Sunday 28 January 2018

HADITHI!!!!!!!!!!................. SEHEMU YA KUMI

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 10


Ni kweli walishtuka, hawakuamini kile walichokisikia kwamba mbali na kuwatafuta wanawake waliotakiwa kuwapeleka kwa ajili ya kuigiza filamu, kulikuwa na kazi nyingine ya ziada ambayo iliitwa Biashara ya Kifo.

“Ndiyo inakuwaje hiyo?”

“Ni kazi rahisi tu japokuwa unahitajika umakini wa hali ya juu,” alisema bwana Cook.

Hapo ndipo mzee huyo alipoanza kueleza namna ambavyo biashara hiyo ilitakiwa kufanyika. Kulikuwa na kundi la wanawake mitaani waliokuwa wakihitaji ajira, watu waliokuwa wakitafuta ajira kila siku, mbali na hiyo, kulikuwa na kundi kubwa la wanawake ambao kila siku walitamani kufika nchini Marekani.

Hao ndiyo waliotakiwa kufanyiwa biashara hii. Kazi ilikuwa ni kuwafuata na kuanza kuwalaghai kwa maneno matamu kwa kuwaahidi kwamba wangewapa ajira yenye kiasi kikubwa cha fedha na hivyo wawasafirishe kwenda nchini Marekani, wanapofika huko, walazimshwe kuigiza filamu za ngono, kwa atakayetaka kuendelea basi aendelee lakini kwa wale ambao wangekataa kuendelea na kulilia kurudi nyumbani, basi hao wauawe na kisha kuchunwa ngozi ambayo ingepelekwa nchini China kwa ajili ya kutengenezea vitu vya asili.

“Mmmh!” aliguna Ethan.

“Unahisi ni kazi ngumu?”
“Kwangu! Kuchuna ngozi ya binadamu, sijawahi kufanya kazi hiyo,” alijibu Ethan.

“Kazi yako si kuchuna ngozi, kazi yako kubwa ni kutafuta wasichana tu, hakuna jingine, hiyo ni kazi ya watu wengine,” alisema bwana Cook.

“Kama ndiyo hivyo, hakuna shida.”

Hiyo ndiyo kazi aliyoahidiwa kulipwa kiasi kikubwa cha fedha. Kilichofanyika ni kupewa kiasi cha dola elfu hamsini ambazo zilikuwa ni zaidi ya milioni hamsini, akatengenezewa pasipoti kubwa kwa ajili ya kusafiria nchi hadi nchi na kisha kuanza safari za kuwatafuta wasichana kwa ajili ya kuigiza filamu za ngono.

Safari yao ya kwanza kabisa kwenda ilikuwa nchini Hispania, huko wakakutana na wasichana kadhaa na kuhitaji kufanya nao mahojiano kwa ajili ya kazi za uongo walizowaambia kwamba zilikuwa nyingi nchini Marekani.

“Upo tayari?”

“Kiasi gani?”

“Dola elfu moja kwa siku,” alijibu Ethan.

“Mmmh! Ni kazi gani?”
“Zipo nyingi tu lakini unatakiwa kuchagua. Kuna kazi za hotelini, kupika na nyingine nyingi,” alisema Ethan.

“Nipo tayari!”

“Sawa.”
“Si umesema Marekani?”
“Ndiyo!”

“Hakuna tatizo!”

Kutokana na wimbi kubwa la wasichana wa Ulaya kukosa ajira na kutamani sana kwenda nchini Marekani kwa kuamini kwamba kulikuwa na maisha mepesi, wakakubaliana na Ethan na mwisho wa siku kuelekea huko.

Ishu zote za usafirishaji zilikuwa chini yake, alitumia kiasi kikubwa cha fedha alichopewa na bwana Cook hivyo hakukuwa na tatizo lolote lile. Walipofika nchini Marekani katika Jiji la New York ambapo ndipo kulipokuwa makao makuu ya kampuni hiyo ya filamu za utupu, wakapelekwa hotelini na kuambiwa wasubiri.

“How many are they?” (Wapo wangapi?)

“Ten young girls!” (Wasichana wadogo kumi)

“What do you mean? Below 18?” (Unamaanisha nini? Chini ya miaka kumi na nane?) aliuliza bwana Cook.

“No! Above 18 but below 23,” (Hapana! Zaidi ya miaka 18 lakini chini ya miaka 23)

“Ok!” (Sawa)

Mara baada ya kufika katika hoteli hiyo, wakaambiwa waoge kwa ajili ya chakula cha usiku na siku inayofuata wangeanza safari ya kuelekea katika eneo la kazi, kule walipotakiwa kufanya kazi.

Kila mmoja alikuwa na furaha mno, kutoka nchini Hispania mpaka kufika nchini Marekani, tena kufanya kazi ndogo kwa mshahara mkubwa ilionekana kuwa kama bahati kwao. Sheria moja kubwa waliyokuwa wamepewa ni kutokutumia simu tu.

Waliufurahia usiku huo kwa kuona kwamba ndiyo ilikuwa mwanzo wa safari yao ya kuwa mamilionea mara watakaporudi nchini mwao, hakukuwa na mtu aliyehisi kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na zoezi zima la kuigiza filamu za utupu na kama kungekuwa na yeyote atakayekataa basi ilikuwa ni lazima auawe na kuchunwa ngozi.

“Andikisheni majina yenu na nafasi unazotaka kufanya kazi,” alisema Ethan, alikuwa akiwaambia wasichana hao kumi ambao wakafanya kama walivyotakiwa kufanya.

Siku iliyofuata Ethan akarudi hotelini hapo kisha kuwachukua, akawapeleka katika jumba moja kubwa lililokuwa pembezoni mwa Jiji la New York, aliwaandaa kwa ajili ya kazi aliyotaka kuwapa. Kwa kuwaangalia wasichana wale, walionekana kuwa na furaha kubwa kwa kuamini kwamba huo ungekuwa mwanzo tu kwani hata mapokezi waliyokuwa wamepewa siku hiyo yalikuwa makubwa na ya kifahari.
Wakateremka kutoka garini na kuingia ndani ya jumba moja kubwa, humo wakaambiwa watulie kwani kulikuwa na mtu aliyetaka kuzungumza nao. Wakatulia vitini na Ethan kuelekea chumbani. Baada ya dakika moja akarudi na mwanaume mmoja, alikuwa mtu mwenye umri mkubwa ambapo kwa kumwangalia tu, ungehisi kwamba alikuwa na miaka zaidi ya hamsini.

“Karibuni sana,” aliwakaribisha mzee huyo.

“Asante sana,” waliitikia kwa pamoja.

“Mpo hapa kwa ajili ya kufanya kazi, si ndiyo?”
“Ndiyo!”

“Kazi ipo, ila mmekwishaambiwa ni kazi gani mtakayofanya?”

“Hotelini!”

