWATAKUSIKILIZA
2. 1/2 (NUSU) YA UTAOWAAMBIA WATAKUCHEKA
3. 2/3 (THELUTHI MBILI) YA UTAKAO WAAMBIA NAO WAKO NA SHIDA KAMA WEWE!!!!
HIVYO CHUNGA SANA KINYWA CHAKO JUU YA MABO YAKO:

VITUKO MASHULENI:




Mwalimu katoa kazi kwa watoto, kila mmoja atunge sentensi kutokana na maneno yafuatayo;
  1. TUMAINI
  2. SUKARI
Mwanafunzi: 
1.SENTENSI: TUMAINI TWA MBUZI NI TUTAMU KULIKO TWA NG'OMBE

Mwanafunzi:
2. SENTENSI: NILIKUNYWA CHAI ASUBUHI NA MAPEMA SANA:
Mwalimu: SASA NENO SUKARI LIKO WAPII??
Mwanafunzi: SUKARI IMO NDANI YA CHAI, MWL UTAKUNYWAJE CHAI BILA SUKARI KWELI INAWEZEKANA:
                                         




Christmas
C is for Christmas I wait for all year.
H is for holly that brings so much cheer.
R is for reindeer that pull Santa's sleigh
is for icicles dripping all day.
S is for Santa who seldom is seen.
T is for tree that is lovely and green.
is for mistletoe, hugs and a kiss.
A is for angel who looks just like this.
S is for stockings all loaded with toys
From all of the elves to the girls and the boys.



Christmas Time (Farmer in the Dell)
Christmas time is here
Christmas time is here
Hustle bustle busy time
As Christmas time is here

Christmas trees are up
Christmas trees are up
Tinsel balls and popcorn too             

As Christmas time is here

Santa Claus is here
Santa Claus is here
Bringing gifts and stockings too
As Christmas time is here

Christmas time is a beautiful time
With lights all red and green,
I think it is the prettiest time
That I have ever seen!




Christmas Acrostic (may be used for a concert)
C - is for the Christ child born upon this day
H - is for the holly to make our mantle gay.
R - is for red ribbon to wrap the parcels tight
I - is for the icicles On this cold winter night.
S - is for dear Santa Please leave him a treat
T - is for the turkey It is so good to eat.
M - is for the manger Where Baby Jesus lay,
A - is for the angels On that first Christmas Day.

S - is for the stockings Hanging in a row With candy canes out of the top and bulges in the toe.


Isn't it strange?
• Isn't it strange how a 20 dollar bill Seems like such a large amount when You donate it to church, but such a Small amount when you go shopping?

Isn't it strange?
•Isn't it strange how 2 hours seem so long when you're at church, and how short they seem when you're watching a good movie?

Isn't it strange?
 •Isn't it strange that you can't find a word to say when you're praying, but you have no trouble thinking what to talk about with a friend?

Isn't it strange?
•Isn't it strange how difficult and boring it is to read one chapter of the Bible, but how easy it is to read 100 pages of a popular novel?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how everyone wants front - row - tickets to concerts or games, but they do whatever is possible to sit at the last row in Church?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how we need to know about an event for Church 2 - 3 weeks before the day so we can include it in our agenda, but we can adjust it for other events in the last minute?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how difficult it is to learn a fact about God to share it with others, but how easy it is to learn, understand, extend and repeat gossip?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how we believe everything that magazines and newspapers say, but we question the words in the Bible?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how everyone wants a place in heaven, but they don't want to believe, do, or say anything to get there?

Isn't it strange?
• Isn't it strange how we send jokes in e - mails and they are forwarded right away, but when we are going to send messages about God, we think about it twice before we share it with others?

Isn't it strange?
• IT'S STRANGE ISN'T IT?
Now that you've read this message, forward it to anybody that you consider a friend. If you don't do it, not only you will deprive yourself from being blessed, but you will also do that to others who may need God in their life.

Isn't it strange?
YES, IT IS STRANGE …

GOD BLESS YOU !!!!!!!!!!!!

If your boss comes to you and says:
There will be no salary increases for this year ……….. 
There are no bonuses either ……… All overtime has been cancelled No expenses will be paid.....
And there will be no additional healthcare !



What will your reaction be ? …………………….!! 

No comments:

Post a Comment