Thursday 26 March 2015

VIBONZO VYA MTAA


1.    HASIRA HASARA
Sikia kisa cha bwana mmoja ambaye alikuwa mkali sana kwa mke na watoto wake kwa ujumla,
Mkasa ulikuwa hivi yule Bwana aliumwa kiasi cha kuzidiwa sana tu ndiko akapelekwa hospitali na mkewe. Ndipo akatakiwa afanyiwe uchunguzi wa kina kujua nini tatizo linalomsibu.
Daktari akamwambia mkewe kua akalete mkojo toka kwa mumewe wapate mfanyia uchunguzi.Ndipo akaenda akamweleza hilo swala naye mume hakusita akafanya hivyo na kumpatia mkewe huo
Mkojo apate ufikisha kwa daktari, sasa wakati anatoka kwenda kwa daktari bahati mbaya akajikwaa na hatimaye kumwaga ule mkojo wote alokua akipeleka kwa daktari.
Akawaza moyoni mwake
“kwa jinsi mume wangu alivyo mkali ntamwambia nini sasa tena ukizingatia anaumwa “
Alichoamua ni kwenda kuweka mkojo wake binafsi   na kumpelekea daktari kwa uchunguzi ili kuepuka ugomvi na mumewe kisha akarudi kwa mgojwa ili wasubirie majibu toka kwa daktari.
Muda si mrefu daktari akaingia kuwapatia majibu ndipo akaanza kwa kusema
“kutokana na uchunguzi tulio ufanya kwa mgonjwa wetu, mgonjwa anaonekana kuwa ana Ujauzito wa miezi miwili". Mgonjwa akasema naomba rudia kusema hayo majibu?.
Akamwambia vivyohivyo tena kuwa mgonjwa ana ujauzito wa  miezi miwili, ndipo akaamua kuondoka na akawa amepona tokea hapo kutokana na majibu yaliyo msitaajabisha toka kwa daktari.

USHAURI WA BURE
UKALI HAUFAI KABISAAAAAAAAAAAAAA



No comments:

Post a Comment