“Sawa! Ila kwa bahati baya huko kazi imekwisha, iliyobakia ni moja tu,” alisema mzee huyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Gregory.

Wasichana wale walipoambiwa kwamba kazi ya hotelini ambao walikuwa wameifuata ilikwisha, kila mmoja akanyong’onyea lakini walipoambiwa kwamba kulikuwa na kazi nyingine ambayo ilikuwepo mahali hapo, wakarudi kwenye tumaini jipya.

“Kazi gani?”
“Mnajua kuigiza?”

“Mimi najua...” alisema msichana mmoja.

“Hata mimi najua,” alisema mwingine, mwisho kabisa, wote walisema wanajua.

“Nani anamjua Blue Diamond?”

“Mimi simfahamu.”

“Mimi namfahamu! Ni mcheza filamu za utupu,” alijibu msichana mmoja.

“Sawasawa! Blue alikuwa msichana kama nyie, wakati alipotoka nchini Canada, alifikia ndani ya nyumba hiihii, alikuwa masikini sana, lakini tukayabadilisha maisha yake na kuwa tajiri namna hiyo. Tulipomwambia kuhusu kuigiza filamu hizo, aliogopa sana lakini sasa hivi anatushukuru na kutulaumu kwa kuwa tulimchelewa kumwambia juu ya mafanikio makubwa ambayo angeyapata.

“Sasa hivi Blue ni msichana mwenye mafanikio, anaoglelea kwenye bwawa la fedha, anaendesha gari analotaka. Wangapi mpo tayari kuwa kama Blue?” alisema mzee Gregory na kumalizia na swali.

“Kuwa muigizaji wa filamu za utupu?” aliuliza msichana mmoja.

“Ndiyo! Hatukulazimishi kuigiza, hakuna mtu anayelazimishwa kuyafuata mafanikio na utajiri. Huwa tunalipa dola elfu tatu kwa kila kipande kimoja kwenye filamu zetu, kwa maana hiyo ikitokea ukafanya mapenzi na wanaume wawili kwa mpigo, utapata dola elfu sita,” alisema mzee huyo.

Kiasi cha fedha ambacho walitajiwa kilikuwa kikubwa mno zaidi ya milioni sita kwa mtu mmoja na milioni kumi na mbili kama utafanya mapenzi na wanaume wawili kwa pamoja, kila aliyekisikia, alitamani kukipata hapohapo lakini tatizo likawa namna ya kuigiza filamu hizo.  Wasichana hao wakaanza kutoa minong’ono ya chinichini lakini mzee yule aliendelea kuwaambia kwamba ilikuwa ni lazima wafikie mafanikio kama wangekubaliana nae.

Ili kuendelea kuwalaghai, wakawaletea mikataba na kuwawekea mbele yao, walitakiwa kusaini kisha kuandika akaunti zao ili mara watakapoanza kuigiza basi wawekewe kiasi hicho cha fedha.

“Mimi sipo tayari,” alisema msichana mmoja.

“Hata mimi sipo tayari,” alisema msichana mwingine.

“Sawa! Hakuna tatizo!”

“Mimi nipo tayari!”

“Safi sana!”

Kati ya wasichana kumi, wanne walikuwa tayari, wakakubaliana na mzee Gregory kisha kuambiwa wabaki mahali hapo huku wale sita waliokataa wakiambiwa warudi hotelini tayari kwa kujiandaa na safari siku ijayo kurudi nchini Hispania.


Wakasimama na kutolewa nje, wakaingizwa ndani ya gari huku Ethan akiwa pamoja nao. Gari halikwenda hotelini, lilibadilisha njia na kwenda katika jumba jingine kabisa, wao wenyewe walishangaa, hawakujua waliletwa pale kwa ajili gani, wakashushwa na kuingizwa ndani ya jumba lile, lengo kamili lilikuwa ni kuuawa na kisha kuchunwa ngozi, hiyo ndiyo ilikuwa Biashara ya Kifo, walitakiwa kuuawa na ngozi zao kutumwa nchini China ambapo kulikuwa na biashara nzuri tu.

HADITHI!III!!!!!!!!!!............SEHEMU YA TISA

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 09
 Hawakuwa na haja ya gari lile, walikuwa tayari kuliacha lakini wayaokoe maisha yao, hawakutaka kusimama sehemu yoyote ile, waliendelea kusonga mbele kwa kuamini kwamba wangefika sehemu iliyo salama kabisa.

Wakati wamefika umbali urefu, mara wakaanza kuwaona polisi wakiwa mbele yao, tena wakija kwa kasi huku wakiwa na bunduki na mbwa walioonekana kuwa na mafunzo makubwa ya kunusa. Wakati wamebakiza kama hatua mia moja kutoka walipokuwa, wakawaona mbwa wale wakiongeza kasi ya unusaji wao na kuona kwamba iwe isiwe wangeweza kukamatwa.

“Tufanye nini? Turudi tulipotoka au?” aliuliza rafiki yake, Thomson.

“Twende kulia,” alisema Ethan na kuanza kukimbilia upande wa kulia.

Hiyo haikusaidia, mbwa wale waliendelea kuwaongoza polisi kule walipokuwa, tayari waliona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wao. Hawakusimama zaidi ya kuongeza kasi zaidi, hiyo wala haikusaidia kwani kadiri walivyoongeza kasi na ndivyo ambavyo polisi wale waliokuwa na mbwa walipozidi kuwafuata, tena nao wakiongeza kasi.

“Wooo...wooo...wooo...” walisikika mbwa wakibweka.

Japokuwa walikimbia sana tena kwa kasi lakini mwisho wa siku wakajikuta wakikamatwa na kutiwa nguvuni. Hawakuwa na jinsi, wakabebwa na kupelekwa Jijini Texas ambapo huko wakafikishwa kituo cha polisi tayari kwa kupelekwa mahakamni.

“Sikutarajia kama kuna siku ningekamatwa,” alisema Ethan.

“Hata mimi! Ila kosa lilikuwa pia?”
“Hatukujipanga, tulikurupuka tu.”

Kesho yake, wakachukuliwa na kupandishwa mahakamani ambapo huko wakajikuta wakikosa dhamana na hivyo kupelekwa rumande. Baada ya wiki mbili Ethan na mwenzake wakarudishwa tena mahakamani ambapo siku hiyo ilionekana kuwa bahati kwao kwani hakukuwa na shahidi yeyote ambaye alijitokeza na kusema kwamba kweli gari hilo liliibwa, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alisimama kinyume nao na kuweka ushahidi wao ili wahukumiwe, hivyo mwisho wa siku wakajikuta wameshinda kesi ile.

“Siamini,” alisema Ethan huku akionekana kutokuamini macho yake.

Wakawa huru, Ethan akamuahidi rafiki yake huyo kwamba asingeweza kurudia tabia ya kuiba magari tena kwani kwa kile kilichokuwa kimetokea ni Mungu tu ndiye aliyemsaidia mpaka kuwa huru muda huo. Baada ya kila kitu kuihs amahakamani, wakatoka nje.

