Tuesday 23 January 2018

HADITHI!!!......SEHEMU YA NNE

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 04

Hakukuwa na kitu alichokifikiria zaidi ya ngono, alitaka kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake, hakutaka kumuacha Irakoze hivihivi, alitaka kuhakikisha kwamba kibaridi kile kilichokuwa kikipiga, ni lazima kikatishwe na joto la mwili wa Irakoze.
Alitembea kwa harakaharaka kama mtu aliyekuwa akiwahi kitu fulani, alipofika ndani, akasikia maji yakimwagika bafuni, akajua ni lazima Irakoze alikuwa ndani ya bafu lile akioga. Hakutaka kujiuliza, akausukuma mlango, ukafunguka, naye akazama ndani.
“Aaaah! Padri!” alisema Irakoze huku akijifanya kujificha.
“Usiogope.”
“Naoga padri, naomba uende nje,” alisema Irakoze.
Hiyo ilikuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze, padri Benedicto hakutaka kutoka, alichokifanya ni kuusukuma mlango na kubaki humohumo. Kwa sababu naye mwenyewe alikuwa akimpenda sana padri huyo kutokana na uzuri wa sura yake, hakutaka kuiacha nafasi hiyo, akaitumia vilivyo na hivyo kujikuta wakigusana miili yao, maji ya bomba la mvua yaliwamwagikia, walipapasana hapa na pale na hatimaye kufanya dhambi.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kila kitu, mchezo walioufanya siku hiyo ukampelekea hata Irakoze kuhama chumba chake na kuhamia kwa padri huyo. Waliishi kama mume na mke, hakukuwa na mtu yeyote nje ya nyumba hiyo aliyefahamu kile kilichokuwa kikiendelea.
Ilikuwa siri kubwa mno, na kila alipotoka nyumbani, padri Benedicto alijifanya kuwa mtakatifu mno, kumbe jana yake tu alikuwa amelala na Irakoze usiku mzima. 
“Tumsifu Yesu Kristo!” alisema padri yule.
“Milele Amina.”
Usiri mkubwa uliendelea, padri Benedicto hakutaka kuonekana kuwa rahisi kwa wanawake wengine ambao walimfuata kwa kisingizio cha kutaka kumwagiwa maji ya baraka kumbe upande wa pili walikuwa wakihitaji kulala naye.
Mwanamke aliyekuwa naye nyumbani, alimtosheleza na hata alipokuwa akifuatiliwa na wanawake wengine, hakutaka kuwakubalia kwa kisingizio kwamba alikuwa mtu wa Mungu na hakutakiwa kuoa kutokana na cheo alichokuwa nacho.
“Ninakupenda mpenzi,” alisema Irakoze.
“Nakupenda pia!”
“Hivi siku ikitokea nikapata mimba?”
“Utapataje? Haiwezekani, tupo makini kila siku, wala usijali, mimba haiwezi kutokea,” alisema padri Benedicto.
Hakukuwa na aliyejali sana, padri Benedicto alikuwa na uhakika kwamba kila kitu ambacho kiliendelea kamwe asingeweza kumpa mimba msichana huyo. Siri kubwa iliendelea, waliishi kama mume na mke.
Wakati mwingine padri Benedicto hakuwa akielekea kanisani, alibaki nyumbani kwa ajili ya kufanya mapenzi na msichana huyo tu. Japokuwa kila siku washirika walimtembelea padri wao lakini hakukuwa na yeyote aliyefahamu kama watu hao walikuwa kwenye uhusiano mkubwa wa kimapenzi.
Siku zikakatika, miezi ikaendelea kukatika. Padri Benedicto akaingia moja kwa moja kwenye ulimwengu wa kishetani, naye akaanza kwenda klabu usiku, akaanza kunywa pombe kali zilizomfanya hata kutokuthamini kazi yake ya upadri.
Mabadiliko yale yalimshangaza mno Irakoze, hakutaka kuzungumza naye sana kwa kuamini kwamba mabadiliko hayo yangetokea kipindi hicho tu, cha kushangaza, hakuacha, kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo alivyozidi kubadilika.
Kila siku usiku, akawa mtu wa kutoka na kwenda klabu, huko, alikuwa akivalia kofia kubwa ili asijulikane na mtu yeyote. Alikunywa pombe na wakati mwingine kulewa mno, maisha ya kidunia yakaanza kumteka kiasi kwamba wakati mwingine alipokuwa akirudi nyumbani na kulewa, kesho yake hakwenda kabisa kanisani kwani kichwa bado kilikuwa na pombe kali.
“Kuna kitu ninataka kuzungumza nawe,” alisema Irakoze.
“Kitu gani?”
“Mbona sikuelewielewi! Hebu tulia kwanza,” alisema msichana huyo.
“Nitulie kivipi tena? Unajua leo lini?”
“Jumapili!”
“Basi subiri kwanza niende kanisani,” alisema padri Benedicto.