“Samahani,” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja, alikuwa amemshika bega kwa nyuma, Ethan akageuka.

“Bila samahani.”
“Unahitajika!”

“Wapi? Na nani?”

“Kuna mtu anakusubiri ndani ya gari ile pale.”
“Nani?”
“Twende, utamfahamu tukifika,” alisema mwanaume huyo.

“Twende Thomason....” alimwambia rafiki yake.

“Hapana! Unahitajika peke yako, labda huyu anaweza kusubiri hapa,” alisema mwanaume yule.

Hakuwa na amani kabisa, alikuwa akijiuliza juu ya huyo mtu aliyekuwa akimsubiri ndani ya gari lile. Kwa kuliangalia tu, lilikuwa gari la thamani lililomfanya kuona kwamba mtu aliyekuwa akimiliki gari hilo alikuwa na fedha nyingi.

Hakutaka kusita, alichokifanya ni kuelekea lilipokuwa gari lile, alipolifikia, mlango ukafunguliwa na mwanaume yule kisha kuingia ndani. Kulikuwa na giza, hakukuwa na mwanga, alipokaa kitini, taa zikawashwa na macho yake kutua kwa mwanaume mmoja, hakuwa mgeni machoni mwake, alimfahamu sana, mara ya kwanza kabisa alikutana naye ndani ya ndege na kumpa business card yake, na ndiye yule aliyekuwa akitamani kuwasiliana naye kipindi cha nyuma, alikuwa bwana Boyla Cook.

“Cook!” aliita Ethan kwa mshtuko mkubwa.

“Unaendeleaje Ethan?” aliuliza bwana Cook huku akichia tabasamu pana.”
“Naendelea vizuri, nilikutafuta sana, nilisahau nilipoiweka business card yako, nimefurahi kuonana nawe tena,” alisema Ethan huku akionekana kutokuamini.

“Nimefurahi pia.”

Hapo ndipo bwana Cook alipomwambia kwamba kila kitu kilichoendelea kule mahakamani kilikuwa nyuma yake, alikuwa amepanga kila kitu na ndiyo maana hata mara ya pili alipofikishwa mahakamani pale kesi ilikuwa nyepesi sana kwa kuwa alitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kumtoa katika matatizo aliyokuwa nayo.

Ethan akafurahi sana, akamshukuru mzee huyo lakini hapohapo akaanza kujiuliza juu ya msaada ule, mzee yule alikuwa akihitaji nini.

“Nashukuru sana! Ila kwa nini umenisaidia? Na umejuaje kama nilikamatwa?” aliuliza Ethan.

“Nilikuwa nakufuatilia kila kona, nilikwamba kwamba biashara uliyokuwa ukiifanya haikuwa salama kwani muda wowote ule ungekuwa kwenye hatari. Nilitamani sana kufanya kazi na wewe na ndiyo maana kila ulipokuwa, nilihakikisha nakufuatilia kwa ukaribu.

“Wakati mzee Sanchez amefariki, nilitaka kuja kukuchukua lakini nilikuwa na safari ya kwenda Brazil, hivyo nikaamua kuachana nawe kwa muda. Nimerudi siku kadhaa zilizopita na ndipo nilipotuma vijana wakufuatilie na kujua upo wapi, wakasema umekuja huku Texas na umekamatwa kwa kosa la kuiba gari na kutaka kulivusha mpakani, hivyo nikatuma fedha zisaidie kukutoa ili tufanye kazi,” alisema mzee huyo kwa kirefu.

Ethan akashusha pumzi ndefu, hakuamini kile alichokuwa amekisikia, kumbe wakati yeye akijaribu kukumbuka juu ya kile kikaratasi alichokuwa amepewa chenye namba ya bwana Cook, kumbe naye alikuwa akimfuatilia kwa ukaribu. Mpaka kufikia hatua hiyo tayari akajiona kuwa miongoni mwa watu waliokuwa na bahati kubwa.

“Unataka tufanye kazi gani?” aliuliza Ethan.

“Twende nyumbani, tutaongea mengi,” alisema bwana Cook.

“Siwezi kwenda peke yangu, si unajua nina mwenzangu,” alisema Ethan huku akimwangalia rafiki yake, Thomson dirishani.

“Mwambie aje,” aliagiza mzee huyo.

Hapohapo Thomson akaitwa na kisha kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwa mzee huyo. Kichwa cha Ethan bado kiliendelea kujiuliza maswali juu ya kazi aliyotakiwa kufanya kwa mzee huyo. Hakuijua ilikuwa ni kazi gani lakini kwa sababu alionyeshewa msaada mkubwa, hakuwa na jinsi, alijiona lingekuwa suala la busara kama angekubaliana naye.

Safari ile ikaishia mbele ya jumba moja la kifahari, kwa kuliangalia wala usingejiuliza maswali kwamba jumba hilo lilikuwa likimilikiwa na mtu mwenye fedha, mtu aliyekuwa na zaidi ya dola bilioni kumi katika akaunti yake. Geti likafunguliwa na kisha gari kuingizwa.

Lilikuwa jumba kubwa lililosheheni vitu vyote ambavyo vilitakiwa kuwa ndani ya jumba la bilionea fulani, kulikuwa na bwana kubwa la kuogelea ambalo sakafu yake ilikuwa ni ya kioo, kulikuwa na mbuga ndogo ya wanyama na kwa mbali kulionekana kuwa na wanyama fulani na ndege wengi, kulikuwa na magari ya kifahari na vitu vingine, ukiachana na hivyo, kulikuwa na masanamu manne ya kike yaliyoonekana kuwa uchi kabisa.

Milango ya gari ikafunguliwa na kisha kuteremka, wakaanza kupiga hatua kuelekea ndani. Muda wote huo Ethan na Thomson walikuwa wakiangalia huku na kule, kila kitu kilichoonekana kwao kilionyesha ni kwa namna gani bwana Cook alikuwa mtu tajiri aliyeogelea fedha.

Walipojingia ndani, kitu cha kwanza kabisa walichokutana nacho ni picha za wanawake wengi zilizokuwa zimebandikwa ukutani, walikuwa watupu kama walivyozaliwa, walikaa katika mapozi tofautitofauti na walikuwa wanawake wa kila asili.

Ethan aliziangalia picha zile, hakuelewa ni kwa nini zilikuwa mahali hapo, ziliusisimua mwili wake kwani kilipita kipindi kirefu hakuwahi kukutana kimwili na mwanamke yeyote yule. Alizunguka huku na kule, macho yake yalikuwa yakiangalia kila kona.

“Mbona kuna picha nyingi sana za wanawake?’ aliuliza Ethan.

“Ninapenda kuwa nazo.”
“Ndiyo ziwe nyingi namna hii?”
“Yeah! Huwa ninafurahia ninapomwangalia mwanamke akiwa mtupu.”
“Mmmh!”

“Ndiyo hivyo! Karibuni sana,” alisema bwana Cook huku akiachia tabasamu pana.

Wakakaa kwenye makochi ya manyoya na kutulia. Wote wawili walikuwa wakiangalia huku na kule, bwana Cook akatoka sebuleni hapo na kuelekea chumbani kwake, baada ya dakika tatu akarudi huku akiwa amebadilisha nguo zake, akaagiza vinywaji, vikaletwa na kuanza kunywa.

“Ninataka unifanyie kazi Ethan,” alisema bwana Cook.

“Kazi gani?”

“Kwanza unajua mimi ni nani?”
“Unaitwa Boyle Cook, sijui kingine zaidi ya hicho,” alijibu Ethan.

“Sawa. Hujawahi kulisikia jina langu sehemu yoyote?”

“Hapana!”

“Mimi ni mkurugenzi wa kampuni ya kutengeneza filamu za utupu ya Bravilian.sex, ni kampuni inayojitegemea na ambayo imetengeneza filamu nyingi mno,” alisema bwana Cook.

“Sawa! Nimefurahi kukufahamu! Kwa hiyo unataka na mimi niigize?”

“Ungependa kuigiza?”
“Hapana! Siwezi kabisa.”
“Sawa! Lengo la kukuita hapa si kutaka uigize bali kuna kazi nyingine nataka uifanye,” alisema bwana Cook.

“Kazi gani?”
“Kunitafutia wasichana wengi duniani kwa ajili ya kuigiza, kila msichana nitakulipa dola elfu kumi,” alisema bwana Cook.

“Mmmh!”

“Ni kazi ngumu?”

“Si sana, kama nitapewa fedha za kutosha kuzunguka duniani, si kazi ngumu, hakuna tatizo,” alisema

“Ila kuna kazi nyingine nataka ufanye, ila kwa siri sana.”
“Kazi ipi?”

“Biashara ya Kifo,” alisema bwana Cook, Ethan na Thomson wakashtuka.

INAENDELEA...                       