Japokuwa Irakoze alikuwa na jambo muhimu la kuzungumza na padri huyo lakini hakuweza kupata nafasi hiyo. Ilikuwa ni Jumapili ya tatu tangu asitishe kwenda kanisani kwa kisingizio cha kuwa bize kufuatilia mizigo iliyotumwa kutoka nchini Vatican kwa maendeleo ya kanisa hilo.
Ingawa alikuwa akidanganya kwa kujifanya mfuatiliaji namba moja lakini hakukuwa na mtu aliyemshtukia kwamba ni pombe za janausiku ndizo zilizomuweka nyumbani na kushindwa kabisa kwenda kanisani.
Siku hiyo alipanga kwenda huko kwa ajili ya kuhubiri, alijua ni kwa jinsi gani washirika wake walikuwa wamemkumbuka kwani katika kipindi chote alichokuwa akikaa nyumbani, alikuwa akipigiwa simu na kuuliziwa maendeleo yake.
Siku hiyo alipoonekana kanisani, kila mshirika alikuwa na furaha, wiki tatu ambazo hakuonekana kabisani hapo zilionyesha kila dalili kwamba kanisa hilo lingepwaya sana na hatimaye lingeweza kupotea kabisa.
Ujio wake ukaibua ari ya washirika wake na hatimaye kuendelea na huduma kama kawaida. Kwa kumwangalia, usingeweza kuamini kwamba jana usiku alishinda klabu ya muziki, alionekana mchangamfu na hata macho yake hayakuonyesha kabisa kama alikuwa mtu aliyekesha.
Japokuwa alikuwa akihubiri na kuwabariki watu waliokuja na watoto wao kanisani hapo lakini mara alipokumbuka kwamba Irakoze alitaka kuzungumza naye asubuhi ya siku hiyo, ghafla amani ikakatika.
Hakukuwa na kitu alichokiogopa kama kuambiwa kwamba mtu fulani alitaka kuzungumza naye. Hakujua ni kitu gani kiliendelea lakini mwisho wa siku akataka kukaa chini na msichana huyo ili kumsikia alikuwa na jambo lipi la kuzungumza.
Ibada ilipokwisha, hakutaka kukaa kanisani na kuwasalimia washirika, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea nyumbani kwake. Alipofika huko, kama ilivyokuwa siku nyingine, alipokelewa kwa mahaba mazito mpaka chumbani, hata kabla hajafanya lolote, akavuliwa joho na kupigwa mabusu mfululizo, ndani ya dakika tatu tu, alibaki kama alivyozaliwa.
Kilichofuata ni kilekile kilichokuwa kikitokea siku zote, walifanya dhambi kwa takribani masaa matatu na ndipo kila mmoja akaridhika na kutulia pembeni ya mwenzake.
“Aya niambie ulitaka kuniambia nini asubuhi,” alisema padri Benedicto.
“Una moyo?”
“Ninao. Hebu niambie wala usinitishe.”
“Usiogope, nafikiri ni baraka kutoka kwa Mungu.”
“Ipi?”
“Nina mimba yako!”
“Unasemaje?” aliuliza padri huku akionekana kushtuka.
“Nina mimba yako!”
Padri Benedicto akasimama na kuanza kumwangalia Irakoze, hakuamini kile kilichokuwa kimeongelewa maahali hapo, alimwangalia msichana yule, ndiyo kwanza alikuwa akitabasamu kwa furaha, hakuonekana kujua ni kwa jinsi gani padri alijisikia moyoni mwake.
Kama masharti ya kanisa hilo, hawakutakiwa kuoa, si kuoa tu, hawakutakiwa kuwa na mtoto pia. Kauli ya Irakoze ilimuweka katika wakati mgumu,  mwili wake ukaanza kutetemekea huku kijasho chembamba kikimtoka.
“Unasemaje?”
“Nina mimba yako!”
Alitamani jibu libadilike na kuambiwa kwamba alikuwa akitaniwa, kile alichoambiwa sekunde chache ziliopita kilikuwa kilekile alichoambiwa kwa mara nyigine tena, akajikuta akitoka chumbani humo na kuelekea sebuleni.
“Kuna nini?” aliuliza Irakoze.
“Hivi unajua misingi ya kania letu?”
“Ndiyo! Ila mtoto ni baraka mpenzi!”
“Haiwezekani! Mtoto si baraka katika maisha yangu! “
Hakukuwa na kitu kilichomchanganya katika maisha yake kama hicho, hakuamini kile kilichokuwa kimetokea kwamba baada ya kufanya sana mapenzi mwisho wa siku msichana wake alikuwa mjauzito.
Wakati mwingine alifikiria kuikataa mimba hiyo ila kila alipona kwamba ndipo kungekuwa na madhara zaidi kwa msichana huyo kutangaza, akaogopa. Kama ilivyokuwa siri katika kipindi cha nyuma, ilitakiwa kuendelea kuwa siri maisha yake yote, iwe isiwe, ilikuwa ni lazima kuhakikisha kwamba jambo hilo halijulikani na mtu yeyote yule.
“Naomba tufanye kitu ili unifiche na aibu hii,” alisema Padri Benedicto huku kijasho chembamba kikianza kumtoka na mwili ukizidi kumtetemeka. Irakoze akamkazia macho.


INAENDELEA...

No comments:

Post a Comment