Friday 26 January 2018

HADITHI SEHEMU YA NANE

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 08


Biashara ilimwendea vizuri, japokuwa hakuwa bosi lakini kwa kiasi fulani kila kitu kilikwenda kama alivyokuwa akitaka. Yeye ndiye alikuwa msafirishaji mkuu wa madawa hayo kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Aliaminika mno kwa kuwa kila mzigo aliokuwa akitumwa ulifika salama mikononi mwa mtu aliyekuwa akihitajika kuupata mzigo huo. Siku zikaendelea kukatika, akaanza kuwa na maendeleo makubwa lakini tatizo lilikuja pale alipoanza kufanya starehe.
Kiasi kikubwa cha fedha alichokuwa akikipata kutoka katika biashara zile, alikiweka katika mstari wa starehe zake. Kila siku Ethan alikuwa mtu wa kubadilisha wanawake na kubadilisha viwanja kiasi kwamba kiasi cha fedha alichokuwa akikipata wakati mwingine hakikutosha kabisa.
Alisahau alipotoka, alisahau kama kule Manhattan alipokuwa kulikuwa na rundo la watoto masikini, watu wasiojiweza ambao kila siku maisha yao yalikuwa pembeni ya mapipa ya takataka. Alisahau kila kitu, aalichokuwa akikifanya kwa wakati huo kilikuwa ni starehe tu.
Wanawake walimopapatikia kwa kuwa hakuwa mchoyo, alichokuwa akikipata aligawana nao na hivyo kutengeneza jina kubwa masikioni mwao. Siku zikakatika na kukatika mpaka pale aliposikia taarifa kwamba bosi wake aliyekuwa akimuweka mjini, bwana Sanchez alikuwa hoi kitandani.
Kilichomlaza kilikuwa ni saratani ya damu, alikuwa akiugua kila siku kwa kutokwa na damu puani na mdomoni. Ugonjwa huo ulimuanza kwa kasi hali ambayo ilimfanya kupelekwa hospitali ambapo madaktari wakawaambia ndugu zake kwamba asingeweza kupona.
“Hawezi kupona ugonjwa huu, ni lazima afe,” alisema daktari, aliamua kuwaambia ukweli kwamba mgonjwa waliyekuwa wamempeleka ilikuwa lazima afe.
“Hawezi kupona?”
“Hawezi. Ni lazima afe.”
Kansa yake ilisababishwa na ubwiaji mkubwa wa madawa ya kulevya, hakuwa na nafuu hata kidogo walichokifanya ndugu zake ni kumchukua na kumrudisha nyumbani kumuuguza katika kipindi cha mwisho.
Walipomfikisha huko, wakamfungia chumbani kwake. Hawakutaka kumuacha hata kidogo na hawakutaka kumficha juu ya kile alichokisema daktari kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kufa hivyo kama alitaka kufanya vitu vyake kwa mara ya mwisho, alitakiwa kufanya kwa wakati huo.
“Nitagawa utajiri kwa watoto wangu! Niitieni mwanasheria wangu,” alisema bwana Sanchez.
Mwanasheria wake akaitwa na kisha kuandika kile alichotakiwa kuandika, mirathi ikagaiwa kwa watoto wote. Kitu ambacho hakukiamini Ethan ni kwamba hakukuwa na mali yoyote aliyoachiwa japokuwa yeye alikuwa mtu wa karibu sana na mzee huyo.
Bwana Sanchez alipofariki hapo ndipo maisha yalipomgeukia, akaanza kurudi kule alipotoka, bisahara zikakata, mitego yote aliyokuwa ametega ikaharibika vibaya, marafiki zae ambao kila siku alifanya nao starehe wakamkimbia kwani waliona kwamba hakuwa na kitu tena.
Aliogopa kurudi New York katika mtaa aliozaliwa kwa kuhisi kwamba bado alikuwa akitafutwa sana, hivyo alichokifanya ni kukimbilia Texas, sehemu iliyokuwa na mpaka mkubwa wa kuingilia nchini Mexico.
Huku akiwa huko ndipo alipokumbuka kwamba mara ya mwisho alikutana na mzee mmoja ndani ya ndege ambaye alimwambia sana kuhusu biashara ile ya madawa kwamba haikuwa nzuri hivyo alitakiwa kuachana nayo.
“Namba yake niliiweka wapi?” alijiuliza.
Hicho ndicho kilichomuumiza kichwa wakati huo, hakukumbuka mahali alipoihifadhi namba ile, alikumbuka vilivyo kwamba alipewa na kurudi nayo nyumbani, baada ya hapo, hakukumbuka aliiweka wapi kwani kilipita kipindi kirefu mno na hata kumbukumbu zake zikawa zimepotea kabisa.
“Nilirudi nyumbani nikiwa nacho, nikakaa kitandani, baada ya pale nilikiweka wapi? Mhh! Hapana! Mbona sikumbuki vizuri?” alijiuliza lakini akakosa jibu.
Aliendelea kupigika mitaani, maisha yakampiga sana. Alipoona kwamba kila kitu kinakwenda kombo hapo ndipo alipoingia katika biashara ya kuuza magari, yaani walikuwa wakiiba magari nchini Marekani, wanayapitisha kwa njia za panya kuelekea Mexico na kuyauza huko.
Hakuwa na jinsi, japokuwa ilikuwa ni kazi ya hatari iliyohatarisha maisha yake lakini hakuwa na jinsi, alitakiwa kupambana ili atoke katika umasikini mkubwa uliompigia hodi mlangoni. 
“Ushawahi kuiba Lambonghin?”
“Hapana!”
“Sasa leo tunakwenda kuiiba, kama tukifanikiwa, sisi matajiri,” alisema jamaa yake, walikuwa wezi wakubwa hapo Texas.
“Hakuna noma, ila hatuwezi kukamatwa?”
“Tutakamatwa vipi? Kama tumewahi kuiba magari zaidi ya mia tano, tutakamatwaje kwa gari moja?” aliuliza rafiki yake huyo.
“Basi sawa. Lipo wapi?”
Huo ndiyo mpango waliopanga siku hiyo, walitaka kuiba gari ya thamani na kisha kuisafirisha kwa njia za panya mpaka nchini Mexico. Kuhusu kuiba, hilo wala halikuwa tatizo kabisa, waliweza kufanya hivyo ila kazi kubwa waliyokuwa nayo mahali hapo ni kulitoa gari hilo sehemu lilipokuwa na kulipeleka huko walipotaka kulipeleka.
Saa mbili usiku wakakutana karibu kabisa na ukumbi mmoja wa starehe, mbele yao kulikuwa na magari mengi lakini miongoni mwa magari hayo, kulikuwa na gari moja la thamani sana lililokuwa na gharama zaidi ya dola mioni tano, zaidi ya bilioni moja, ilikuwa lambonghin nyekundu iliyoonekana kuwa mpya kabisa.
Walikuwa wazoefu wa kuiba magari, hata kuiba gari hilo wala haikuwasumbua kabisa. Kwa sababu Ethan alikuwa mtaalamu mkubwa wa kuendesha magari, akakaa sehemu ya dereva, kwa kutumia utundu kwa kuunganisha nyaya, wakaunganisha na gari kuwaka, kilichobakia ni sauti za watu huko nyuma.
Hapo ndipo walipoanza safari ya kuelekea mpakani kwa njia za panya ili waweze kuliingiza gari hilo nchini Mexico. Walipanga kwamba huo ndiyo ungekuwa wizi wao wa mwisho hivyo baada ya hapo wangeacha kabisa kwani ilikuwa moja ya kazi ya hatari kabisa kuwahi kuifanya.
“Hivi unakanyaga mafuta kweli?” 
“Ndiyo!”
“Upo ngapi hapo?”
“180 kwa saa!”
“Gari mwisho ngapi?”
“400 kwa saa!”
“Sasa hizo nyingine unamuachia nani?”
“Ebwana tutakufa.”
“Kama kufa acha tufe, kuna raha gani ya kuishi, kama kufa tutakufa hata ukiendesha 1 kwa saa, kanyaga moto kaka,” alisema rafiki yake.
Mwendo aliokuwa akiendesha ulikuwa ni wa kasi mno, gari lilikuwa likijiweza kwa kasi hivyo Ethan hakuwa na jinsi, akaanza kukanyaga mafuta mpaka kuhisi kwamba gari hilo lingeweza kupaa. 
Kutokana na kuwa usiku mwingi, barabarani hakukuwa na magari kabisa, walitembea kwa mwendo waliotaka tena kwa kasi zaidi na baada ya masaa mawili walitaraji kufika karibu na mpaka huo ambapo wangechukua njia za panya na kuingia Mexico.
Wakati wamebakiza kilometa tatu kabla ya kuingia katika kituo cha mafuta cha Gapco, kwa mbali wakaanza kuyaona magari ya polisi yakiwa yamesimama barabarani huku taa zikiwaka.
Kwanza wakaogopa, kwa kasi waliyokuwa wakienda nayo walijua kwamba endapo wangeyagonga magari yale basi ingekuwa kifo chao hivyo alichokifanya Ethan ni  kupunguza kasi na kisha kuchukua barabara nyingine ya vumbi, magari yale ya polisi yakawashwa na kanza kuwafuata.
“Kanyaga mafuta!”
“Haiwezekani! Hakuna lami huku,” alisema Ethan.
Walikwenda na gari hilo kwa umbali mrefu mpaka mafuta yalipowaishia. Hawakuwa na jinsi, wasingeweza kubaki na wakati polisi waliendelea kuwasogelea kule walipokuwa, walichokifanya ni kuteremka na kisha kuanza kukimbia huku wakiwa wamelitelekeza gari lile.
Walikimbia kwa umbali mrefu, mbele kabisa wakakutana na korongo kubwa, lilionyesha kwamba mchana huwa kunakuwa na watu wanaochimba kokoto kutokana na ardhi ya Texas kuwa na kokoto nyingi, walichokifanya ni kuingia katika korongo lile na kuendelea na safari yao.
Hawakutaka kusimama sehemu yoyote ile, walichokuwa wakikitaka ni kufika walipotaka kufika pasipo kugundua kwamba polisi wale wa nyuma walipoona wezi wale kule walipokimbilia, wakawasiliana na polisi wa mpakani na kuwapa taarifa, nao wakaanza kusogea kule walipoambiwa wezi wale walipokimbilia, kwa maana hiyo, kadiri Ethan na rafiki yale walivyokuwa wakipiga hatua, ilikuwa ni sawa na kuwasogelea polisi hao waliotoka mpakani.


INAENDELEA...

HADITHIIII...........SEHEMU YA SABA

BIASHARA  YA KIFO

SEHEMU YA 7.

 “Ethan, stop,” (Ethan, acha) ilisikika sauti ya mama yake kutoka nyuma.
Ethan hakutaka kuiachia bunduki ile, alikuwa amedhamiria kumuua baba yake wa kambo, hakumpenda kabisa, alimchukia mno, kitendo cha kumuona kila siku katika maisha yake kilimkasirisha.
Alijiandaa kumfyatulia risasi na kumuua kabisa, lakini hata kabla hajafanya hivyo, mama yake akamsogelea na kisha kumzuia kubonyeza kitufe cha bunduki ile. Hiyo ikaonekana kuwa bahati ya mtende kwa mzee George, kwa jinsi alivyomwangalia Ethan, alikuwa amedhamiria kumuua kabisa.
Ethan akaondoka mahali hapo, kundi lile la watu lililokuwa limewazunguka nao wakaondoka kuendelea na kazi zao kama kawaida. 
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, alichukiwa na kila mtu kwa kuwa alikuwa mtemi, japokuwa alikuwa na miaka kumi na sita lakini tayari Ethan alijifunza maisha ya mitaani hasa ya kutumia bunduki katika maisha yake.
Alikuwa mtu wa fujo, alijulikana sehemu kubwa hapo Manhattan huku akianzisha kundi lake kubwa la kihuni lililojulikana kama The Mobb. Lilikuwa na vijana ishirini, walioshindikana katika maisha yao, walikuwa watumiaji wazuri wa bunduki, walikuwa wavuta bangi na hata wakati mwingine kutumia madawa ya kulevya.
Walikuwa vijana wadogo lakini wale ambao hawakuwa na huruma hata kidogo. Polisi wa hapo Manhattan waliliogopa kundi hili, hawakuyathamini maisha yao, kwao, kupigwa risasi na kufa lilikuwa jambo jema tu kwani waliamini kwamba kulikuwa na mungu wao wa kisela ambaye angewpokea nakuwaingiza katika mbingu yao iliyokuwa na makontena makubwa ya madawa ya kulevya na bangi.
Wakati kundi hilo likiendelea kukua, likiwapiga watu na hata wakati mwingine kuwaua, hapo ndipo walipotumwa polisi waliokuwa na hasira, polisi waliotoka nje ya Manhattan kwa ajili ya kufanya jambo moja tu, kuwakamata vijana hao na hata kama wataleta ubishi au kufanya chochote kilicho kibaya cha kuhatarisha maisha yao, basi wawaue.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kumaliza magenge hayo, vijana wengi walikamatwa na kufungwa gerezani lakini kwa Ethan, akatoroka jijini New York na kuhamia Washington DC ambapo maisha yake yakaendelea.
Hakutaka kuwa mhuni kama alivyokuwa, hakutaka kufanya usela wa mitaani alichokifanya kwa wakati huo ni kujikita katika uuzaji wa madawa ya kulevya kwa kuyasafirisha sehemu moja kwenda nyingine. 
Hapo ndipo alipokutana na wale watu aliokuwa akiwasikia kwamba walikuwa wauzaji wazuri wa madawa ya kulevya na walikuwa watu wenye kuogopwa sana. Alipofikishwa kwa mzee mmoja aliyekuwa na asili ya Mexico, mzee Sanchez El Paso, akamchukua na kumfanya mfanyakazi wake ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kusafirisha madawa nchini Marekani.
“Ukifanya kazi na mimi, utakuwa tajiri mno,” alisema mzee Sanchez.
“Nitatajirika vipi?”
“Utafahamiana na watu wengi, nisingependa ufanye kazi kwangu milele, pia ningependa baadaye ufanye kazi wewe kama wewe,” alisema mzee Sanchez.
“Ili nifikie ndoto ya kufanya biashara zangu mwenyewe, natakiwa kufanya nini?”
“Kujitoa kazini, hakuna cha zaidi, ila epuka sana wizi, ukiiba na kugundulika, nitakuua,” alisema mzee huyo maneno yaliyomtia hofu mkubwa.
“Siwezi kufanya hivyo! Umenitoa mbali, hakika nitaendelea kukuheshimu na sitokufanyia ujinga,” alisema Ethan.
Alimheshimu mzee huyo kwa kuwa ndiye aliyekuwa akimfanyia mambo mengi na kukutana na watu ambao hakutegemea kukutana nao katika maisha yake. Kila siku alikuwa mtu wa kutoka, hakutulia sehemu moja, leo alikuwa akienda California, kesho Texas na kesho kutwa sehemu nyingine.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, kila siku alikuwa akibadilisha muelekeao wake ambapo kote huko kazi kubwa aliyokuwa akiifanya ni kusafirisha madawa ya kulevya tu. Jina lake likaanza kukua, mnyororo mkubwa aliokuwa nao mzee Sanchez ukamsaidia mno na hata katika viwanja vya ndege mbalimbali hakuwa akipata usumbufu wowote ule.
“What do you want?” (Unataka nini?) aliuliza mzee mmoja.
“What do I want? What do you mean?” (Nahitaji nini? Unamanisha nini?)
“For how long have you been doing this work?” (Kwa kipindi gani umekuwa ukifanya kazi hii?)
“Three years?” (Miaka mitatu)
“Ok!” (Sawa)
Alikuwa akizungumza na mzee mmoja aliyekuwa amekaa naye ndani ya ndege. Hakujua ni nani alimwambia kuhusu biashara ya madawa ya kulevya aliyokuwa akiifanya, mzee huyo alianza kumuuliza maswali mengi kiasi kwamba akaanza kuogopa kwani hata humo ndani ya ndege alipokuwemo, alikuwa na mzigo mkubwa aliokuwa akiupeleka Los Angeles.
“Lakini wewe ni nani?” aliuliza Ethan huku akionekana kushikwa na hofu.
“Ninaitwa Boyle Cook,” alijibu mzee yule.
“Umejua vipi kama ninafanya kazi hii?”
“Hauwezi kunificha, ninawajua kwa kuwaangalia, umekuwa na amani katika kufanya kazi hii?” aliuliza bwana Cook.
“Kiasi, si sana, wakati mwingine unakuwa na hofu kubwa.”
“Utakuwa tayari kama nikikupa kazi nyingine, nzuri tu?”
“Kazi gani?”
“Ninataka uwe na amani, siwezi nikakupa kazi ngumu. Niambie, upo tayari?” aliuliza bwana Cook.
“Mmmh!”
“Usijali! Chukua hii, ukiwa tayari niambie,” alisema bwana Cook na kisha kumpa business card yake iliyokuwa na mawasiliano yote.
Mpaka kufikia hatua hiyo Ethan alichanganyikiwa, alikuwa akimwangalia mzee huyo mara mbilimbili, hakumfahamu alikuwa nani, hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana naye, tena walizungumza kwa muda mchache kabla ya mzee huyo kubaki kimya mpaka ndege ilipotua Jijini Los Angeles na kisha kuteremka.
Hawakuzungumza chochote kile, kila mmoja akaendelea na kazi zake zilizomleta ndani ya jiji hilo la starehe. Ethan akaondoka na kupeleka mzigo alipoelekezwa kwani hata kuutoa pale uwanja wa ndege hakukuwa na kazi kubwa kwani kila kitu kiliwekwa tayari.
Kichwa chake kikawa na maswali mengi, alikuwa akijiuliza kuhusu mzee yule ambaye alionekana kumfahamu mno, hakuishia hapo, aliendelea kufikiria hata ile kazi aliyotaka kumpa, hakujua ilikuwa kazi gani ila alimwambia kwamba endapo angekuwa tayari basi amtafute.
Uuzaji wa madawa ya kulevya ilikuwa biashara mbaya na yenye hatari mno lakini hakutaka kuiacha kwani ilimpa kisasi fulani cha fedha na kuanza kuyabadilisha maisha yake. Alichokifanya ni kumpuuzia bwana Cook na yeye kuendelea na maisha yake kama kawaida ingawa mara nyingi mno alikuwa akijiuliza kuhusu mzee yule na kukosa jibu.


INAENDELEA...

Wednesday 24 January 2018

HADITHI!!!......SEHEMU YA SITA

BIASHARA YA KIFO
Sehemu ya 06


Maisha yaliendelea kama kawaida. Hakukuwa na kitu kilichokisumbua kichwa cha padri Benedicto kama kumuona mzazi mwenzake akiishi mbali naye. Hakuwa na uwezo wa kwenda kukaa naye lakini kila siku alikuwa mtu wa kutamani kumuona mwanamke huyo akiwa karibu naye kwani ndiye mtu pekee aliyeonekana kuwa faraja katika maisha yake.
Kutokana na mapenzi mazito aliyokuwa nayo juu yake, muda wote alihisi kwamba alikuwa akiibiwa tu. Aliwafahamu vijana wa Sinza, walikuwa vijana makini kuhusu masuala yote ya mapenzi, walikuwa na uwezo mkubwa wa kumteka msichana yeyote hata kama angekuwa mgumu kiasi gani.
Hakutaka kusalitiwa, alitaka Irakoze awe wake peke yake, hivyo alichokifanya ni kuanza kupanga mipango kabambe ya kumbana mwanamke huyo kwa kumpeleka katika Chuo cha Utawa,  St. Mary’s Catholic kilichokuwa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam na kuingia pale kama mpishi.
Mipango yote ya Irakoze kuingia ndani ya chuo kile ilifanywa na padri Benedicto huku akimchukua Annabel na kumpeleka nchini Marekani kwa ajili ya kusoma huko katika Shule ya Consolatha Seminary School iliyokuwa katika Jiji la New York nchini Marekani.
Kidogo moyo wake ukawa na amani, kutokana na umbo lake kuwa dogo na sura ya kitoto aliyokuwa nayo, mara baada ya kufika katika chuo hicho cha Utawa, masista wote walihisi kwamba Irakoze alikuwa msichana mdogo, hivyo wakamchukulia hivyohivyo.
Kila siku alikuwa hapo huku akiwasiliana na padri Benedicto simuni, bado wawili hao waliendelea kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa siri sana kiasi kwamba hakukuwa na mtu yeyote aliyefahamu kilichokuwa kikiendelea.
Huo ulikuwa mwaka wake wa kwanza chuoni hapo, alionekana kuwa mtu mwenye heshima, alimheshimu kila mtu kuanzia wale wa chini mpaka wa juu. Wasichana wengi waliokuwa chuoni hapo walimpenda Irakoze ambaye walipenda kumuita kwa jina la Sista Magdalena.
Siku zikaendelea kukatika, kila alipokuwa akitumwa mjini kwa ajili ya kununua baadhi ya vitu kwa ajili ya shule hiyo, alikuwa akienda na kuonana na padri Benedicto na kisha kulala wote hata kwa masaa mawili kisha kurudi chuoni.
Huko ndipo alipopata taarifa kuhusu binti yake aliyekuwa nchini Marekani. Masomo yaliendelea vizuri na mara kwa mara safari za Benedicto kuelekea nchini Marekani hazikuisha, kila alipokwenda, alihakikisha anaonana na binti yake na kisha kurudi nchini Tanzania.
“Amekua sana, mwaka wa sita huu,” alisema Benedicto, alikuwa akimwambia Irakoze.
“Nina kiu ya kumuona.”
“Usijali! Ila nataka tuifanye kitu kimoja”
“Kipi?”
“Na wewe usomee utawa!”
“Mmmh!”
“Hakuna tatizo! Utafanikiwa tu, nataka uwe na safari za kutosha kwenda Ulaya na sehemu nyingine,” alisema Benedicto.
“Sawa! Hakuna tatizo!”
Hilo ndilo walilokuwa wamekubaliana, ilikuwa ni lazima Irakoze aanze kusomea utawa ndani ya chuo hicho alichokuwa akifanya kazi kama mpishi. Hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu tayari alikwishafanya kazi hiyo kwa miaka mitatu, akachukuliwa na kuanza masomo moja kwa moja.
Kila siku alikuwa akiamka asubuhi na mapema kama wanachuo wengine na kisha kuelekea kanisani ambapo walisali kisha kujiandaa na masomo kama kawaida. Japokuwa hakuwa amesoma sana kipindi cha nyuma lakini uwezo wake wa kawaida ulitosha kabisa kuonyesha kwamba kama angeendelea zaidi basi angeweza kufanikiwa sana katika maisha yake.
Aliishi kama mtumishi wa Mungu, kila wakati alikuwa mtu wa kusali huku rozali ikiwa shingoni mwake. Kila mtu alimheshimu na alipoonekana kwamba yeye ndiye alikuwa mcha Mungu mkubwa kuliko wengine, wakampa uongozi wa bweni pasipo kujua kwamba mwanamke huyo alikuwa na mtoto ambaye alikuwa akisoma nchini Marekani.
Padri Benedicto hakuacha, kwa kuwa katika kila hatua aliyokuwa akipitia Irakoze ilikuwa chini yake, hivyo alihakikisha kwamba hata kwenda nje ya chuo hicho linakuwa jambo jepesi ili mradi mwisho wa siku aweze kuonana naye na kufanya mambo yao.
Alichokifanya ni kukaa chumbani na kuandika barua, alikuwa akiuandikia uongozi wa chuo hicho kwamba kutokana na heshima aliyokuwa nayo Irakoze, aliruhusiwa kila Jumapili kwenda kusali nje ya chuo hicho.
Nafasi hiyo haikutolewa mara kwa mara, ilitolewa mara chache sana tena kwa wanachuo walioonekana kuwa na nidhamu ya hali ya juu. Kwa Irakoze hakukuwa na mtu aliyeonekana kuwa na wasiwasi, jinsi nidhamu yake ilivyokuwa chuoni hapo, ilimfanya kila mmoja kukubaliana na padri Benedicto kutokana na jinsi alivyokuwa chuoni hapo.
Hiyo ndiyo ilikuwa nafasi nyingine na waliitumia vilivyo kuwa pamoja. Kila kitu kilichokuwa kikifanyika kiliendelea kuwa siri kubwa. Baada ya miaka miwili kukatika, hatimaye aliyekuwa Kardinari wa Kanisa la Kiroma nchini Tanzania, Paulo Alonso akafariki dunia na hatimaye barua kuandikwa kutoka Vatican kwamba Padri Benedicto alitakiwa kutawazwa na kuchukua nafasi hiyo kwani kwa sifa zote za kuwa kardinari alikuwa nazo.
“Lakini kwa nini apewe padri? Kwa nini asipewe askofu?” maaskofu waliulizana tu.
“Hata sisi hatufahamu, ila kwa sababu ni barua iliyoletwa kutoka Vatican, hatuna budi, acha tukubaliane nayo,” alisema askofu mmoja.
Baada ya wiki mbili, padri Benedicto alitakiwa kuelekea nchini Vatican kwa ajili ya kutawazwa na hatimaye kuwa kardinari mkubwa nchini Tanzania. Hiyo ilikuwa nafasi yake pekee, moyo wake ulikuwa na furaha kubwa, hakukuwa na kitu kilichowahi kumpa furaha maishani mwake kama kipindi hicho.
Suala la kuwa na mtoto liliendelea kuwa siri yake, hakutaka mtu yeyote afahamu na alikuwa akijitahidi kufanya kila liwezekanalo kusiwe na mtu yeyote anayelifahamu hilo. Kwenye kila mwaka, alikuwa akimtumia mtoto wake Annabel kiasi cha fedha kwa kutumia akaunti nyingine kabisa iliyosomeka kwa jina la Andrew McDonald, raia kutoka nchini Kenya.
Japokuwa Annabel katika kipindi hicho alikuwa na miaka kumi, lakini aliendelea kufichwa kwamba baba yake alikuwa padri ambaye katika kipindi hicho alitarajiwa kutawazwa na kuwa kardinari nchini Tanzania.
“Unataka kuwa nani ukikua?” aliuliza Benedicto.
“Nataka kuwa mwanasheria.”
“Kwa nini usiwe sista?”
“Sitaki! Nitataka niolewe. Nimesikia kwamba sista haolewi! Kweli baba?”
“Ndiyo!”
“Basi mimi nataka kuwa mwanasheria, ninataka kuolewa baadaye!”
Alikuwa akizungumza na binti yake katika kipindi alichokwenda kumtembelea nchini Marekani. Japokuwa alikuwa nchi nyingine lakini kofia aliyokuwa ameivaa haikutoka kichwani mwake. Shule hiyo aliyompeleka binti yake kusoma ilimtunza vizuri, alipata malezi yote na hakukuwa na shida sana kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akifika hapo na kumuona.
Annabel alikuwa binti mzuri, mwenye sifa zote za kuitwa mrembo. Alichanganyikana, alikuwa na sura ya baba yake lakini pia alikuwa na sura ya mama yake. Watu wengi waliokuwa wakimuona, walikiri kwamba binti huyo angekuja kutikisa sana siku za usoni kutokana na urembo wake huo.
“Baba!”
“Naam!”
“Unafanya kazi gani?”
“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Kwani sijawahi kukwambia binti yangu?”
“Hapana! Hukuniambia!”
“Mimi ni mfanyabiashara binti yangu, huwa nasafirisafiri sana,” alijibu Benedicto.
“Kweli baba?”
“Ndiyo! Nikitoka hapa, nakwenda Dubai, nikuletee zawazi gani nikija?”
“Chochote upendacho baba, nitafurahi!” alisema Annabel.
Benedicto hakuwa na jinsi, ni kweli alimpenda binti yake lakini kulikuwa na vitu ambavyo hakutakiwa kuwa mkweli kabisa, alimdanganya kwamba alikuwa mfanyabishara kwa kuwa hakutaka ajue kwamba alikuwa padri ambaye hakutakiwa kuoa au kuwa na mtoto yeyote yule.
Kwake, bado lile liliendelea kuwa siri kubwa, kila siku lilimuumiza moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi, alikubaliana na kila kitu kilichokuwa kiiendelea, na hata kama alifanya dhambi, aliamini kwamba hakukuwa na mwanadamu aliyekuwa mkamilifu mbele za Mungu.
Baada ya siku tatu, akarudi nchini Tanzania ambapo moja kwa moja akawasiliana na Irakoze na kumwambia kuhusu mtoto wao na ndoto aliyotaka kuwa nayo katika maisha yake.
“Kakataa kuwa sista?”
“Amekataa!”
“Daaah! Ngoja niende, nitazungumza naye,” alisema Irakoze.
“Hakuna tatizo!”
Japokuwa aliamini kwamba binti yake angeweza kumsikiliza na hatimaye kukubaliana nao kuwa sista lakini hilo halikuwezekana, bado msimamo wa Annabel ulikuwa ni kuwa mwanasheria mkubwa duniani.
Hakukuwa na mtu aliyemzuia, waliachana naye, aendelee na maisha yake na mwisho wa siku kukamilisha kile alichokuwa akikitaka.
Wakati Annabel akifikisha miaka kumi na sita, alionekana kuwa binti mrembo mno, kipindi kirefu cha maisha yake alikitumia nchini Marekani, hakuwahi kurudi nchini Tanzania, aliondoka huko miaka mingi iliyopita, tangu alipokuwa na miaka minne.
Hakufahamu sehemu yoyote nchini Tanzania, hakufahamu mitaa na hata watu wa huko walikuwa na utamaduni gani. Baada ya kufikisha miaka hiyo, hakutaka kukaa nchini Marekani, alitaka kuwa na muda wa kurudi nchini Tanzania ili aweze kukaa na wazazi wake ambao hakuwahi kukaa nao hata siku moja.
Alitaka malezi yao, alichokifanya ni kuwasiliana nao, hawakuwa najinsi, wakajipanga kwamba mara binti yao atakapofika nchini Tanzania, wampelekea katika nyumba yao nyingine iliyokuwa Kisarawe, pembezoni mwa Jiji la Dar es Salaam ambapo waliamini kwamba hakukuwa na watu wengi.
Siku ya safari ilipofika, Annabel akaingia ndani ya ndege tayari kwa kurudi nchini Tanzania. Hapo Marekani akapanda ndege ya Shirika la Ndege la American Airlines ambayo ilikuwa ikifanya safari mpaka nchini Uingereza, Italia na baadaye kuelekea Uholanzi ambapo huko wangebadilisha ndege na kuelekea Dubai, kisha India na Kenya jijini Nairobi na kuingia nchini Tanzania kabla ya kuelekea Afrika Kusini.
Baada ya abiria kutakiwa kuingia ndani ya ndege hiyo, Annabel akasimama na kuanza kuelekea ndani ya ndege hiyo. Kwa muonekano, alionekana kuwa binti mkubwa, mrembo, mwenye mvuto ambaye alivutia sana, kila mwanaume aliyemwangalia, alitamani kuwa na msichana mrembo kama alivyokuwa.
Wakati ameingia ndani ya ndege hiyo na kukaa katika viti vya watu wawili, akaja mwanaume mmoja, alionekana kuwa kijana mtanashati, aliyependeza, alivalia suti ya gharama, muda wote uso wake ulionekana kuwa na tabasamu pana, alimuona Annabel, tabasamu likaongezeka usoni mwake.
“How are you cute,” (Habari yako, mrembo) alimsalimia Annabel.
“I’m fine, you are welcome,” (Salama, karibu) alimkaribisha mwanaume yule aliyejitambulisha kwa jina la Ethan Dylan.

INAENDELEA...